vinneboy
JF-Expert Member
- Aug 12, 2015
- 478
- 436
- Thread starter
- #81
SORRY MADAM (68)
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Macho ya Eddy, Sa Yoo, Shamsa na Madam Mery
wakawashuhudia Phidaya na Rahab wakiingia
kwenye moja ya gari la kifahari huku nyuma yao
akiwepo dokta Ranjiti.
“RANJITIIIIIIIIIIIIIIIIIII…………………….”
Eddy aliita kwa sauti kubwa na kumfanya dokta
Ranjiti kutazama sehemu sauti hiyo inapo tokea,
kwa haraka aliweza kuotambua sauti hiyo ni ya
Eddy, ila sura ni tofauti kabisa, ila macho yake
yalipo muona Madam Mery akiwa nyuma ya mtu
huyo akagundua kwamba kila kitu kimeharibika.
Kwa kiwewe dokta Ranjiti akajikuta akifyatua risasi
kadhaa kuelekea anapotokea Eddy na kusababisha
watu kuanza kukimbia kimbia ovyo kuyaokoa
maisha yao.
ENDELEA
Dokta Ranjiti hakuhitaji kupoteza muda au
kuangalia risasi zake zimemdhuru nani kwa haraka
akaingia ndani ya gari na kumuamuru dereva wake
waondoke kwa kasi katika eneo hilo. Risasi alizo
zifyatua dokta Ranjiti kwa muda mchache ulio pita
kwa bahati mbaya ziliwapata raia wawili ambao
walikuwa wakikatiza mbele ya Eddy. Eddy
akajairibu kulifukuzia gari hilo kwa miguu ila mbio
zake hazikuweza kusaidia chochote mbele ya
mwendo kasi wa gari hilo. Madam Mery, Sa Yoon a
Shamsa wakafika sehemu alipo simama Eddy
anaye hema kwa hasira.
“Sasa inakuwaje?”
Sa Yoo aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka
asijue ni nini afanye kwa wakati huo. Kila mmoja
wao hakujua afanye nini ubaya ni kwamba wote ni
wageni katika nchi ya Misri.
***
“Ranjiti kwa nini unatufanyia hivi lakini?”
Phidaya alizungumza huku machozi yakimwagika.
“Nyamaza wewe, unahisi unaweza kunikimbia
mimi, pumbavu sana wewe”
Muda wote huo, Rahab alikaa kimya asizungumze
kitu chochote akilini mwake akipanga ni kitu gani
anacho weza kukifanya kuyaokoa maisha yao.
Hakuhitaji kuonyesha uwezo wake kwa wakati huo,
alihitaji waweze kufika katika eneo ambalo dokta
Ranjiti alikusudia kuweza kufika ili aweze kufanya
atakacho weza kukifanya kwa wakati huo.
Safari yao ikachukua takribani dakika arobaini,
wakafanikiwa kufika kwenye moja ya gorofa refu
kwenda juu, ambalo kwa haraka haraka
linaonekana ni gorofa kuu kuu(limechakaa).
Wakaingia kwenye ndani, dokta Ranjiti akapolewa
na kikundi cha vijana wenye silaha mikononi
mwao, huku sura zao zikiwa zimefunikwa na
vitambaa vyeusi huku ni sehemu ya macho yao tu
ndio inayo onekana. Wakamtoa Phidaya kwenye
gari pamoja na Rahab, kila mmoja akapelekwa
upande wake jambo ambalo lilimchanganya sana
Rahab.
Rahab akaingizwa kwenye chumba kimoja chenye
kiti kimoja cha chuma pamoja na meza moja iliyo
tengenezwa kwa chuma. Akakalishwa kwa nguvu
kwenye kiti hicho, akafungwa miguu na mikono
yake kwenye kiti hicho. Lugha ya kiarabu wanayo
zungumza vijana hao wawili walio muingiza ndani
ya chumba hicho, ikazidi kumtatiza Rahab, hata
wazo la kujiokoa likapotea kichwani mwake.
