Spika Ndugai, Pascal Mayalla alijiandaa. Kasome upya makala,utaadhirika...

Spika Ndugai, Pascal Mayalla alijiandaa. Kasome upya makala,utaadhirika...

leonaldo

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2014
Posts
2,584
Reaction score
3,185


Je Bunge linajipendekeza?

"Naomba nisilijibu swali hili nisije kuitwa mbele ya kamati ya haki,kinga na madaraka ya bunge na kuambiwa nimelikashifu Bunge"
Mwisho wa kunukuu sehemu ya makala inayolalamikiwa.

Mheshimiwa spika kwa heshima na taadhima ningependa kuchukua nafasi hii kukupa ushauri wa bure,licha ya kufahamu kuwa wewe ni nguli wa sheria na ni mbabe lakini katika hili umekurupuka utadharilika mapema na asubuhi.

Nilikusikiliza ulivyokuwa ukitoa povu kuwa bunge ni mhimili na spika sio mtu wa mchezo mchezo na jinsi ulivyokuwa ukimsikitikia pascal kwa kitendo chake cha kuandika makala chonganishi kati ya serikari,wananchi na bunge!
Katika hili mheshimiwa umeshindwa vita kwenye hatua ya maandalizi,au umeanguka kabla hujasimama.

Nenda upitie hoja hizi utafakari na ufanye marejeo kwenye maamuzi yako:-
  1. Ni katika aya ipi Pascal katoa hitimisho kuwa "Bunge linajipendekeza"
  2. Katika mifano aliyoitoa Pascal upi ni wa uongo?
  3. Ni sheria au kanuni ipi inayoruhusu ripoti ya kamati ya Bunge kuwasilishwa kwenye muhimili mwingine?
  4. Hukujua kuwa kwa kuwasilisha ripoti ya kamati ya Bunge kwenye muhimili wa serikali(Rais) ulikuwa ukikiuka kanuni za bunge na kulidharilisha Bunge?
  5. Je Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikali nae amelisingizia Bunge kuwa halitekelezi wajibu wake wa kuisimamia serikali?
  6. Ni shetani gani ameliingilia Bunge lako na kuiacha serikali itumie fedha za umma bila kuidhinishwa wala kuleta marejeo ya bajeti? Na Bunge lako likikaa kimya kana kwamba hakuna kinachotokea!
  7. Ndio kwaza unasikia toka kwa mayalla kuwa bunge lako ni butu kuliko bunge lolote katika historia ya Tanzania? Na je mtu kusema ukweli nalo ni kosa? Na hata hivyo unataka kukataa kuwa wabunge wengine wamebaki kutoa huduma za kijamii (kibinadamu)na kuacha majukumu yao ya kimsingi ya kuisimamia serikali na kutunga sheria? Au wewe umelichukuliaje neno "huduma za kibinadamu" Ni mbunge gani hajawahi kufuatwa na wapiga kura wake toka jimboni kwake hadi Dodoma wakihitaji huduma za kibinaadamu(kijamii) ? je Wabunge hawatoi misaada kama ya maziko usafiri na rambirambi kwa wapiga kura wao, vitu kama magari ya wagonjwa,msaada wa karo nk? Si kweli kuwa wabunge hawaishi kulialia bungeni serikali iwatizame kwa jicho la huruma ili wapatiwe maji,hospitali nk, wakati huo huo wakisahau serikali inaendeshwa bila kuzingatia bajeti?
  8. Unadhani wananchi walikuwa usingizini wakati unapewa maelekezo ya kuwakomoa wabunge wenye kihelehele na wenye kidomodomo ndani ya Bunge na kuwa uwatimue na wakija nje muhimili mwenza uwaahughurikie? Unadhani wananchi ni vipofu hawakuona kilichotokea?
  9. Je cheo cha uspika ulicho nacho ni cha kudumu? Kama sio unaenda kuacha nini nyuma yako!
  10. Historia huwa haikosei, niambie toka Bunge la kwanza la Tanzania ni Bunge lipi liliwahi kukumbwa na vituko,ubabe,hatari na visasi kama hili la kwako?
Mwisho nakushauri mheshimiwa Muungwana akivuliwa huchutama,ingawa kuchutama si utamaduni wa serikali ya awamu hii lakini wewe katika hili chutama Pascal hutamuweza,utaadhirika.

Pia soma > Spika aagiza mwandishi Pascal Mayalla na Wahariri wa gazeti la Raia Mwema wahojiwe kwa kulidhalilisha Bunge
 
Hahahahahahahah lol! Wewe Pascal Mayalla nimecheka sana aisee na dharau na kejeli za huyu dikteta uchwara mwingine.

