GE2025 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Samia Suluhu na Dkt. Emmanuel Nchimbi

GE2025 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Samia Suluhu na Dkt. Emmanuel Nchimbi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mada Maalum itakayozungumzia ziara nzima kwenye mchakato wa kampeni za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza Dkt. Emmanuel Nchimbi.

Agosti 27, 2025

Mwenyekiti wa INEC, Jaji Mstaafu Jacobs Mwambegele kwa mamlaka aliyopewa amemteua Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea wa kiti cha Makamu wa Rais kupitia CCM.

Pia soma > GE2025 - Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi yawateua Samia na Nchimbi kugombea urais kwa tiketi ya CCM


Tume.jpg
Agosti 30, 2025, Dakawa, Mvomero, Morogoro

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema endapo Watanzania watakiunga mkono chama hicho, kitahakikisha kinaijenga Tanzania ambayo wananchi wanaitaka.

Dkt. Samia aliyasema haya wakati akizungumza na wakazi wa Mvomero katika Uwanja wa Dakawa Sokoine, ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa kampeni za chama hicho.

"Jambo lingine tutajenga njia kubwa ya usafirishaji wa umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Morogoro kwenda Dumila, umeme ule utapita Mvomero na utawanufaisha Wanamvomero, uhakika wa umeme utakwenda kuwepo"

"Ndugu zangu, baada ya kusema hayo na mengine yatakayojitokeza tutakayoyatekeleza, niwaombe sasa tusimame pamoja na kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi ili tuendelee na kasi ya kuijenga Tanzania tunayoitaka,"

"Niwaombe sasa, tusimame pamoja na kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi ili tuendelee na kasi ya kuijenga Tanzania tunayoitaka. Tumesema ikifika 2050, Dira yetu inatuambia tuwe tumefika kwenye Tanzania tunayoitaka- Tanzania ya uchumi wa kipato cha kati lakini cha ngazi ya juu, Tanzania ambayo hakuna atakayelia na huduma za afya wala huduma za elimu wala atakayekosa maji bora na kukosa umeme wa kufanyia kazi zake na kumwangazia pahali alipo. Hiyo ndiyo Tanzania tunayoitaka, Tanzania ambayo uchumi wake utasimama na kujitegemea, Tanzania ambayo hatutaishi wala kufanya shughuli zetu za maendeleo kwa mikopo mikubwa, hiyo ndiyo Tanzania tunayoitaka, ifikapo mwaka 2050, safari yake inaanza miaka mitano inayokuja."


Kilosa

"Kwanza ninajua, bado kuna barabara ambazo zinataka kufanyiwa kazi, Barabara ya Kilosa- Ulaya-Mikumi, tumejenga sehemu, sehemu bado hatujajenga. Ninataka niwaambie miaka mitano ijayo tunakwenda kuifanyia kazi barabara hii. Lakini jingine ni kwamba kuna ushoroba ilikopita Reli ya SGR, ushoroba ule tunakwenda kuujenga viwanda na maghala ili uwe ushoroba wa biashara na kwa ilivyo bahati, ndani ya Wilaya ya Kilosa mna vituo viwili vya SGR kwahiyo jitayarisheni kwa fursa zilizoko kule, zile ni fursa za biashara na ninawaomba Wanakilosa mzitumie na msiwaache watu kutoka maeneo mengine kuja kuzitumia"
 
Kuchezea hela tu hali ya kua washanyakya madaraka.
 
Traffic Alert: On the 28 Aug 2025, CCM will launch it presidential campaigns at Kawe Grounds -Tanganyika Packers. All roads leading to the grounds from Namanga Area, America Embassy, Mbezi beach darajani, Mikocheni B Area will be congested with traffic. Kindly use alternative routes to avoid traffic jams or leave very early in the morning around 5am at the latest. Most roads will be closed for long hours. Staff leaving the side of Mwenge, Africana, Massana Tegeta, Boko to Bunju will be mostly affected.
Security will be very tight
IMG-20250828-WA0022.jpg
 
Inakadiriwa zaidi ya watu 400,000 wamehudhuria kwenye ufunguzi wa kampeni za uchaguzi za CCM 2025 pale Tanganyika Packers.

Mafuriko ya watu kwenye mkutano huo ni ishara ya kwamba, Watanzania wamemshiba haswa kiongozi wao, Rais Samia Suluhu Hassan.
WhatsApp Image 2025-08-28 at 15.45.22_1b8a774d.jpg

WhatsApp Image 2025-08-28 at 15.45.24_278766ce.jpg

Ziko propaganda za wapinzani na wahafidhina waliokuwa wanasema kwamba CCM haina mvuto mtaani, wengi husema hivi kutokana na hali ya mtandaoni, kutokana na posts za Mange na wanaharakati wengine uchwara, bila kujua kwamba, nguvu ya kweli ya chama cha siasa hapo mitandaoni, ipo mitaani ambapo wapiga kura wapo.
WhatsApp Image 2025-08-28 at 15.45.23_d0760f9e.jpg
 
Inakadiriwa zaidi ya watu 400,000 wamehudhuria kwenye ufunguzi wa kampeni za uchaguzi za CCM 2025 pale Tanganyika Packers.

Mafuriko ya watu kwenye mkutano huo ni ishara ya kwamba, Watanzania wamemshiba haswa kiongozi wao, Rais Samia Suluhu Hassan.

Ziko propaganda za wapinzani na wahafidhina waliokuwa wanasema kwamba CCM haina mvuto mtaani, wengi husema hivi kutokana na hali ya mtandaoni, kutokana na posts za Mange na wanaharakati wengine uchwara, bila kujua kwamba, nguvu ya kweli ya chama cha siasa hapo mitandaoni, ipo mitaani ambapo wapiga kura wapo.
Rushwa tupu hamna lolote hapo
 
Mmezuia wamachinga wasifanye biashara leo kariakoo, waende kumsapoti mama.

Nchi ya kisenge sana hii
Ukiona wameenda basi jua wamependa kwenda umezuiwa usifanye biashara sawa je umelazimishwa kwenda kwa nini usilale kwako ukafanya shughuli zako zingine
 
Back
Top Bottom