Vija hao wakatoka ndani ya chumba hicho chenye
mlango wa chumba, na kuufunga kwa nje. Vijana
wawili wakabaki nje ya mlango huo kwa ajili ya
kuimarisha ulinzi.
Phidaya akaingizwa kwenye moja ya chumba,
ambacho kinakitanda kikubwa. Akarushwa
kitandani na vijana walio muingiza humo ndani
wakatoka na kumuacha dokta Ranjiti peke yake
ndani ya chumba hicho.
“Hivi wewe ni mjanja kuliko mimi, si ndio……?”
Dokta Ranjiti alizungumza huku bastola yake akiwa
ameishika mkononi, Phidaya hakujibu kitu
chochote zaidi ya kutetemeka mwili mzima na
kumwagikwa na machozi mengi.
“Umeisumbua akili yangu, umeusumbua moyo
wangu. Nashindwa kufanya vitu vya maana kwa
ajili yako wewe”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa hasira huku macho
yake yakimtazama Phidaya aliye zidi kutetemeka
na kulia kwa woga.
“Nimelimisi sana penzi lako”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akianza kuvua
nguo zake moja baada ya nyingine. Alipo bakiwa
na nguo ya ndani akapanda kitandani na kuanza
kumsogelea Phidaya taratibu huku bastola yake
akiwa nayo mkononi mwake.
***
Eddy na wezake wakajikuta wakirudi kwenye
chumba anacho lala Shamsa na Sa Yoo, kila
mmoja alijikuta akiwa mwingi wa mawazo,
hususani Eddy, alijihisi kichwa kitampasuka kwa
kuwaza. Simu ya mezani ikawatoa wote kwenye
dibwi la mawazo. Kila mmoja akaitazama simu
hiyo inavyo ita. Kwa haraka Sa Yoo akasimama na
kwenda kuipokea simu hiyo.
“Haloo”
Sauti ya kiume ilisikika upande wa pili wa simu, Sa
Yoo akajikuta akipata kigugumizi kuijibu sauti
hiyo. Eddy kwa akili ya haraka akagundua
kigugumizi cha Sa Yoo kina jambo fulani ambalo
Sa Yoo anashindwa kulijibu. Eddy akanyanyuka
kwa haraka na kumpokonya simu Sa Yoo na
kuzungumza na aliye piga simu hiyo.
“Nani?”
Eddy aliuliza kwa sauti yenye msisitizo mkubwa.
Mpiga simu wa upande wa pili akajikuta akikaa
kimya kwa muda asijubu kitu cha aina yoyote.
“Halooo”
Eddy alizungumza tena kwa msisitizo.
“Samahani nahisi nimekosea namba”
Mtu huyo mwenye sauti ya kiume alizungumza na
kukata simu. Eddy taratibu akaurudisha mkonga
wa simu kwenye sehemu husika kisha akarudi
kwenye sofa alilo kuwa amekaa.
Hadi inatimu majira ya saa tatu kasoro usiku
hapakuwa na jibu lolote walilo weza kulipata juu ya
kutekwa kwa Phidaya. Hata polisi ambao walianza
upelelezi wao hawakuweza kumpata mualifu wala
hawakujua ni wapi muhalifu huyo alipo.
“Kukiwa na chochote, mutanifahamisha, naeleka
chumbani kwangu”
Eddy alizungumza kwa sauti ya unyonge huku
taratibu akinyanyuka na kutoka katika chumba
walipo Shamsa, Madam Mery na Sa Yoo. Kila
mmoja alimtazama Eddy akitoka katika chumba
hicho.
“Mutakula nini?”
Madam Mery alizungumza huku akiwaangali
Shamsa na Sa Yoo.
“Mimi sijisikii njaa”
Shamsa alizungumza huku akinyanyuka na kueleka
katika chumba cha Eddy na kuwaacha Sa Yoo, na
madam Mery alio amua kushuka chini kabisa ya
gorofa la hoteli hiyo kwenye mgahawa mkubwa
kwa ajili ya wageni walio fika kwenye hoteli hiyo.
Shamsa akagonga kwenye chumba cha Eddy mara
kadhaa, baada ya kuona mlango haufunguliwi,
kaingia ndani na kumkuta Eddy akiwa amejilaza
kwenye sofa pasipo kuwasha taa.
“Eddy”
“Mmmmmmm”
“Usiwaze sana”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya unyonge huku
taratibu akikaa sofa la pembeni ya sofa alilo lala
Eddy.
“Ni lazima niwaze, sifahamu ni kitu gani kinacho
endelea kwenye hii dunia”
“Kivipi?”
“Kila kitu ninacho kikusudia kukifanya kwenye
maisha yangu naona kinakwenda kinyume na jinsi
nilivyo taraji kiende”
Eddy alizungumza kwa sauti iliyo jaa huzuni na
unyonge ndani yake huku machozi yakimlenga
lenga.
“Eddy, tambua kwamba kila jambo hutokea kwa
wakati wake. Kuna wakati wa kulia na kunawakati
wa kucheka”
“Sawa Shamsa ila mimi naona ninalia kuliko huko
kucheka. Tazama Junio mwangangu amefariki,
mbaya ameuawa na dada yangu Manka. Mama
amefariki, ameuliwa na baba yangu tena mzazi.
Mke wangu ambaye nilikuwa ninajua amefariki leo
hii namuaona yupo hai, basi nimchukue. Anatokea
mtu anamteka ni nini nitafanya hapa duniani ili
nitulie”
Maneno haya Eddy aliyazungumza huku machozi
yakimwagika, taratibu Shamsa akanyanyuka
kwenye sofa alilo kaa, akakinanyua kichwa cha
Eddy na kukaa kwenye sofa hilo kisha akakaa na
kukiweka kichwa cha Eddy kwenye mapaja yake
yaliyo jazia kiasi.
“Eddy, jinsi unavyo umia wewe ndivyo name pina
ndivyo ninavyo umia”
“Shamsa, hupaswi kuumia tena. Maisha yangu kwa
sasa ninaona hayana thamani yoyote. Nitafanya
chochote nitakacho agizwa ili kumuokoa mke
wangu”
“Bado unathamani kubwa moyoni mwangu Eddy.”
Shamsa alizungumza huku mkono wake wa kulia
akiupitisha pitisha kwenye kifua cha Eddy. Eddy
hakuliweekea maanani jambo hilo, akili yake na
mawazo yake yote yapo kwa mke wake ambaye
hadi sasa hatambui ni wapi alipo. Shamsa
akajikuta akizidi kuipeleka mikono yake yote miwili
kwenye mwili wa Eddy, hadi akaifikisha kiuno cha
Eddy na taratibu akaanza kufungua mkanda wa
suruali.
***
Dokta Ranjiti akaendelea na shuhuli ya kumuingilia
Phidaya, pasipo ridhaa yake japo ni mke wake,
aliye kuwa akiishi naye, ila kwa wakati huo Phidaya
kumbukumbu zake hazikuwepo. Muda wote dokta
Ranjiti anavyo muingilia Phidaya, aliendelea kulia
hadi dokta Ranjiti alipo maliza.
“Aghaaaaaaaa”
Dokta Ranjiti alishusha pumzi huku akitoa miguno
ya kumaliza mpambano wa ulazima alio ufanya
kwa Phidaya. Kama kawaida yake dokta Ranjiti
akajilaza pembani huku akihema kana kwamba
amekimbia umbali wa mbio nyingi.
