Spika Makinda acha kudharau Watanzania

Spika Makinda acha kudharau Watanzania

Wimana

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2012
Posts
2,449
Reaction score
718
Mh Lembeli kauliza swali la nyongeza; ripoti ya utoroshaji wa fedha Uswisi itatolewa, maana Watanzania wengi wanaisubiri kwa hamu.

Kabla AG hajajibu Spika Makinda akachomekea,"kwanza hata hawayajui!

Napenda kumjulisha kuwa;
1. Inawezekana Watanzania wengi hawajui lkn ndio maana wamechagua Wabunge wakiamini wana uelewa.

2. Watanzania wa leo sio wa enzi zako ukiwa Waziri kwenye Serikali ya Nyerere.
 
Mkuu, bibi huyu ni aina ya viongozi tulo nao nchini ambao wanaamini kuwa waTanzania ni wajinga wasiojua lolote kabisa na hatuna umakini wowote kwa masuala yanayotuhusu. Haya maneno aliyotamka ni kejeli mbaya sana kwa wananchi. Swali kwa wote wenye mawazo kama yake: kama hayo hatuyajui wao bungeni waanajadilli kwasababu gani? Au ni kutimiza tu wajibu wapate posho? Bibi amechoka arudi akacheze na wajukuu.
 
Awali huyu mama alivyochaguliwa kuwa Spika wa Bunge la JMT, binafsi nilionesha wasiwasi...
Ni kweli kwamba Mama Makinda ana uzoefu wa muda mrefu kwenye uongozi na hata saikolojia ya uongozi anaifahamu vyema.
Ni mtu aliyeanza kuitumikia CCM tangu ikiitwa TANU na zaidi Baba yake alikuwa ni mtumishi wa Serikali akiwa kama Mkuu wa Mkoa.
Lakini linapokuja suala la kuongoza Vikao vya Bunge ni wazi Spika huitajika kuwa na uwezo wa ziada zaidi ya uzoefu wa kuongoza.
Anapaswa awe ni mtu mwenye kuilinda na kuisimamia Demokrasia kwa kuwa Bunge letu ni mkusanyiko wa Wabunge kutoka vyama mbalimbali, na hapa ndipo Mama Makinda anapoonesha udhaifu.
Unapouzima mjadala kwa kisingizio kuwa Watanzania hawafahamu huo ni upunguani na ukosefu wa uwezo kwenye kuongoza.
Sasa kama Watanzania hawajui, si ndio katokea mtu ambaye anataka kuwafanya Watanzania wafahamu!!
 
Natamani nami ningekuwa waziri mkuu, labda na mie ningemuita askari ili madame spika amtoe bungeni. Hivi wanafikiri matusi ni kama ya Serukamba tu......
 
hata me nilisikia hilo neno alinigadhibisha sana huyu bibi anazeeka vibaya huyu gamba
 
Nimeamua rasmi kuacha kutazama bunge...mana nimekuta natoa maneno makali kwa nguvu mbele ya wanangu!Kauli ya Makinda imenifanya nitamke neno kama la Serukamba nikilielekeza kwa spika!uzuri tu Mama mkwe hajui Kizungu!
 
Mh Lembeli kauliza swali la nyongeza; ripoti ya utoroshaji wa fedha Uswisi itatolewa, maana Watanzania wengi wanaisubiri kwa hamu.

Kabla AG hajajibu Spika Makinda akachomekea,"kwanza hata hawayajui!

Napenda kumjulisha kuwa;
1. Inawezekana Watanzania wengi hawajui lkn ndio maana wamechagua Wabunge wakiamini wana uelewa.

2. Watanzania wa leo sio wa enzi zako ukiwa Waziri kwenye Serikali ya Nyerere.
Kauli ya spika wa bunge iliniuimiza sana na kunikera. Yeye anaamini kuwa watanzania hawafahamu chochote kuhusu fedha zilizofichwa Uswis. Hii ni dharau kwa wananzania na ni ishara ya kulewa madaraka. Kama watu wake wa Njombe waliompigia kura hawafahamu ajue ni kutokana na uzembe wake yeye wa kuchelewesha miundo mbinu kama vile barabara, mawasiliano ya njia zote kama simu, television na radio ndio maana watu wake hawapati habari. Sisi tuna vyanzo vyote vya habari, hivyo tunaelewa kila kinachoendelea katika nchi yetu. Acha dharau kwani madaraka uliyonayo ni ya kupita tu. Haukuzaliwa kiongozi na utaucha uongozi pengine kabla hata Mungu hajakuita. Nonesense.
 
Mh Lembeli kauliza swali la nyongeza; ripoti ya utoroshaji wa fedha Uswisi itatolewa, maana Watanzania wengi wanaisubiri kwa hamu.

Kabla AG hajajibu Spika Makinda akachomekea,"kwanza hata hawayajui!

Napenda kumjulisha kuwa;
1. Inawezekana Watanzania wengi hawajui lkn ndio maana wamechagua Wabunge wakiamini wana uelewa.

