Sserunkuma Atakuwa Kama Tambwe

Sserunkuma Atakuwa Kama Tambwe

Ukisikia kilio baada ya jiwe kutupwa gizani ujue kuna mburula limempata kichwani.
 
Wanyama, Olouch na Mariga aliyecheza kwenye final ya champions league akiwa na Inter.Tupe wa ligi yenu ngumu aliyecheza ulaya hata ya mashariki hivi karibuni?
 
Proffesionals wako nimewaona leo wakitolewa jasho na Mnyama mkubwa Abajalo na kutoka sare ya 3-3 huku mashabiki wa mgongo wazi wakiomba mpira uishe.
 
Mkuu ngoja nikupe shule kidogo.....

Ili upate haki ya kuonyesha ligi katika makampuni makubwa, yakupasa utoe pesa ndefu ili upate haki ya kuonyesha ligi husika kupitia media outlet yako..
Ligi ya Tanzania inapokea Pesa ndefu ya udhamini wa haki ya ligi kutoka kwa kampuni ya Azam Media ukilinganisha kiasi cha pesa wanachopokea Ligi ya kenya kutoka kwa supersport.

Hao sijui, DSTV Walitaka kulipia haki ya ligi ya Tanzania lakini hawakuweza kutokana nae Bakhresss(Azam Media) aliweka dau zuri mezani, na TFF walimchagua Azam, hivyo iliwabidi (supersport) warudi kwao.

Thats enough lesson tho...!

DSTV hakuwa na mpango dhati wa kuonesha Ligi Ya Tanzania Bara. Angekuwa na nia Azam wasingeweza kushindana nao. Msuli wa kifedha wa DSTV huwezi kuulinganisha na Azam Media.
 
DSTV hakuwa na mpango dhati wa kuonesha Ligi Ya Tanzania Bara. Angekuwa na nia Azam wasingeweza kushindana nao. Msuli wa kifedha wa DSTV huwezi kuulinganisha na Azam Media.

Kuna rushwa ilitembea. Azam TV walimwaga 10% kuanzia TFF Bodi ya Ligi hadi kwa wadau.
We hushangai Azam TV ilishinda tenda wakati hata stesheni haikuwa hewani haikuwahi kurusha hata tangazo. Uliona wapi duniani
 
DSTV hakuwa na mpango dhati wa kuonesha Ligi Ya Tanzania Bara. Angekuwa na nia Azam wasingeweza kushindana nao. Msuli wa kifedha wa DSTV huwezi kuulinganisha na Azam Media.

Ni kweli, kwamba DSTV wanafedha za kutosha lakini they do have a company policy when it comes about Television Right.
The policy ambayo haiwaruhusu kuchukua haki ya Television kwa malipo ya juu zaidi ,kulingana na ubora,ushindani na umaarufu wa ligi husika.
 
Mambo ya magazeti hayo yapo tu mbona yanga au kandambili walisajili Jagi(Jaja) na hakuna matunda yeyote ambayo aliyaonesha katika timu hiyo wakati mwanzo kabisa walianza kumnadi kwenye media mabali mbali na mwishoweee kumbe ni takataka tena ya muda mrefu Ila kwa moto huu wa msimbazi cyo media tena mtajionea wenyewe moto wake tena salamu ziwafikie kandambili popote walipo
 
Proffesionals wako nimewaona leo wakitolewa jasho na Mnyama mkubwa Abajalo na kutoka sare ya 3-3 huku mashabiki wa mgongo wazi wakiomba mpira uishe.

Na Maprofesheno Wengine Wamepigwa 4-2 Na Walitamani Kukimbia Uwanjani!
 
Ni kweli, kwamba DSTV wanafedha za kutosha lakini they do have a company policy when it comes about Television Right.
The policy ambayo haiwaruhusu kuchukua haki ya Television kwa malipo ya juu zaidi ,kulingana na ubora,ushindani na umaarufu wa ligi husika.

Hamno policy, issue kubwa ni ukubwa wa soko la ving'amuzi. Ligi za Ghana na Zambia ni kubwa, maarufu na zenye ushindani mkubwa kuliko ile ya Kenya lakini bado DSTV anamwaga fedha nyingi kwenye Ligi ya Kenya kuliko Zambia na Ghana.

DSTV hana interests na Ligi za Afrika zaidi ya kuuza ving'amuzi. Rwanda wana a very organised league with more fans than KPL and Uganda lakini DSTV hataki kurusha ligi yao kwa sababu ya udogo wa soko la ving'amuzi.
 
Kuna rushwa ilitembea. Azam TV walimwaga 10% kuanzia TFF Bodi ya Ligi hadi kwa wadau.
We hushangai Azam TV ilishinda tenda wakati hata stesheni haikuwa hewani haikuwahi kurusha hata tangazo. Uliona wapi duniani

Azam TV walitoa rushwa kwenye ofa yao wenyewe? Hakukuwa na competitive tender, hawakuwa na mshindani yeyote. Wao ndio walitoa ofa ndio maana walipewa haki hata kabla ya kuanza kurusha matangazo.
 
Azam TV walitoa rushwa kwenye ofa yao wenyewe? Hakukuwa na competitive tender, hawakuwa na mshindani yeyote. Wao ndio walitoa ofa ndio maana walipewa haki hata kabla ya kuanza kurusha matangazo.

Una uhakika na unachokinena? DSTV walitoa ofa
 
Hamno policy, issue kubwa ni ukubwa wa soko la ving'amuzi. Ligi za Ghana na Zambia ni kubwa, maarufu na zenye ushindani mkubwa kuliko ile ya Kenya lakini bado DSTV anamwaga fedha nyingi kwenye Ligi ya Kenya kuliko Zambia na Ghana.

DSTV hana interests na Ligi za Afrika zaidi ya kuuza ving'amuzi. Rwanda wana a very organised league with more fans than KPL and Uganda lakini DSTV hataki kurusha ligi yao kwa sababu ya udogo wa soko la ving'amuzi.

Mkuu nataka unithibitishie kwa ushahid wa maandishi kwamba..DSTV wanalipa pesa nyingi sana kpl kuliko Ghana na Zambia.
1.Rwanda hawana Luigi yenye mvuto kuliko Tanzania .
2.Kama ni interest ya kuuza vifaa vyao basi wangeichukua ligi ya Tanzania yenye passionate and craziest fans.ambao wangekua ready to buy decoders to watch the league matches.
3.How come kpl is their biggest market.....wakati fans base ya kpl ni nusu ya Vpl.nani atakuwa Tatar ku-buy dstv decoder to watch kpl.
4.Ligi ya Tanzania ndiyo pekee east Africa yenye gate collection kubwa.
 
Naanza kuamini sasa maneno ya wambura kuwa hao friends of simba wana pesa lakini hawaujui mpira. Wao kila mchezaji anyeibukia kucheza vizuri na wengine ni kuibuka kwa msimu tu (na wengine walishaachwa hapo simba miaka 3 iliyopita) wanataka kumsajili. Tatizo kubwa la simba ni beki 1 mzoefu wa kati wa kusaidiana na owino na madogo isihaka +mgeveka wao wanakimbilia kusajili fowadi wakati wanao kibao na hawajawatumia ipasavyo. Wana timu nzuri inayohitaji kukaa pamoja kwa muda mrefu ili wapate matokeo lakini wao wanataka matokeo hapo hapo baada tu ya kufanya usajili. Mpaka uongozi aveva umalize muda wake utaingia kwenye orodha ya uongozi uliwahi kusajili na kuacha wachezaji wengi tangu tupate uhuru.
 
Mkuu nataka unithibitishie kwa ushahid wa maandishi kwamba..DSTV wanalipa pesa nyingi sana kpl kuliko Ghana na Zambia.
1.Rwanda hawana Luigi yenye mvuto kuliko Tanzania .
2.Kama ni interest ya kuuza vifaa vyao basi wangeichukua ligi ya Tanzania yenye passionate and craziest fans.ambao wangekua ready to buy decoders to watch the league matches.
3.How come kpl is their biggest market.....wakati fans base ya kpl ni nusu ya Vpl.nani atakuwa Tatar ku-buy dstv decoder to watch kpl.
4.Ligi ya Tanzania ndiyo pekee east Africa yenye gate collection kubwa.

Hujaelewa kabisa, ukubwa wa soko la ving'amuzi hautokani na mvuto wa ligi bali ukubwa wa uchumi wa nchi husika. Uchumi wa Kenya upo juu ya Tanzania hivyo wananchi wake wengi zaidi wanaweza kununua ving'amuzi vya DSTV kuliko Tanzania na Rwanda zenye ligi zenye mvuto zaidi ya Kenya. Pia idadi ya watu inachangia, mfano ni Botswana, uchumi wao uko safi lakini idadi ya watu ni ndogo sana hivyo DSTV hana mpango wa kudhamini ligi yao.

Ghana na Kenya, zinakaribiana kiuchumi lakini Kenya ina idadi kubwa zaidi ya watu hivyo kupata udhamini mkubwa kuliko Ghana.

Ligi ya Nigeria haina mashabiki kabisa lakini ina udhamini mkubwa sana, zaidi ya $8mn kwa mwaka kwa sababu wanaijeria ni wengi na wengi wao wana uwezo wa kununua ving'amuzi.

Kama sijakosea, nakumbuka udhamini wa DSTV kwa ligi ya Zambia unahusisha vilabu kupata milioni 60 tu kwa mwaka. Kenya vilabu hupata zaidi ya milioni mia kwa mwaka, DSTV wanamwaga around Ksh200mn ambazo ni zaidi ya Tsh3.5bn.

KPL being their market has nothing to do with football, it boils down to economy size, consumer purchasing power, middle class base where Kenya is way ahead of Tanzania. (Our middle class is reported at around 12% whereas Kenya at 44% and Uganda at 28% ndio maana DSTV wanadhamini Ligi za Kenya na Uganda ambazo hazina mashabiki na kuziacha Rwanda na Tanzania zenye mashabiki wengi zaidi).

Kwenye uchumi tunasema, uhitaji sio tu kupenda kitu bali sharti huambatane na uwezo yaani 'mfuko' (demand is all about willingness and ability of the consumer).
Kwa hiyo ni kweli kuwa Watanzania tunapenda mpira zaidi ya Wakenya na Waganda lakini uhitaji wa ving'amuzi vya DSTV ni mdogo kutokana uwezo wetu wa kiuchumi kulinganisha na Kenya na Uganda.
 
Una uhakika na unachokinena? DSTV walitoa ofa

Mia kwa mia, hakukuwa na bidders wengine...DSTV walionesha expression of interests (EOI) tena walitaka kuonesha mechi za Simba na Yanga tu. Mwisho wa siku they never tabled any bid. Kuna clip youtube kwenye chaneli ya Shaffih Dauda inayomuonesha Wallace Karia, makamu mwenyekiti wa TFF akiongelea hilo jambo.
Several times, nimemsikia meneja wa DSTV Afrika Mashariki akiongelea hii ishu.
 
Back
Top Bottom