STARTV: Maamuzi ya NEC-CCM kuelekea 2015

Nape ajibu hili: Vyuo siyo majengo au eneo, chuo ni wanafunzi, na walimu wao, kama CCM imerasimisha kuwaingiza rasmi wanafunzi wa vyuo kwenye siasa ni sawa na kufanya siasa vyuoni, na akubali kuwa kitendo hiki kimetokana na CCM kukosa mvuto kwa vijana wa vyuo!
 
Kukimbilia kutangaza siasa vyuoni ni dalili ya kutapatapa, namshauri Nape kama kweli ana uchungu na nchi hii, atafute chama cha wapambanaji wa kweli ajiunge nacho. Kubaki katika chama kilichoshindwa ni sawa na kupoteza muda wake bure.
 
Kwa kuanzia ningependa jina NEC LA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI libadilishwe kuleta utofauti na ile NEC YA CCM. NEC iwe TEC (Tanzania Electoral Commission). Kuhusu maadhimio ya NEC wala sina shaka, CCM ni mavuvuzela, sina imani nao hata kidogo, kifupi wamedandia hoja kwa kuogopa upepo wa kisiasa usiwadhuru. Then inakuwaje wao waruhusu? Kwani nchi chini ya mfumo wa chama kimoja?
 
Nape mnaanzisha mkoa wa wanafunzi huku wakiwa na lundo la matatizo, mnatatua vipi matatizo yao?
 
Pamoja na mapendekezo haya ccm wametoa ccm hawana nia ya kweli kwa haya hii ni kutafuta simpathy iliionekane wania nzuri.
 
Nape, mnapendekeza vyama vingi kwa lengo la kuumiza upinzani au kwa ustawi wa demokrasia nataifa kwa ujumla?
 
Hatuulizii CCM ya zamani!

Mimi nilikuwa CCM na nilikuwa naweza kuchaguliwa ila sasa siwezi kuchaguliwa, na hatuongelei viti maalum kwa sababu hapo napo kuna shida.

Na hao vijana walio na nafasi CCM ni mafisadi vijana na naomba awataje na sisi tutamwambia walivyo.
 
Nape uelewe kuwa wabunge vijana kwa Ccm watakuwa wengi tu kiuhalisisa zaidi ya vyama vya upinzani. Sababu ni kwamba nyie ni wengi sana zaidi ya hao wengine. Kuwa makini Nape na matamshi yako kwani mara nyingi huwa yanazua mjadala mkubwa huku mtaani.
 
Wa Dodoma:

CCM wamekuwa waendelezaji wazuri wa sera za upinzani hilo ni zuri. Mimi kama kijana nimeichoka CCM na kila kijana kaichoka.

Mfano juzi pamoja na kupeleka mabasi ya Shabiby vyuo vya Dodoma kuwabeba wanafunzi kuja kwenye makao makuu ya chama wachache sana walijitokeza.

Kimsingi CCM ituache tujadili kama watu huru kuhusu maswala ya katiba na sio kutupa misimamo.
 
Nape naomba unieleze kwa nini CCM hamtaki mjadala juu ya mfumo mzuri wa Muungano? Kwanini mnaelekeza tuwe na serikali 2 badala ya 3 huku mkitambua hili suala linabishaniwa tangu enzi za akina Aboud Jumbe? Je kwanini hamuoni hiyo haja? Au mpaka wapemba na watanganyika waanze kujitoa mhanga?

CCM kwa sasa ni sawa na meli inayojaribu kuendelea na safari jangwani.

Kimsingi ni chama kilichoifikisha nchi hii katika umasikini mkubwa. Usimamizi mbovu wa rasilimali za nchi chini ya utawala wa chama hiki umesababisha mali nyingi ya nchi kupotea kwa mikataba mibovu. Tukiachana na usimamizi mbovu wa mali ya nchi,

Swali dogo kwa Nape: Ni kwanini CCM imekuwa ikijipendekeza kwa muungano usio na faida yoyote?
 
hakika hili la kuanzishwa kanda maalum vyuo vikuu ccm ni lazima litaighalimu, sasa wasilaumu, chadema hiyo itakuwa ni fursa yao, subiri...
 
Halafu Nape acha kumuiga JK kuongea eti 'Mie napata shida kweli' huu msemo wa JK.
 
Binafsi ni mwanachama Hai wa CCM, naomba nimshauri Nape na viongozi wengine wa kada za juu wa CCM, ni ukweli usiopingika kuwa zaidi ya nusu ya vijana waliopo Tanzania wamehamia au wanaunga mkono upinzani, vijana tuliobaki CCM ni wachache mno.

Ushauri wangu:
Tukiwa tunaelekea kwenye chaguzi za kata na wilaya na badae mkoa na Taifa, vijana wahakikishiwe kutowekewa mizengwe kama ambavyo imekuwa ikitokea hili Nape analifahamu, mfano baadhi ya nafasi kutorusiwa kutokuwa na mawakala kule Dodoma ili uhuni ufanyike, eti ni aibu waziri akigombea na kushindwa hivyo abebwe.

Vinginevyo hata sisi wachache tuliobaki ccm mtatukosa! huu ni ushauri sihitaji Nape atoe majibu ya utetezi
 
naomba kumuuliza nape na wenzake, kwanini mmetoa matamko ya kukataza baadhi ya hoja kuzungumziwa kwenye mjadala wa katiba, wakati ni nafasi ya wananchi kuchagu wanacho kitaka.. Kwanini mnafanya hivyo wakati mnajua wazi katiba si mali ya CCM ni mali ya WANANCHI?
 
Back
Top Bottom