Specifications za Tigo Kitochi 4G

Specifications za Tigo Kitochi 4G

Hiyo ya Vodacom shilingi ngapi nayo?
Hiyo ya vodacom ni nzuri sana kwa bundle la internet. Unapata bundle la internet + simu. Ngoja nikajilipue. Miezi ikiisha na unlock kisha natumia mitandao yote.
 
Ahsante sana Mwalimu Kashasha, haka kasimu kama lengo lako ni kupata MB chukua, ila kama ni good performance soma maoni yangu.

1. Matumizi yake ni magumu kidogo. Mfano back button tuliyoizoea haina kazi hiyo. Badala yake home button (kitufe chekundu/cha kukatia simu) ndio ina kazi hiyo. Ukiandika 0754 333 333 ukitaka kwenda home na uandike namba nyingine, hakuna shortcut mzee, futa moja moja.

2. Ina OS ya upweke inaitwa KiOS, zile apps ulizosikia redioni kama Facebook, Whatsapp nk ndio hizo hizo. Store yao ina apps ambazo wame-recommend udownload hizo tu. Hakuna sehemu ya kusearch ili udownload unazotaka wewe, ukidownloadia nje kwenye browser haziwezi kufunguka. (Hizo Facebook na Whatsapp inawezekana waliwafauta wahusika wenyewe akina Mark na kuwekewa direct).

3. Facebook yake huwezi kubadilisha picha ya profile wala kupost kwenye news timeline, unapakia vizuri tu but ukifika hatua ya "done" cursor inapotea, hata ukiscroll inakuwa haikolezi maandishi ulipofikia ili ubofye. Labda utumie Facebook kwa kutumia kivinjari.
 
4. Kana tabia fulani kama familia ya Tecno smartphones (tabia za Tecno zinajulikana)

5. Ukaaji wa battery ni wa kawaida.

Mimi hapa nimeandika kwa Tecno T402 yenye thamani ya sh 30,000 lakini naenjoy kutumia, chaji inakaa siku 3. Lakini haka kasimu nimenunua jana nikachaji, na sasa hivi nimekachomeka chaji tena.

UZURI WA SIMU HII

1. Kanashika radio kati ya 34 kwa hapa Dar ila uchomeke earphones.

2. Spika zake zinatoa sauti nzuri, sio nyembamba ya kuumiza masikio

3. Kana muonekano mzuri

4. Milio ya kuitia ni mizuri

5. Nimeona kana setting za security ingawa sijazipitia.
 
[QUOTE="Mr Easy,
Thanks for the advice but mimi hayo ya mitandao hata sina habari nayo. Nawaza hayo ma-GB. Matumizi tu madogo madogo ya mawasiliano. Siwezi kusumbuka na hicho kitochi kuitafuta JF wakati natumia JF vizuri via hili dubwana langu.
 
Hapa ndipo pa kujiuliza, utakuta wamekupa na line zao au wana activate kwa hiyo simu pekee na endapo utatoa line kwisha habari yake. Hapa nadhani panahitaji ufafanuzi wa kina. Kwa waliowahi kutumia hizi simu waje kutufafanulia

MC44
 
Wakuu ISO M.CodD MC44 na Shombe la Kisomali nawajibu maswali yenu kwa ujumla kwa sababu kasimu kangu haka-qoute.

Labda nizungumzie kwa upande wa Vodacom ambako nilinunua:

1. Ukienda kununua ili upate ofa ya GB kama sio mteja wa Vodacom, itakulazimu usajili laini ya Vodacom (inaweza kuwa bure au 1000) inategemea na duka uliloenda. Lakini kama tayari ni mteja wa Vodacom utaunganishwa kupitia laini yako.

2. Aliyeuliza kuhusu GB, unaweza kuzitumia kwenye kifaa kingine (mimi nimemalizia kwenye PC)

3. Aliyeuliza kama ina WI-FI, jibu ni ndio. Pia ina Mobile Hotspot inayokuwezesha kugawana mdahalisi na vifaa vingine kama kompyuta, simu janja nyingine nk.

Kwa hiyo ni kazuri pia kutumia kama Modem. Ila ni kagumu kutumia, usije ukasahau hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom