Iruru
JF-Expert Member
- Jan 27, 2014
- 1,470
- 2,881
Spika anatetea kile kilichopo kwneye jimbo lake. Ni wivu tu. Ameshindwa kuwashawishi watu wake wasome na wapige hatua, sasa anaona nongwa kwa majimbo mengine ambayo yametoa watu wengi wasomi.
Akimpongeza mbunge wa Mtera mh Lusinde kwa uchambuzi mzuri wa hotuba ya Waziri Mkuu uliotumia dakika 15 Spika Ndugai amesema Kibajaj anawazidi wasomi wengi mle bungeni.
Spika amesema bungeni yanahitajika maarifa huo uprofesa ni kwa ajili ya kufundisha na kufanya tafiti hivyo katika siasa uprofesa hauna maana yoyote.
Ndio maana wabunge watatu wamewaponda maprofesa tukianza na Kishimba, Kibajaji na kuna wakati Dr Ndugulile aliwahi kumuita waziri fulani Profesa Ziro nikamtoa nje haa haaa amecheka Ndugai.
Ndugai amewataka maprofesa kuwa makini wanapohutubia bungeni kwani darasa la 7 akina Kibajaji, Msukuma Tabasamu, Jah people, Kiinanasi, Babu Tale nk nk wako makini kweli.
Chanzo: TBC
My take; Mbona wabunge wa darasa la 7 ni wanaume watupu!