Rooney
JF-Expert Member
- Jan 16, 2015
- 3,782
- 3,910
You nailed it mkuu... sijui km watashangilia wale nyumbuBaada ya kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Dodoma leo Aprili 6, 2017, Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga aliomba muongozo wa hatua watakazochukuliwa Mbunge wa Hai, FREEMAN MBOWE na Mbunge wa Kawe, HALIMA MDEE kutokana na kupotomosha matusi Bungeni kwa kuwatukana viongozi wa Serikali na Spika wa Bunge. Freeman Mbowe amesikika akiwatukana Rais, Waziri Mkuu na Spika wa Bunge baada ya Wabunge wake Laurence Masha na Ezekiel Wenje kupigiwa kura za HAPANA kuwa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki.
Naye Mbunge wa Kawe, HALIMA MDEE Aprili 4, 2017 amenukuliwa akimtukana Spika wa Bunge Job Ndugai. Kutokana na Muongozo huo, Spika wa Bunge, JOB NDUGAI ameonesha masikitiko yake kwa jinsi Wabunge HALIMA MDEE na Mwenyekiti wake FREEMAN MBOWE walivyo na utovu wa Nidhamu. Spika amesema kuwa haiwezekani Bunge linawaita watu wa nje kuhojiwa na Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge wakati wabunge wenyewe wanakuwa na kiwango kikubwa cha Utovu wa Nidhamu.
Kutokana na hali hiyo ameagiza Mbunge wa Kawe, HALIMA MDEE kukamatwa popote alipo na kufikishwa kwenye mamlaka husika. Pia ameagiza FREEMAN MBOWE kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge na ameiagiza kamati hiyo kukutana haraka iwezekanavyo kushughulikia jambo hilo.
Wale mlioshangilia Paul Makonda kuhojiwa na Bunge, mshangilie pia Mbowe na Mdee kuwekwa kikaangoni.
Chanzo: TBC Taifa