Sserunkuma Atakuwa Kama Tambwe

Sserunkuma Atakuwa Kama Tambwe

Mr. SADC_TZ

Senior Member
Joined
Nov 7, 2014
Posts
105
Reaction score
22
-Ujio wa mshambuliaji mpya wa Simba SC, Daniel Sserunkuma unaibua maswali mengi kweli.Kutokana na Taswira ya ushindani ktk ligi yetu...je ataweza kuhimili changamoto za VPL.
-Kama Ushindani ktk ligi.
-Presha kutoka kwa mashabiki ya kumtaka afunge goli kila mechi.
-Sifa kutoka kwa Magazeti ya Udaku.

-Au tutegemee kama yaliyomkuta Mwenzake Hamisi Tambwe.
Msimu wa kwanza tu ..kawa Top scorer.... kashiba sifa kutoka kwa mashabiki na magazeti...sifa zikazidi..basi ndio kiwango kimeporomoka...!na hatimaye baada ya msimu mmoja arudi Gor Mahia.
141204121931_ssrenkuma_512x288_bbc.jpg

Aliyekuwa Mshambuliiaji wa mabingwa wa soka nchini Kenya Gor Mahia Dan Serenkuma amejiunga na kilabu ya Tanzania Simba SC.

Raia huyo wa Uganda alijiunga na kilabu hiyo ya Ligi ya Vodacom na kutamatisha kazi yake ya miaka mitatu katika ligi ya Kenya ambapo alianza kwa kuichezea Nairobi City Stars kabla ya kujiunga na Gor ambapo alikuwa kiungo muhimu katika ushindi wa ligi mara mbili.


''Nimefurahia miaka miwili na nusu katika kilabu ya Gor Mahia,lakini huu ndio wakati muhimu wa kuaga.Tumefurahia nyakati maalum na mafanikio pamoja,na habiki wamenisaidia sana hususan wakati mgumu'',Mfungaji huyo wa mabao mengi katika ligi ya Kenya aliandika katika mtandao wake wa Twitter.

''Ningependa kumshukuru kila mtu katika usimamizi wa kilabu kwa kunipa fursa muhimu ili kuonyesha kipaji changu.
Mchezaji huyo wa kimataifa katika timu ya Uganda Cranes alipigwa picha katika mtandao wa kilabu hiyo akifanyiwa majaribio pamoja na kupimwa afya na sasa anatarajiwa kujiunga na wachezaji wenzake katika barabara ya Msimbazi mjini Daresalaam tayari kwa maandalizi ya mechi za ligi ya Tanzania.

Wakati huohuo imebainika kwamba Kilabu ya Gor Mahia ilishindwa kumzuia mchezaji huyo.
Duru zimearifu kuwa mchezaji huyo aliandamwa na kilabu ya Gor mahia kufuatia ripoti za vyombo vya habari kwamba alitarajiwa kujiunga na Simba.

Lakini Gor Mahia haikuwasilisha ombi lolote la fedha kwa kuwa mchezaji huyo tayari alikuwa ameweka kandarasi yenye thamani ya shilingi millioni 3 pamoja na mshahara wa ksh.250,000 kwa mwezi na kilabu hiyo ya Tanzania ambapo atajiunga na mchezaji mwengine wa Gor Mahia Mungai Kiongera.

BBC Swahili
 
-Ujio wa mshambuliaji mpya wa Simba SC, Daniel Sserunkuma unaibua maswali mengi kweli.Kutokana na Taswira ya ushindani ktk ligi yetu...je ataweza kuhimili changamoto za VPL.
-Kama Ushindani ktk ligi.
-Presha kutoka kwa mashabiki ya kumtaka afunge goli kila mechi.
-Sifa kutoka kwa Magazeti ya Udaku.

