Star TV yarudi Star Times baada ya Maridhiano

Star TV yarudi Star Times baada ya Maridhiano

Mm niko Morogoro,nimesearch upya lkn hakuna Star Tv...na kwa nn Clouds Tv haipatikan Moro?
 
Ok, Ila kuna mambo mengi sana munatakiwa muyarekebishe. Picha zinakatikakatika, TBC1&2 zinasumbua sana. Mimi huku Tabata napata angalau ITV,EATV, CLOUDS. Tangu iwashwe mitambo ya Makongo, sisi watu wa jiran na mitambo ya Kisarawe shida tupu. TBC ni mdau wa Startimes lakini cha ajab muda mwingi utaambiwa No Services, Not subscribed tena wakat umelipa na au No Signal. Namba za kisimbuzi 02035418564
 
Maswali mengi majibu robo,labda kaenda kurekebisha mambo! Tuwe watulivu jama,mambo mazuri hayataki haraka,hadi dstv channels mutapata for free,tulizeni jazba,tupo sambamba na wanasiasa wanaoheshimika, na wana mkono wao kupitia ile station yao,tutaongea nao na mambo yatakuwa freeesh.
 
Nionavyo mitambo yao imeelemewa. Mwaka2010 nilinunua kisimbuzi cha startimes,ilikuwa clear kwa antena ndogo za ndani. Tangu ilivyozimwa analogia na watu wengi kununua decoder kwa wingi nilianza kuona mabadiliko. Ilianza kukatikakatika hasa kuanzia March mwaka huu. Ilipofika April nadhan walipoongeza mtambo wa Makongojuu ndo mambo yameharibika kabisa. Signal strength ziko dhaifu na matumizi ya antena za ndani yameonyesha kushinndwa kabisa. Turekebishieni jamani sisi TBC hatuipati tena hapa Dar tena Tabata Signal ni rahisi kwani ni jiran tu na Kisarawe
 
Baada ya kukaa takribani siku 5 bila ya kuwa kwenye king'amuzi cha startimes hatimae wamerudi..sijui ni baada ya mkwara au la.
 
Cha ajabu hakuna taarifa yeyote iliyotolewa ili tuweze kujua kilichojiri hadi wakaamua kurejea hewani.
 
Mbona huku tanga haionekani kwenye king'amuzi..wamerudi kweli?
 
Star leteni decorder yenu huku chuga faster tutemane na hawa majambazi ya startimes chanel hazionekani mara nyingine watoe kununua umeshanunua, halafu mjitoe mazima huko startimes coz star tv na itv wanaiuza sana startimes
 
hatimaye star tv imeanza kuonekana tena star times. hongeren kwa kukubaliana
 
Tunashukuru kwa kuirudisha big up sana,kuna tetesi kwamba uwa mnazima mtambo yenu ya makongo au ya kisarawe ndio maana signal zinakuwa weak hamuiwash yote kwa pamoja ndio maana kuna siku inatulia then baada ya siku 2 inaanza tena skrach kuna ukweli wa hz tetesi?


habari yako King Kong, sio kweli, mitambo yetu yote inafanya kazi muda wote, mtambo wa kisarawe ni mkubwa na ni maalumu kwa ving'amuzi wakati ule wa makongo ni mtambo maalumu wa mobile tv ingawa pia uko kama repeater kwa upande wa signal za ving'amuzi. Tatizo ambalo tunalipata kwa sasa ni kuwa kunatokea interference ya signals baina ya mitambo miwili na hii hupelekea wateja wetu hasa walio katikati ya mitambo hii miwili kupata usumbufu mara kwa mara,

mafundi wetu wanajitahidi sana kuweza kutatua hili tatizo.
 
Sasa mkuu, mbona imekua kwa Dar tuu? Sisi wa mikoani tumewakosea nn?

habari yako Jonta ni kweli startv haijarudi mikoa yote,ila imerudi mikoa kadhaa, Katika makubaliano ni kwamba startv itaendelea kupatikana mikoa ile tu ambayo awali ilikuwa inapatikana kwa kupitia analog signals
 
habari yako Jonta ni kweli startv haijarudi mikoa yote,ila imerudi mikoa kadhaa, Katika makubaliano ni kwamba startv itaendelea kupatikana mikoa ile tu ambayo awali ilikuwa inapatikana kwa kupitia analog signals
majanga....decoda ninunue mie, salio niweke mie, channel ukate weweee....majanga....ona majanga
 
Kuna channel kama msnbc mnatangaza zipo halafu mnaziondoa kimya kimya
why?

habari yako Boss, chanel ya MSNBC hatunayo kwa sasa katika king'amuzi chetu, na hii ilitokana na matatizo ya kiufundi toka kwa owner wa chenel, hii ni miongoni mwa chanel ambazo zinapendwa sana na wapenzi wetu, kwa kuwa tatizo lilitokea upande wa provider wa chanel, imetupa tabu sana kutatua tatizo mapema, lakini wataalamu wetu wanafanya kazi kwa ukaribu na watu wa MSNBC kutatua tatizo

pia sio kwamba tuliitoa kimya kimya la hasha ilikata ghafla na sisi tulituma flash SMS katika ving'amuzi kuwataarifu wateja wetu.
 
Ok, Ila kuna mambo mengi sana munatakiwa muyarekebishe. Picha zinakatikakatika, TBC1&2 zinasumbua sana. Mimi huku Tabata napata angalau ITV,EATV, CLOUDS. Tangu iwashwe mitambo ya Makongo, sisi watu wa jiran na mitambo ya Kisarawe shida tupu. TBC ni mdau wa Startimes lakini cha ajab muda mwingi utaambiwa No Services, Not subscribed tena wakat umelipa na au No Signal. Namba za kisimbuzi 02035418564

habari chaza tutajaribu kukupigia simu kupitia namba iliyoandikwa kwenye acc yako 02035418564, kukupatia msaada, stay tuned
 
Back
Top Bottom