Asante CCM
JF-Expert Member
- Jun 22, 2023
- 346
- 1,301
Duru za kweli kabisa zinatabanaisha bwana Aloyce Nyanda, mtangazaji wa kituo cha runinga Star TV, huenda akafutwa kazi kwa kile kinachodaiwa " hayupo upande wa wakubwa."
Nukuu ya chanzo;
Jamaa kibarua ki shakani sana, maana hata boss kapigiwa simu kibao akilalamikiwa kuhusu yeye kuendesha mijadala hasi ihusuyo Mamlaka.
Yule mwenzake toka amhoji Dk. Slaa kapokea simu nyingi za vitisho na kwa pamoja usishangae vibarua vikaota nyasi.
Chanzo.
Kinachoendelea:
Inasemekana ndugu Antony Diallo ameweka ngumu vijana wake kuingiliwa na ameomba ushahidi wa jambo lolote baya walilolifanya ili basi awahukumu kwa haki.