STARTV: Maamuzi ya NEC-CCM kuelekea 2015

STARTV: Maamuzi ya NEC-CCM kuelekea 2015

Nape ni kwanini serekali yako imeshindwa kuipa thamani shilingi ya Tanzania? Huoni ni udhaifu mkubwa na hali watu wanalipia viywaji na chakula kwa dola mahotelini?
 
Wingi wa wabunge unaozungumziwa hapa ni wa uwiano wa wabunge vijana kwa wabunge wote. Je, ni chama gani kina uwiano mkubwa wa wabunge vijana?

Kwa hesabu za haraka haraka tu, NCCR inaongoza kwa uwiano, ikifuatiwa na CHADEMA, then CUF, CCM, na za mwisho ni UDP na TLP.
 
Yahaya napendekeza kipindi kuongezewe muda angalau kiwe kinąanza saa 1: 30 mpaka saa 3:30 hasa hiki cha jumapili kwani wengi ndiyotunapata muda kutokana na majukumu ya kikazi natumaini ombi kangu mtalichukulia kwa uzito.
 
Nape na CCM yake wanatapatapa tu na mambo, ana maanisha nini anaposema mikoa ya kisiasa vyuoni? Mikoa hiyo ni ya CCM tu? au na vyama vya upinzani?

Maana nyie mtu akifanya siasa chuoni ni upinzani tu, lakini akifanya siasa za CCM chuoni huyo haguswi lakini akifanya siasa kwa mtazamo wa siasa za kiupinzani chuoni huyo anafukuzwa kwa kuambiwa anaendesha siasa chuoni. Mfano mzuri ni UDOM, wanafunzi wanafukuzwa chuo bila sababu kwa kisingizio cha kufanya siasa chuoni, bila ushaidi wowote bali ni fitina za CCM.
 
Nape, CCM ina msimamo gani kuhusu kikundi cha UAMSHO cha kule Zanzibar kinachoendesha mijadala ya kukashifu viongozi waasisi wa Muungano, hasa kumkashifu hayati Nyerere?
 
siasa zinanipa shida sana.ukidhibiti dola thamani yashilinngi itapanda kwa kiasi kikubwa na mishahara ya wafanyakazi itakuwa na thamani kweli.huoni sisi wafanyakazi kutoiuuga mkono ccm ni haki yetu?
 
1. Hoja ya kupoteza mvuto kwa CCM inajengwa na sababu za msingi kwamba wanachama wenu wengi sana leo hii wanahamia vyama vya upinzani. Hili hata mwananchi wa kawaida analiona. Hata nyie Nape hamuwezi kulikubali moja kwa moja lakini mbinu zenu mbadala juu ya hili tunaiona--- Mmeanzisha mikoa maalumu ya Elimu ya juu kwa nia ya kucompansate namba ya wananchama wanaokumbwa na wimbi la kuhamia vyama vya upinzani toka CCM.

2. Uhuru wa kiuchumi tunaweza kuupata kwa kuwa na ridhaa ya kisiasa juu ya matumizi halisi ya raslimali za nchi yetu la sivyo tutake tusitake tutafuata masharti ya mabwana fedha wa dunia hii hhadi mwisho wa dunia.

3. Ruzuku: CCM imepora mali zote (zile zote ambazo zilitengenezwa kabla ya siasa ya vyama vingi 1992) ambazo nadhani zingekuwa zikitumiwa na chama chochote ambacho kitachukua madaraka ya nchi hii. Ama sivyo, mali zote hizi zingekuwa chini ya Usimamizi wa Serikali ili kuwepo na fair ground kwa vyama vyote
 
Naomba Nape anijibu hili? Kwanini NEC haijakaa KUJADILI kurudisha UTANGANYIKA WETU? Mzanzibari anajitambulisha kwa Uzanzibari wake.

Mimi mtanganyika najitambulisha kwa UTANZANIA WANGU, ambao ni muungano huo wa nchi mbili kuzaa Tanzania
 
hakuna uamuzi mpya yote ni yaleyale ya 1970 siasa ni kilimo na utawala bora. Kinachofanyika ni CCM kukumbuka shuka kumekucha.
 
ni lazima mabadiliko ya kweli yatokee tanzania ili kuivuruga system iliyopo ilituanze upya.hili litatuokolea pesa nyingi sana za walipa kodi zinazotumika ndivyo sivyo.
 
nape kaeni mkao wa kula chadema na sisi tutakuja na sera mpya za mavyuoni.msipige kelele maana nyie mmeanza sisi tunamalizia
 
Sioni kama maoni ya Nape yanatawaliwa sana na hoja, zaidi ya kutaka chama chake ku-win sympathy kutoka kwa wananchi
 
Wingi wa wabunge unaozungumziwa hapa ni wa uwiano wa wabunge vijana kwa wabunge wote. Je, ni chama gani kina uwiano mkubwa wa wabunge vijana?

Kwa hesabu za haraka haraka tu, NCCR inaongoza kwa uwiano, ikifuatiwa na CHADEMA, then CUF, CCM, na za mwisho ni UDP na TLP.
From academic point of view nakubaliana na wewe kabisa lakini kiuhalisia nadhani iko tofauti
 
namuuliza tena Nape.

Anazungmzuaje uhusiano wa chadema na CDU? jee una manufaa kwa watz hasa ukizingatia Watz ni wamoja wa kidini kwa miaka mingi?

Umekwisha wahi ona waarabu wanaleta zawadi za tende kipindi cha xmass.
 
Shukrani Mkuu, tuendelee na mjadala wanajamvi

Yahya fanyen matengenezo wa mitambo yenu,huku Kilimanjaro matangazo yenu yanatikana kwa kukatikakatka sana na ni mwezi mzima sasa,tunashindwa kupata mtiririko mzima wa maada ya michango kwa ujumla.Kama wawakilishi hawawaambii basi nimechukua hilo jukum.
 
Back
Top Bottom