“Utamu wako mke wangu bado haujaondoka, bado
tunda lako lina joto kali kama nilivyo liacha”
Dokta Ranjiti alizungumza maneno ambayo yalizidi
kumchoma moyo Phidaya, na kuzidi kuipandisha
hasira ya Phidaya iliyo jijenga mara baada ya
kumbukumbu zake kumrejea”
“Hivi niambie mke wangu ni wapi ulipo kuwa?”
Phidaya hakujibu kitu chochote zaidi ya kukaa
kimya.
“Ukikaa kimya sio swala muhimu, kwako. Ila
nimetambua kwamba kamume kako ka zamani
bado kapo hai. Kitu nitakacho kwenda kukifanya
utasikia”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akishuka kitandani
na kuanza kuvaa nguo zake. Alipo maliza kuvaa
akakaa tena kitandani kwa dharau.
“Huto toka hapa hadi nihakikishe Eddy ANAKUFA”
Phidaya alipo sikia kauli ya dokta Ranjiti, mapigo
yake ya moyo yakaanza kumuenda mbio, woga
ukazidi kumtawala maradufu na ilivyo kuwa wali.
“Tafadhali Ranjiti ninakuomba usimuue Eddy, kwa
maana hajafanya kosa lolote baya kwako”
“Nikumuacha hai atafanya kosa ambalo litakuwa
baya kwangu. Wewe ni wangu na hakuna ambaye
atakutoa wewe mikononi mwangu”
Dokta Ranjiti baada ya kuyazungumza maneno
hayo akanyanyuka kutoka kitandani na kutoka
ndani ya chumba hicho na kumuacha Phidaya
akiendelea kulia.
Dokta Ranjiti baada ya kutoka kwenye chumba
alipo Phidaya moja kwa moja akaeleka kwenye
chumba alipo shikiliwa Rahab.
“Mumempatia chakula?”
Dokta Ranjiti aliwauliza vijana wake kwa luhga ya
kiarabu, alio wakuta nje ya chumba walipo
muhifadhi Rahab.
“Ndio mkuu, ila anaonekana amekata chakula”
“Nifungulieni”
Dokta Ranjiti akafunguliwa mlango na kuingia
ndani akamkuta Rahab hajakula chochote na wala
hajafunguliwa jinsi alivyo kuwa amefungwa tangu
mwanzoni, alipo ingizwa katika chumba hicho.
Dokta Ranjiti akamtazama vizuri Rahab na kujikuta
akistuka na kumsogelea vizuri usoni mwake.
Kumbukumbu zake kwa haraka zikampelaka siku
ya msiba wa Phidaya nchini Tanzania. Aliweza
kumshudia akiletwa na msafara mkubwa na
kuheshimiwa.
“Wewe si mke wa raisi Praygod”
Dokta Ranjiti alizungumza huku macho yakimtoka
na kumuangalia vizuri Rahab, akaanza kumgeuza
geuza Rahab sura yake. Jibu alilo kuwa nalo
kichwani mwake ni sahihi kwani Rahab kweli ni
mke wa raisi Praygod. Dokta Ranjiti akakaa kimya
kwa muda kisha akatoka kwenye chumba hicho
akiwa na wasiwasi mkubwa moyoni mwake japo ni
jasiri ila kosa ambalo anahisi litayagharimu maisha
yake ni kitendo cha kuweza kumteka mke wa raisi.
Japo kuwa haelewi ni kitu gani kinacho endelea
ndani ya Tanzania.
“Nahitaji mumuachie huyu msichana”
“Kwa nini mkuu?”