I salute you Sir Pascal Mayalla umegusa penyewe kabisa pale pale panapostahili na kulitikisa Bunge uchwara kitengo cha jiwe na hii Serikali dhalimu.
 
Spika anawaka hasira kama moto wa petrol, hata kuliongelea swala la brother Mayalla kaongea kwa mihemko mno na vitisho kana kwamba anahukumu kuwa Mayalla kakosea sasa kwenye kamati anamuita kufanya nini??
Yaani kaongea kama vile ana ugomvi binafsi na Mayalla. Maneno yale tu yameshaharibu dhana nzima ya kumuita mbele ya kamati kwasababu tayari spika ameshamhukumu kuwa ni mkosaji. Hata Zitto alimtishia hivi hivi nadhani huyu spika anashida sana na Mass communication skills anaongea utadhani yupo kwenye ugomvi kwenye kilabu cha pombe
 
Yaani spika kahukumu tayari kabla hata kamati ya maadili haijakaa. Sasa kazi ya kamati ni nini? Na je hiyo kamati ikibaini kuwa mayalla alikuwa sahihi spika atasemaje? Ndugai anaposema spika hachezewi anamaanisha kuchezewaje? Ni kosa la jinai kulituhumu bunge kama linakiuka misingi yake? Maswali ni mengi sana na ndugai ajue kuwa lile bunge ni la wananchi aisdhani ni mali yake na kijifanya kutunisha misuli kwa vitisho hapa.
Hakuna asiyejua kuwa bunge la sasa ni la hovyo na la kinafiki sana. Wabunge wengi wapo pale kwa maslahi yao na wale wa ccm utadhani wote ni mawaziri maana kila wakisimama ni kusifia tu serikali na kujibu hoja za wabunge wa upinzani na kiti cha spika nacho kinasifia serikali waziwazi hata bila kujua wanadhalilisha muhimili wao huo japo ni muhimili jina tu.
 
Leonardo, asante kwa ufafanuzi. Lile neno hufima za kijamii jinsi alivyolisisitiza Mhe. Supika alinifanya nami kutingwa, kumbe wewe umenieka sawa. Asante sana.
Ni kweli wabunge sasa wengi husaidia angalau gari la wagonjwa, kuzikia, chf, jezi, mpira, rambirambi na kadhalika. Na wale wasiotoa hawahesabiki HAKI.
 
Wabunge wanapoomba kura kwa wananchi wanakuwa wapole wako tayari kutoa hata makalio yao wachapwe viboko na wapiga kura wao ili wapate kura.

Wakishapata wanajigeuza miungu watu wasiotaka Udhaifu wao uhojiwe na wapiga kura wao na kusahau kuwa ndio wale waliokuwa tayari kutoa makalio yao kwa wapiga kura wao wachapwe viboko.
 
Aende tu Na yote aliyojiandaa nayo atakutana Na wajuzi wenzie kule hakuna haja ya kuruka ruka hapa jamii forums
Hivi wewe ni MTU au roboti iliyotengenezwa kutetea tuu bila kufikiri? Mbona hoja hapa iko wazi sasa ugomvi wa nini nawe kutumia nguvu (badala ya akili) kutetea?
Unatumika kama condom ambayo huwa haijui utamu wala imevaliwa kumkinga MTU na mimba au magojwa!
 
Mkuu haya maswali yako inaelekea unataka spika arudishwe tena India!!!

Ninachokumbuka kuna kamati ziliundwa huku spuka akipata muongozo toka Magoogoni jinsi ya kuweka wajumbe kwenye yale mambo ya makinikia!!

Kwa karba ya kina Mlinga,KKibajaji na hata yule aliyempiga mgombea mwenzie kwa gongo hadi akazirai kule Kongwa naona bunch of fools Inapendeza zaidi miongoni mwao! !!
 
alidhani Pascal ni mwandishi maadazi , Pascal alijua anachokiandika na alijihami mapema na "?"...by the way Pascal anazijua siasa za nchi, siyo mgeni.
Kiti Moto
Dah Mkuu Umenikumbusha Mbali Enzi ya Kiti Moto Pascal alikua Moto na hajabadilika..Ni Moja Kati ya Waandishi ninao wakubali Tz.
Hata hapa Jukwaani kunawasio mwelewa Pascal kwenye Mada zake..
 
Back
Top Bottom