Hapana my dear natofautiana na wewe kabisa Messi amecheza vizuri tu basi tu hajabahatika kupata goli lake pamoja na kubanwa sana na kukamiwa mno lakini bado anajitahidi kuwatoka opponents anafanyiwa faulo nyingi mpaka naogopa asije rudi majeruhi Barca ,tukiangalia goli la kwanza la Aguero katika mechi ya kwanza ngoma ilianzia kwake kawatoka watu fresh akabanwa Aguero km kawaida kimshale kikachomoka kilikokuwa kikafanya mambo, hata goli LA jana amsha amsha ilianzia kwake,analeta uhai mkubwa kwenye timu yake...kwa kweli bado ni maestro tu maana kwa jinsi wanavyomkamia si mchezo, Ila mtu mmoja hawezi kubadilisha mambo yote peke yake, tatizo bado la Argentina kwa hizi mechi 2 ni kwenye finishing nafasi nyingi sana wanapoteza.