“Huyu sina kazi naye. Hakikisheni kwamba
munamuachia hapa na kumtelekeza huko mtaani”
Hapakuwa na kijana aliye weza kuipinga amri hiyo
ya bosi wao dokta Rajiti, vijana hao wakaingia
ndani ya chumba walipo Rahab. Wakamvunga
macho yake kwa kitambaa cheusi kisha
wakambeba juu juu na moja kwa moja wakempeka
kwenye gari lao jeusi aina ya Toyota Land Cruser
V8. Safari ikaaza kumpeleka kwenye mtaa mmoja
ambao hauna watu wengi. Bila ya kupoteza muda
wakafungua mlango wa gari lao na kumsukumia
Rahab pembezoni mwa barabara na akaangukia
kwenye nyasi nyingi kisha wakaondoka kwa
mwendo wa kasi pasipo kumfungua kamba na
kitambaa walicho mfunga usoni mwake. Rahab
akaanza kujitahidi kujifungua kamba hizo kwa
bahati nzuri akapita kijana wa kiume aliye amua
kumsaidia Rahab na kumfungua kamba hizo
pamoja na kitambaa alicho fungwa usoni mwake.
“Asante”
Rahab alizungumza huku akijipangusa pangusa
majani yaliyoshikamana na nguo zake. Kutokana
na kijana huyo kuzungumza kiarabu na Rahab
haifahamu lugha hiyo ikamlazimu Rahab
kumshukuru kwa vitendo kijana huyo ambaye naye
pia alijibu kwa vitendo. Kwa bahati nzuri katika
eneo hilo ambalo Rahab alitelekezwa, aliweza
kulifahamu kwani ni moja ya maeneo ambayo
hupita asubuhi anapo kimbia akichukua mazoezi
ya viungo.
***
Wasiwasi ukaanza kumtawala Raisi Praygod
ambaye kila alipo itazama simu yake hapakuwa na
simu yoyote ambayo imeingia kutoka kwa mke
wake, ambaye walikubaliana baada ya kufika
hotelini na kukutana na Eddy wawasiliane. Akaanza
kuipiga namba ya simu ya mke wake Rahab, kwa
bahati mbaya ikawa haipatikani jambo lililo zidi
kukiumiza kichwa cheke. Masaa yakazidi kukatika
pasipo Rahab kurudi nyumbani. Kwa haraka
akakumbuka kwamba kuna namba ambayo mke
wake aliweza kuwasiliana na watu ambao
wanakwenda kuonana nao. Kwa haraka akaitazama
kwenye simu yake na kuipiga, kwani Rahab
alimpatia namba hiyo kipindi alipokuwa anaondoka
eneo hilo.
Namba ya simu hiyo kwa bahati nzuri inaita, baada
ya muda ikapokelewa, ila mtu aliye ipokea
hakuzungumza chochote hata pale alipo jaribu
kuzungumza neon Hallo
Sauti nzito ya kiume ilimuuliza kwa lugha ya
Kiswahili kwamba yeye ni nani. Ikamlazimu dokta
Ranjiti kuomba msamaha kwamba amekosea
namba. Raisi Praygod alizungumza hivyo baada ya
kumuona Rahab akiingia ndani, huku jasho
likimwagika. Kwa haraka akakata simu na kwenda
kumlaki mke wake.
“Phidaya ametekwa”
Rahab alizungumza huku akihema, akiwa
amemkumbatia mume wake, kipenzi.
“Ametekwa………..?”
“Ndio ametekwa na mwanaume mmoja ambaye
sina kumbukumbu naye. Ila alipo niona mimi
akanikumbuka na kujikuta akiniachia mimi huru”
Rahab alizungumza huku akihema, hii ni kutokna
na kukimbia kwa umbali mrefu.
“Huyo mtu ana asili gani?”
“Kivipi?”
“Namaanisha kwamba ni muafrika, mzungu au?”
“Ni muarabu”
Raisi Praygod alijikuta akibaki na mshangao
mkubwa kwani hakujua ni nani aliye tekeleza agizo
la Phidaya kutekwa.
“Au labda ndio huyo mume wake ambaye
alitueleza?”
“Ndio sasa nimepata picha, itabidi tuhakikishe
tunamuokoa Phidaya”
“Sasa unapakumbua sehemu alipo kuwa
amewapeleka?”
“Hapana ila nitahakikisha kwamba tunamkomboa”
***
“Shamsa stop”
Eddy alisimama na kutoka mikononi mwa Shamsa
ambaye alisha fanikiwa kuufungua mkanda wa
suruali pamoja na kifungo cha suruali.
“Kumbuka kwamba mimi ni baba yako”
“Hapana Eddy wewe si baba yangu. Mimi nimesha
kuwa na nina hisia za kupenda kama wanawake
wengine na siwezi kuendelea kuzidanganya hisia
zangu kwamba wewe ni baba yangu wakati tayari
nimesha weza kuonja mate yake.”
Shamsa alizungumza kwa kujiamini na kumfanya
Eddy abaki akiwa ameduwaa asijue amjibu nini
Shamsa.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 69 YA SIMUHILI HII.
(Destination of my enemies)
WRITER……………………………..EDDAZARIA GERSHOM
MSULWA(Next level Author)
WEBSITE…………………………… www.storizaeddy
.blogspot.com
EMAIL…………………………………storyzaeddy@yahoo.com
CONTACT…………………………….0657072588/
0768516188
ILIPOISHIA
Macho ya Eddy, Sa Yoo, Shamsa na Madam Mery
wakawashuhudia Phidaya na Rahab wakiingia
kwenye moja ya gari la kifahari huku nyuma yao
akiwepo dokta Ranjiti.
“RANJITIIIIIIIIIIIIIIIIIII…………………….”
Eddy aliita kwa sauti kubwa na kumfanya dokta
Ranjiti kutazama sehemu sauti hiyo inapo tokea,
kwa haraka aliweza kuotambua sauti hiyo ni ya
Eddy, ila sura ni tofauti kabisa, ila macho yake
yalipo muona Madam Mery akiwa nyuma ya mtu
huyo akagundua kwamba kila kitu kimeharibika.
Kwa kiwewe dokta Ranjiti akajikuta akifyatua risasi
kadhaa kuelekea anapotokea Eddy na kusababisha
watu kuanza kukimbia kimbia ovyo kuyaokoa
maisha yao.
ENDELEA
Dokta Ranjiti hakuhitaji kupoteza muda au
kuangalia risasi zake zimemdhuru nani kwa haraka
akaingia ndani ya gari na kumuamuru dereva wake
waondoke kwa kasi katika eneo hilo. Risasi alizo
zifyatua dokta Ranjiti kwa muda mchache ulio pita
kwa bahati mbaya ziliwapata raia wawili ambao
walikuwa wakikatiza mbele ya Eddy. Eddy
akajairibu kulifukuzia gari hilo kwa miguu ila mbio
zake hazikuweza kusaidia chochote mbele ya
mwendo kasi wa gari hilo. Madam Mery, Sa Yoon a
Shamsa wakafika sehemu alipo simama Eddy
anaye hema kwa hasira.
“Sasa inakuwaje?”
Sa Yoo aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka
asijue ni nini afanye kwa wakati huo. Kila mmoja
wao hakujua afanye nini ubaya ni kwamba wote ni
wageni katika nchi ya Misri.
***
“Ranjiti kwa nini unatufanyia hivi lakini?”
Phidaya alizungumza huku machozi yakimwagika.
“Nyamaza wewe, unahisi unaweza kunikimbia
mimi, pumbavu sana wewe”
Muda wote huo, Rahab alikaa kimya asizungumze
kitu chochote akilini mwake akipanga ni kitu gani
anacho weza kukifanya kuyaokoa maisha yao.
Hakuhitaji kuonyesha uwezo wake kwa wakati huo,
alihitaji waweze kufika katika eneo ambalo dokta
Ranjiti alikusudia kuweza kufika ili aweze kufanya
atakacho weza kukifanya kwa wakati huo.
