Inaendelea.
Tsh.1,500,000/= wakati kiwango halisi cha ada ambayo ilitozwa na chuo ni Tsh.1,820,000/= bila ya michango yeyote na ada iliyojumuisha michango mingine ilikuwa ni Tsh.2,100,400/=. Hali hii iko vivyo hivyo kwa kozi za uhandisi ambapo ada na michango Mingine inafikia TSh. 3,000,000/=. Hili limekuwa ni suala ambalo haliwaumizi wanafunzi tu bali wazazi wote wenye watoto wanaosoma katika chuo hiki ambao wamekuwa wakibeba mzigo mkubwa ambao hau hakisi hali halisi ya viwango vya ada katika vyuo vingine nchini kwetu.Vile vile kumekuwa na viwango vikubwa vya ada ya mitihani ambayo ina faini endapo mwanafunzi atachelewa kulipa. Viwango hivi vipo kati ya Tsh. 120,000/= hadi 150,000/= Kwa mwaka wa masomo viwango hivi ni vikubwa na havina uhalisia na viwango vya ada za mitihani katika vyuo vingine.
HATUA ZILIZOTEKELEZWA NA WANAFUNZI KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO ZILIZOBAINISHWA.
1. Mnamo mwaka 2013 wanafunzi wa kitivo cha Ulimu waliwasilisha kwa wizara ya elimu changamoto zinazowakumba na mwaka huo huo Tume ya vyuo vikuu (TCU) ilituma timu ya wataalumu waliokuja kufanya uchunguzi zidi ya madai ya wanafunzi na walitoa ahadi ya kutoa suluhisho kwa changamoto ambazo wanafunzi walikuwa wakizipata. Hata hivyo mwaka huo ulipita bila ya changamoto kutatuliwa.
2. Mnamo mwaka 2014 kwa mara nyengine Tume ya vyuo vikuu (TCU) ilituma timu ya wataalamu kufanya uchunguzi kwa kuzingatia kanuni na taratibu, Tume ya vyuo vikuu ilipata nafasi ya kufanya kikao na serikali ya wanafunzi na changamoto ziliwasilishwa na serikali ya wanafunzi kwa niaba ya wanafunzi na Tume ili ahidi kuchukua hatua katika kuhakikisha changamoto zinatatuliwa na shughuli za masomo kuendelea kama kawaida kwa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za vyuo vikuu.
3. Katika kuendelea kutafuta suluhisho za changamoto hizi ambazo ilionekana kutotafutiwa suluhisho mapema, mnamo mwaka 2015 wanafunzi wa chuo hiki walifanya mgomo wa kutoingia madarasani jambo lililopelekea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuagiza wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi kuunda tume ya uchunguzi na kuhakikisha ripoti ya chuo hiki inawasilishwa bungeni, katika kutafuta suluhu ya changamoto zilizoainishwa katika waraka huu aliyekuwa Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi wa serikali ya awamu ya nne Mh.Shukuru Kawambwa mwaka huo alifika chuoni akiambatana na Katibu mtendaji Tume ya vyuo (TCU) vikuu ndugu Prof,Yunus .D. Mgaya, ambapo walikutana na uongozi wa chuo, cha kusikitisha hawakuweza kuonana na wanafunzi ambao ndio wa hangwa wa changamoto za chuo hiki na hata kile kilichoafikiwa katika kikao cha Mh.Waziri na uongozi wa chuo