2. Watanzania wa leo sio wa enzi zako ukiwa Waziri kwenye Serikali ya Nyerere.

Makinda -(MB) analiabisha sana Bunge....na wa mama wenyewe umri kama wake kwa kuliendesha bunge vibaya kuliko kawaida.....Mkinda amedhalilisha hadhi ya BUNGE ......BUNGE wakati wa Mh. SITA kwa kweli hadhi yake ilikuwa juu sana kuliko ilivyosasa....Mh. Ndugai ndiye kabisa ameshindwa kuliendesha BUNGE.......

Mh. Serukamba, ametukana....TUSI baya kwa kila mtu aliyekuwa anaangalia TV siku hiyo.....

Mh. NKamia pia amewaudhi watanzania wengi kwa ........

Mh. Mohamed......pia amelitukana alidhalilisha BUNGE na watanzania wote kwa ujmla.....

Mh. Ndugai alikuwa ndiye anayeendesha kikao cha BUNGE siku hiyo lakini yeye kwa maarifa, akili zake, na upewo wake ameona ni SAWA kuwafukuza LISSU, LEMA, SUGU, MSIGWA na WENJE kwa kufanya fugo ambayo kimisingi walikuwa wanadai haki ya kupewa rukusa ya kuongea, ameona ni bora kuwatoa nje kwa kuwadhalilisha na kuwapa adhabu ya kutohudhuria vikao vya BUNGE.....akawaacha wale waliotukana, kudhalilisha BUNGE ana WATANZANIA kwa ujumla ....JE NI SAWA ?

Kweli nchi hii sijui tunakwenda wapi........CCM vs. CHADEMA....ndio politics inayoendelea ......

Mkinda na Ndugai hawafai kuliendesha BUNGE.........
 
Mh Lembeli kauliza swali la nyongeza; ripoti ya utoroshaji wa fedha Uswisi itatolewa, maana Watanzania wengi wanaisubiri kwa hamu.

Kabla AG hajajibu Spika Makinda akachomekea,"kwanza hata hawayajui!

Napenda kumjulisha kuwa;
1. Inawezekana Watanzania wengi hawajui lkn ndio maana wamechagua Wabunge wakiamini wana uelewa.

2. Watanzania wa leo sio wa enzi zako ukiwa Waziri kwenye Serikali ya Nyerere.
watanzania hata wakitukanwa lakini watakupa kura tu, watanzania wamelala usingizi wa pono! Ufisadi unaendelea wao wanalala tu!
 
Mh. MAKINDA NA NDUGAI wameonyesha upeo mdogo katika kufanya maamuzi ya misingi kwa kutoa miongozo iyonatija kwa kuipendelea CCM na serikali bila kujua kwamba hujuma hizi zinawalenga na kuwaumiza watanzani wengi.....Halafu Makinda alitumia jina la WATANZANIA VIBAYA....eti kwamba kusema kitendo walichofanya wabunge waliofukuzwa wa CHADEMA kimewaudhi WATANZANIA.....NANI amempa Makinda legitimacy ya kuongea kwa niaba ya wa WATANZANIA.....MAKINDA NA NDUGAI wajue kwamba maamuzi yao na uwendeshaji wao MBAYA wa BUNGE ni dhihaka kwa WATANZANIA WENGI.....
WITO: waandishi wa habari please mwambieni Makinda na NDUGAI kama wanataka kufanya maamuzi sahihi na yenye kupendwa na watanzania wengi ni bora wakapata maoni ya WATANZANIA kabla kutoa maamuzi yao mabaya halafu wakawasingizia WATANZANIA .....HII ni KUTUMIA JINA LA WATANZANIA VIBAYA.......
 
Awali huyu mama alivyochaguliwa kuwa Spika wa Bunge la JMT, binafsi nilionesha wasiwasi...
Ni kweli kwamba Mama Makinda ana uzoefu wa muda mrefu kwenye uongozi na hata saikolojia ya uongozi anaifahamu vyema.
Ni mtu aliyeanza kuitumikia CCM tangu ikiitwa TANU na zaidi Baba yake alikuwa ni mtumishi wa Serikali akiwa kama Mkuu wa Mkoa.
Lakini linapokuja suala la kuongoza Vikao vya Bunge ni wazi Spika huitajika kuwa na uwezo wa ziada zaidi ya uzoefu wa kuongoza.
Anapaswa awe ni mtu mwenye kuilinda na kuisimamia Demokrasia kwa kuwa Bunge letu ni mkusanyiko wa Wabunge kutoka vyama mbalimbali, na hapa ndipo Mama Makinda anapoonesha udhaifu.
Unapouzima mjadala kwa kisingizio kuwa Watanzania hawafahamu huo ni upunguani na ukosefu wa uwezo kwenye kuongoza.
Sasa kama Watanzania hawajui, si ndio katokea mtu ambaye anataka kuwafanya Watanzania wafahamu!!

Yuko hapo kwa matakwa ya watu. Asifikiri Watanzania tumesahau uporaji wa rasilimali uliofanywa na unaondelea kufanywa na Magamba? Tunakumbuka uovu wote.
 
Hajawahi tokea speaker km Samwel Sita. Kwa watu makini na wanaotaka umakini huwezi kumtoa Sita Ukamuweka Makinda. Sawa na kuondoa paka then ukaribishe panya.
 
Ana Makinda aliwekwa kwenye hicho kiti kwa ajili ya kufanya kazi hii ya kutetea UFISADI wa ccm na madhambi yote ya serikali hii impotent.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom