Star TV mmethubutu

KALEBE

JF-Expert Member
Aug 11, 2011
773
338
Mjadala wa leo asubuhi star tv kuhusu mchango wa waandishi wa habari katika kuhakikisha kuwa utawala wa sheria na utawala bora vinazingatiwa umenikuna ilivyo. Nimeufuatilia sana mwanzo hadi mwisho, kama kweli wananchi tungekuwa tunasikiliza mijadala hii tusingesubiri hadi iseme. Leo ndo nimeelewa vizuri kuhusu suala la mauaji yaliyotokea Iringa, Morogoro na kwingineko hapa Tanzania. jamani kwa yule ambaye anataka kujua zaidi nitaweka mchakato mzima wa tukio lilivyokuwa hadi Mwangosi kupoteza maisha mwanzoni nilikuwa dilema now i can stand and speak for something.
 
Mkuu mwaga wengine bado tuna tamani kujua zaidi kama ulivyopata nafasi ya kujua na bahati mbaya hatukupata nafasi ya kufuatilia kipindi ..
 
Mlimuangalia mzee Masako na Tendwa jana usiku ITV? Usipime.
 
Hata mimi nimebahatika kukiangalia hicho kipindi leo asubuhi kupitia STAR TVkwa kweli kilikuwa namvuto mkubwa sana. Lakini kuna jamaa mmoja anajihita mwandishi wa habari alikuwa akichangia pumba tupu. Madai yake ni kwamba gazeti la Tanzania Daima limeandika muuaji wa Mwangosi huyu hapa, yeye madai yake anasema sio sahihi kwa waandisha wa habari kuandika vitu kama vile, ila mwenye uwezo wa kujua kama askari huyo kaua au hakuua ni Mahakama tu.Sasa hebu nisaidieni jamani huyu jamaa ni mzima kweli alafu anajiita mwandishi wa habari. Kuna mwandishi mwenzake mmoja alifafanua kuwa ana wasi wasi na elimu ya mwenzake anaona labda amesomea URUSI miaka hiyo.

Mimi najiuliza kama mwandishi wa habari kama huyu anasubutu kupingana na waandishi wa habari wenzake kuhusu mauaji yaliyofanywa na jeshi la polisi dhidi ya Marehemu Mwangosi ambaye ni mwandishi mwenzake. Je mtu kama huyu ataweza kutetea raia wa kawaida ambaye ameuwawa na polisi? Mimi nakubaliana kabisa na mwanaharakati mmoja aliyekuwa anaongea leo kwenye hicho kipindi, kwamba huyo mwenzao labda ameaahidiwa Ukuu wa Wilaya.
 
Hata Tbccm itakuja nyooka tu!siku staff watakapochoka kuburuzwa na mafisadi,hawataogopa tena redundance za majungu,watasimamia ukweli,watajiunga na wenzao star na itv.
 
Nyie hamjui tu kuwa tbccm ni television ya ccm na imezaliwa toka tumbo la radio tanzania, na gazeti lao ni gazeti la uhuru. Star tv ndio tv pekee isiyoogopa vitisho vya kufungiwa mithili ya mwanahalisi ndo maana chadema tunaitumia kutangazia matangazo yetu baada ya hizoo zingingine kukatazwa kujihusiha na habari za chadema.
 
Ngoja nikupe orodha ya vipindi bomba kabisa nilivyoviona wiki hii;
1. HAMZA KASSONGO HOUR, Chanel 10.- kuhusu mauaji ya mwangosi.
2. KIPIMA JOTO, ITV-Kukithiri kwa mauaji katika mikutano ya vyama vya siasa, je ni kukua kwa demokrasia?
3. JICHO LETU NDANI YA HABARI, Star TV(J'mosi tar 8/9/2012).
Hakyanani hivi kwangu ndo vipindi vya kupewa tuzo, wachangiaji walikuwa active na wenye ueledi wa wanachokizungumza. Ila jamaa mmoja anaitwa Mosses Mathew Star TV aliharibu sana, huyu jamaa sijui ana matatizo gani. niliwahi kumuona pia kipndi Star TV walipokuwa wanaongolea ishu ya kufungiwa Mwanahalisi, kwenye kipindi hichohicho, huyu jamaa kwa kweli anatia hasira. Nadhani ana udugu na kina Kamuhanda, Chagonja, Mwema, Ramadhani Ighondu au Jack Zoka. Huyu jamaa ana roho ngumu ile mbaya, na inavyoonekana huyu jamaa uzeeni atakuwa mchawi.
 
Back
Top Bottom