Aisee kwenye hizi halmashauri zetu watumishi wa kawaida wa ngazi za chini na ambao kiukweli ndiyo wanaofanya kazi na kupandisha chati za halmashauri katika sekta zote iwe Elimu (walimu), Kilimo (maafisa ugani/mabwana shamba), Afya (manesi/madaktari) nk tunateseka sana sana ndugu zangu. Na ushahidi mdogo tu ni huu
Hebu wewe jaribu tu kufikiri kuwa baadhi ya halmashauri wanawakopa watumishi hadi fedha ndogondogo tu mathalani za labda uhamisho wa mtumishi/watumishi flani wa kutoka eneo moja la kazi kwenda jingine, likizo, matibabu au hata viposho vidogodogo vya kazi flaniflani za ziada/maalumu wanazofanya hawa watumishi kwa maelezo ya kipumbavu na kijinga tu kuwa "serikali haina fedha au mafungu kwa sasa" na unakuta maDC au maRC hawahawa wanatetea ujinga kama huu kumbe ndani yake kuna siri kuu!!......
Just look, RC analazimishwa achotewe Tshs. 100,000,000/= na Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha!!....Sasa,sijui kutoka katika source ipi na kwa kazi gani aliyofanya. Na hata haoni kuwa ataathiri kwa kiasi kikubwa uendeshaji wa shughuli za halmashauri iwapo akipewa fedha zote hizo na maana yake ni moja tu, UFISADI!!....
Na unashindwa kuelewa hivi Ofisi za Wakuu wa Mikoa au Wilaya, hazina bajeti kwani? Kwa nini wasijichotee fedha kutoka katika bajeji zao kwa kadiri wanavyotaka na badala wanaingilia utendaji wa ofisi zinazohudumia wananachi maelfu kwa maelfu za halishauri za wilaya, Miji, Manispaa na majiji?
Kumbe CHADEMA wako sahihi sana katika sera na mipango yao kufuta hivi vyeo na ofisi za maDC na maRC kwa sababu kwa namna yeyote hazina maana wala kazi yoyote. Na ndiyo maana hawa jamaa wamejikalia Dodoma na kujitungia/tengenezea Katiba yao kwa namna ya kuulinda mfumo huu wa Kifisadi!!??
Now we get it!!