ST John na umombo "kanumba" - "Temporary Closer" au "Temporary Closure" ?

mwikumwiku

Senior Member
Jul 15, 2011
153
35
Ni kweli kabisa kwamba Umombo siyo Lugha yetu ya Taifa kwa kuwa Lugha yetu ya Taifa ni Kiswahili. Lakini tususaha kuwa tumekubali umombo siyo tu kuwa Lugha ya Kimataifa bali kuwa moja ya Lugha za mawasiliano rasmi ya kiofisi. Cha msingi zaidi tumeamua na tuanaendelea kusisitiza kuwa lugha ya kufundishia kwenye taasisi za elimu ya juu ni umombo!

Nimesoma kwa mshangao tangazo la Chuo Kikuu cha Mtakatifu John kwa Umma kuhusu kufunguliwa kwa Chuo hicho baada ya kufungwa kwa muda. Tangazo hilo linasomeka hivi: " REOPENING OF THE UNIVERSITY AFTER TEMPORARY CLOSER" shida yangu hapa ni neno "closer" nadhani neno sahihi lingetakiwa kuwa "CLOSURE".
Kuna makosa ambayo katika hali ya kawaida huwezi kutajia kufanywa hasa kwa kuzingatia kosa hilo limefanywa wapi na limefanywa na nani! Hili ni tangazo kwa Umma na limetangazwa na chuo kikuu! Mh! Kwa kweli umakini wa chuo hiki unatia shaka! Sipendi kuamini kwamba kosa hili limefanywa na mhariri kwa kuwa yeye hufanya kazi ya kulibandika kama lilivyoandaliwa japokuwa kwa mhariri makini asingetakiwa kuruhusu makosa kama haya. Angekuwa mwanafunzi tungesema "mbumbu" je chuo hiki tukiiteje?
 
Anaitwa Meshack Karimu huyo Afisa Uhusiano wa St. John's. Ni kilaza wa kufa mtu na amedesa sana kupata hako kadigrii kake. Ni aina ya wale watoto walioishi mitaani kwa muda wa miaka tisa mfululizo.
 
Anaitwa Meshack Karimu huyo Afisa Uhusiano wa St. John's. Ni kilaza wa kufa mtu na amedesa sana kupata hako kadigrii kake. Ni aina ya wale watoto walioishi mitaani kwa muda wa miaka tisa mfululizo.

sasa huu ni ukenge, we endelea kufundisha kiingereza huko bana, acha kuleta habari za watu humu.
Wanaume huwa hawawasemi wnaume wenzako kwa mambo ya kipuuzi ki-hivi.
 
sasa huu ni ukenge, we endelea kufundisha kiingereza huko bana, acha kuleta habari za watu humu.
Wanaume huwa hawawasemi wnaume wenzako kwa mambo ya kipuuzi ki-hivi.

We kweli mgonjwa wa akili. Ni nani aliyemsema mwenzake hapa. Hilo jina lake halipo hapo chini ya tangazo?
 
With all due respect kwa ndugu zangu "wanaosingizia" human error, nadhani kwa hili hiyo siyo sababu! Hili Tangazo kwa Umma, umma unaolengwa hapa ni wa wasomi, wanafunzi. Siyo hivyo tu pia tasisi hii ni ya Elimu ya juu! Kama kuna mambo ambayo wangetakiwa kuweka umakini mkubwa basi ni pamoja na Tangazo hili! Naamini hapo ndipo uwezo wa muandaaji ulipofikia.
 
Asubuhi hii nimesoma hilo Tangazo la St. John University nimeshtushwa sana na ki - english chao, japo mimi nimesoma St. Kayumba mwanzo mwisho ila kwa hili tena kwa chuo kikuu ni aibu tupu! Ningeshauri usome zile paragraph mbili za ufunguzi halafu uniambie kama uongozi wa chuo unaweza kutoa tangazo liliandikwa kwa lugha ya hovyo namna ile, product zake huku sokoni ni Zitakuwaje? Ina maana jamaa aliandika halafu mtu mwenye akili zaidi yake akaifanyia edit kisha wakakubaliana kuipeleka gazetini tena kwa kulipia pesa nyingi tu Duh! Nadhani hiki chuo ni Bomu jingine kwa mustakabali wa Tanzania tunayoitaka.
 
Nawaalika msome content ya hilo tangazo mtapata kichefuchefu! Muandaaji hawezi kutofautisha spoken English na written English.
 
Tatizo letu wa-Bongo huwa hatujipi muda wa kusoma na kusoma na kusoma kile tulichoandika. Huwa nashangaa sana sijui huwa tunataka kuwahi wapi? Naamini kabisa huyo jamaa angejipa muda wa kulisoma hilo bandiko lake mara kadhaa angegundua ni wapi alipokosea. Wahariri wetu nao hovyo, utafikri hawajaenda shule!
 
Hamna Human Error hapo ni Upuuzi mtupu! Kama mi ndo Mkuu wa chuo mpaka usawa huu huyu jamaa hana Kazi kwa aibu hii kwa chuo cha mtakatifu Yohana.
 
Tatizo letu wa-Bongo huwa hatujipi muda wa kusoma na kusoma na kusoma kile tulichoandika. Huwa nashangaa sana sijui huwa tunataka kuwahi wapi? Naamini kabisa huyo jamaa angejipa muda wa kulisoma hilo bandiko lake mara kadhaa angegundua ni wapi alipokosea. Wahariri wetu nao hovyo, utafikri hawajaenda shule!

uko sahihi kabisa mkuu!
 
Back
Top Bottom