Kwa wanaokujua Fukayosi au wanaopita njia hii ya Bagamoyo Msata watajua ninachotaka kusema. Kama unakwenda Fukayosi ukitokea Bagamoyo, mara baada ya kuvuka daraja la mto Ruvu upande wa kushoto, kuna akina mama wanachemsha mahindi mabichi pale.
Sikuamini macho yangu,kuna ka-foleni katamu ka ma-vx ya watu wanaotafuna mahindi ya wale akina mama. Pale watu wanakandamiza mahindi kama hawana akili nzuri, vitu vya kiasili ni vitamu havina usomi,sijui cheo cha mtu au nini sijui.
Masufuria ya mahindi yanamalizika moja baada ya jingine. Halafu kuna kambale wa kubanikwa. Jamani wasio na ajira wachangamkie hii fursa.
Kama atatokea mtu akaiboresha ile huduma pale( hakuna choo,hakuna mifuko ya kubebea mahindi, maji ya kunywa hakuna,vinywaji baridi hakuna,sipendi maji ya Ilala yawepo,mchemsho ungekuwepo ingekuwa poa, nk), naamini kinaweza kuwa kituo kikubwa sana cha burdani siku chache zijazo hasa week end. Raha nyingine pale Fukayosi ni kwamba, kama unataka kulala pale ( kuna ka-guest house bubu), inabidi usiende na gari, ukienda na gari bei inapanda mara mbili !!
Sikuamini macho yangu,kuna ka-foleni katamu ka ma-vx ya watu wanaotafuna mahindi ya wale akina mama. Pale watu wanakandamiza mahindi kama hawana akili nzuri, vitu vya kiasili ni vitamu havina usomi,sijui cheo cha mtu au nini sijui.
Masufuria ya mahindi yanamalizika moja baada ya jingine. Halafu kuna kambale wa kubanikwa. Jamani wasio na ajira wachangamkie hii fursa.
Kama atatokea mtu akaiboresha ile huduma pale( hakuna choo,hakuna mifuko ya kubebea mahindi, maji ya kunywa hakuna,vinywaji baridi hakuna,sipendi maji ya Ilala yawepo,mchemsho ungekuwepo ingekuwa poa, nk), naamini kinaweza kuwa kituo kikubwa sana cha burdani siku chache zijazo hasa week end. Raha nyingine pale Fukayosi ni kwamba, kama unataka kulala pale ( kuna ka-guest house bubu), inabidi usiende na gari, ukienda na gari bei inapanda mara mbili !!