Majibu fikirishi kutoka kwa Mh Tulia Ackson kuhusiana na kupotea kwa Mh Mdude Nyangal, mwanachama wa CHADEMA
Your browser is not able to display this video.
Spika na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Tulia Ackson akifafanua hoja ya Bunge kutotoa maelekezo kuhusu uwepo wa matukio ya Watu kudaiwa kutekwa na wengine kupotea Nchini, amesema hiyo inahitaji ushahidi na isiwe suala la kusikia.
Amezungumza hayo wakati akihojiwa na Wasafi FM, Mei 9, 2025, Mtangazaji Charles Williams alimuuliza “Kumekuwa na vitendo vinavyoitwa vya Utekaji, hata Ripoti ya LHRC imeeleza hilo, hapa Mbeya amepotea Mdude (Nyangali), CHADEMA na Serikali wametangaza dau kwa atakayefanikisha kupatikana kwake.”
Akaongoza “Je, vitendo vya Watu kupotea au kutekwa vinaonekana vimeshamiri au vimerejea kwa kasi, Watu wanadhani Bunge lina sababu ya kusimamisha kusimamisha shughuli zake na kulijadili kwa kina suala hilo, wewe unasemaje?"
Muongo mkubwa, anafumbia macho kwakuwa ye ni moja ya wanufaika!
Mdude ametekwa kwasabb ya misimamo yake dhidi ya watawala wasiopenda kukosolewa...na uzuri Mdude alishasema hapa ikitokea amepotezwa mhusika atakuwa ni sa100!.
Uongo mwingine wa Tulia, mke wa Mdude aliyekuwepo wakati wa ukamataji amethibitisha kwamba mmewe amechukuliwa na mapolisi...tena kwa kumpiga sana hadi kutokwa damu nyingi...Tulia anatuzuga hapa na mifano yake yakijinga!
Kipindi kile Cha mauaji ya albino, bunge lilipojadili hiyo hoja ya dharura, je walikuwa na ushahidi wa nani anawateka au kuwaua maalbino?
Anasema hivyo Kwa sababu yeye ni spika aliwekwa hapo kimikakati, hivyo pamoja na uelewa na ubobevu wale mkubwa, bado kwenye issues kama hizi atajifanya kuwa bunge halina Cha kuazimia. Ila la kuongea mechi ya Simba na Yanga hilo wanalo la kuazimia na Wala siyo hali tete ya usalama nchini.
Hivi watanzania tunategemea miujiza? Tumeambiwa upelelezi wa shambulio la Lisu umekwama kwa sababu aliyeshambuliwa yuko nje ya nchi. Hivi anapouawa mtu upelelezi unafanyikaje?