-Au tutegemee kama yaliyomkuta Mwenzake Hamisi Tambwe.
Msimu wa kwanza tu ..kawa Top scorer.... kashiba sifa kutoka kwa mashabiki na magazeti...sifa zikazidi..basi ndio kiwango kimeporomoka...!na hatimaye baada ya msimu mmoja arudi Gor Mahia.
Kama sifa za magazetini, basi yanga ni kama wamenunua waandishi! Hebu tujikumbushe yaliyoandikwa kuhusu Jaja:
Jaja afunika mazoezini!
Jaja hapatoshi!
Jaja ni sheeeda!
Jaja haijapata tokea!
Nani kama Jaja!

Sasa badala ya kumzungumzia Tambwe aliyeng'aa walau msimu mmoja, hebu mzungumzie Jaja ambaye kuna mechi aligusa mpira mara nne dakika 80. Vivyo hivyo badala ya kumzungumzia SSerunkuma, hebu mzungumzie Emerson ambaye kwenye mazoezi yupo kikosi cha pili!
 
Sserenkuma mchezaji. Nashukuru simba kufanyia kazi ushauri wangu. Nilimwambia tangu ule usajili mkubwa uliopita tuachane na Kiongera kumchukue Dan 'Mzee' sserenkuma. Sijui kilitokea nini lakini nadhani wameliona sasa. Am happy
 
Kama sifa za magazetini, basi yanga ni kama wamenunua waandishi! Hebu tujikumbushe yaliyoandikwa kuhusu Jaja:
Jaja afunika mazoezini!
Jaja hapatoshi!
Jaja ni sheeeda!
Jaja haijapata tokea!
Nani kama Jaja!

Sasa badala ya kumzungumzia Tambwe aliyeng'aa walau msimu mmoja, hebu mzungumzie Jaja ambaye kuna mechi aligusa mpira mara nne dakika 80. Vivyo hivyo badala ya kumzungumzia SSerunkuma, hebu mzungumzie Emerson ambaye kwenye mazoezi yupo kikosi cha pili!

Mkuu lakini kumbuka huyu dogo ni kaanduje...kataweza kweli mikiki mikiki ya kina yondani na canavaro....mhhh...sijui lakini.
 
Sserenkuma mchezaji. Nashukuru simba kufanyia kazi ushauri wangu. Nilimwambia tangu ule usajili mkubwa uliopita tuachane na Kiongera kumchukue Dan 'Mzee' sserenkuma. Sijui kilitokea nini lakini nadhani wameliona sasa. Am happy

Lakini mkuu ndio musahau magoli ya vichwa tena...maana huyu andunje wenu sijui atamsumbua nani...!
 
Mkuu lakini kumbuka huyu dogo ni kaanduje...kataweza kweli mikiki mikiki ya kina yondani na canavaro....mhhh...sijui lakini.

Je Yondan na Kanavaro ni warefu kuliko mabeki wote wa ligi ya Kenya . Mbona unaandika pointless, Messi mbona ananatesa SPAIN ni ngongoti. Nyie mlisajili Ngongoti Shikokoti liwafanyia nini?
 
Napitathu Sijui mkomboziwashafunga??
 
Uongozi wa Aveva umeamua kutufanyia kituko kingine ndugu zangu...huu usajili wa haka kachezaji kafupi...sina uhakika nao..simply because kachezaji kaliongoza kwa magoli kwenye kaligi ka kenya sasa nao simba ndio wameona mlango wa kupitia...haka kachezaji ni kafupi kwelikweli...nilikaona pale msimbazi kalikuwa kanaingia ndani kumwaga wino.

Najiulizaga hivi kweli kataweza kuwakabili akina Canavaro na Yondani.

kusema kweli simba yangu ya nsimuu huu ni Ashki Majnuni.Ngoja niende kwa mtani Yanga (kwa mkopo)...hadi msimu huishe.
 
"...Sserunkuma ana tuzo za mfungaji bora wa ligi ya KPL kwa misimu miwili mfululizo iliyopita. Mwaka 2012 pia alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa KPL. Mwaka 2013 alichaguliwa na Chama Cha Waandishi wa habari za Michezo Uganda kuwa mchezaji bora wa mwaka nchini Uganda, akimshinda Tony Maweje anayecheza ligi ya Norway... Pia ni tegemeo katika timu ya taifa lake..."

NB: Kandambili itabidi mjipange sawa sawa trh 13/12/2014 kupambana dhahama la huyu fundi.

Naendelea kujisomea profile ya huyu fundi wetu mpya.
 
Je Yondan na Kanavaro ni warefu kuliko mabeki wote wa ligi ya Kenya . Mbona unaandika pointless, Messi mbona ananatesa SPAIN ni ngongoti. Nyie mlisajili Ngongoti Shikokoti liwafanyia nini?


Dah mkuu usitake kuchekesha watu humu jamvini...hivi kweli sio dhambi kubwa kumfananisha Sserenkuma na Mungu wa soka
(Messi).

Usijaribu tena mkuu...mwishowe utajikuta unavaa soksi zako kichwani ukafikiri kofia.
 
Mboob ndp nani mkuu.....!

Mboom ni kiungo mshambuliaji "matata sana" toka Gambia, ambae ametua Simba Sc kwa majaribio. Mambo yakienda sawa, tutampa mkataba, ili achachafye dimba akisaidiana na Mtalaamu Mkude.
 
Uongozi wa Aveva umeamua kutufanyia kituko kingine ndugu zangu...huu usajili wa haka kachezaji kafupi...sina uhakika nao..simply because kachezaji kaliongoza kwa magoli kwenye kaligi ka kenya sasa nao simba ndio wameona mlango wa kupitia...haka kachezaji ni kafupi kwelikweli...nilikaona pale msimbazi kalikuwa kanaingia ndani kumwaga wino.

Najiulizaga hivi kweli kataweza kuwakabili akina Canavaro na Yondani.

kusema kweli simba yangu ya nsimuu huu ni Ashki Majnuni.Ngoja niende kwa mtani Yanga (kwa mkopo)...hadi msimu huishe.

We jamaa ni serunkuma kabisa kwa iyo unataka wamsajili hasheem thabeet au?
 
Mr. SADC_TZ kwani mpira huchezwa angani tu? Kenya kwenye mabeki ngongoti kama Shikokoti kawasumbua sana, iweje awashindwe mbilikimo wa Kandambili?
Subiri Mtani Jembe ndo utaona atawafanya nini nyinyi Kandambili. Na hatukuhitaji tena Msimbazi, ubaki huko huko.
 
Last edited by a moderator:
We jamaa ni serunkuma kabisa kwa iyo unataka wamsajili hasheem thabeet au?


Angalau na sisi tuende brasil tukatafute mastaa...bwana.....! huyu dogo haiwezi hii ligi...ligi ya wandava...!

labda lets wait and see, time will tell.!
 
Mr. SADC_TZ kwani mpira huchezwa angani tu? Kenya kwenye mabeki ngongoti kama Shikokoti kawasumbua sana, iweje awashindwe mbilikimo wa Kandambili?
Subiri Mtani Jembe ndo utaona atawafanya nini nyinyi Kandambili. Na hatukuhitaji tena Msimbazi, ubaki huko huko.

Mkuu ligi ya kenya ni sawa na ligi daraja la pili hapa Tanzania in terms of competativeness......!
so ligi yao ni nyepesi sana ...hata kama Tambwe akienda kule na kiwango chake alichokuwa nacho sasa hivi bado atawa-sumbua sana.

Ligi yao mbovu in short.! dah huyu Andunje sasa sijui itakuwaje....hukumuona alivyo kuja na timu yake kwenye moja ya pre season match hapa Tanzania...!

Jamaa sijui ataenda wapi ligi ikiisha...Mashabiki wa mpira pesa watamtaka ashindi kila mechi.
 
Back
Top Bottom