Safari yao ikachukua takribani dakika arobaini,
wakafanikiwa kufika kwenye moja ya gorofa refu
kwenda juu, ambalo kwa haraka haraka
linaonekana ni gorofa kuu kuu(limechakaa).
Wakaingia kwenye ndani, dokta Ranjiti akapolewa
na kikundi cha vijana wenye silaha mikononi
mwao, huku sura zao zikiwa zimefunikwa na
vitambaa vyeusi huku ni sehemu ya macho yao tu
ndio inayo onekana. Wakamtoa Phidaya kwenye
gari pamoja na Rahab, kila mmoja akapelekwa
upande wake jambo ambalo lilimchanganya sana
Rahab.
Rahab akaingizwa kwenye chumba kimoja chenye
kiti kimoja cha chuma pamoja na meza moja iliyo
tengenezwa kwa chuma. Akakalishwa kwa nguvu
kwenye kiti hicho, akafungwa miguu na mikono
yake kwenye kiti hicho. Lugha ya kiarabu wanayo
zungumza vijana hao wawili walio muingiza ndani
ya chumba hicho, ikazidi kumtatiza Rahab, hata
wazo la kujiokoa likapotea kichwani mwake.
Vija hao wakatoka ndani ya chumba hicho chenye
mlango wa chumba, na kuufunga kwa nje. Vijana
wawili wakabaki nje ya mlango huo kwa ajili ya
kuimarisha ulinzi.
Phidaya akaingizwa kwenye moja ya chumba,
ambacho kinakitanda kikubwa. Akarushwa
kitandani na vijana walio muingiza humo ndani
wakatoka na kumuacha dokta Ranjiti peke yake
ndani ya chumba hicho.
“Hivi wewe ni mjanja kuliko mimi, si ndio……?”
Dokta Ranjiti alizungumza huku bastola yake akiwa
ameishika mkononi, Phidaya hakujibu kitu
chochote zaidi ya kutetemeka mwili mzima na
kumwagikwa na machozi mengi.
“Umeisumbua akili yangu, umeusumbua moyo
wangu. Nashindwa kufanya vitu vya maana kwa
ajili yako wewe”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa hasira huku macho
yake yakimtazama Phidaya aliye zidi kutetemeka
na kulia kwa woga.
“Nimelimisi sana penzi lako”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akianza kuvua
nguo zake moja baada ya nyingine. Alipo bakiwa
na nguo ya ndani akapanda kitandani na kuanza
kumsogelea Phidaya taratibu huku bastola yake
akiwa nayo mkononi mwake.
***
Eddy na wezake wakajikuta wakirudi kwenye
chumba anacho lala Shamsa na Sa Yoo, kila
mmoja alijikuta akiwa mwingi wa mawazo,
hususani Eddy, alijihisi kichwa kitampasuka kwa
kuwaza. Simu ya mezani ikawatoa wote kwenye
dibwi la mawazo. Kila mmoja akaitazama simu
hiyo inavyo ita. Kwa haraka Sa Yoo akasimama na
kwenda kuipokea simu hiyo.
“Haloo”
Sauti ya kiume ilisikika upande wa pili wa simu, Sa
Yoo akajikuta akipata kigugumizi kuijibu sauti
hiyo. Eddy kwa akili ya haraka akagundua
kigugumizi cha Sa Yoo kina jambo fulani ambalo
Sa Yoo anashindwa kulijibu. Eddy akanyanyuka
kwa haraka na kumpokonya simu Sa Yoo na
kuzungumza na aliye piga simu hiyo.
“Nani?”
Eddy aliuliza kwa sauti yenye msisitizo mkubwa.
Mpiga simu wa upande wa pili akajikuta akikaa
kimya kwa muda asijubu kitu cha aina yoyote.
“Halooo”
Eddy alizungumza tena kwa msisitizo.
“Samahani nahisi nimekosea namba”
Mtu huyo mwenye sauti ya kiume alizungumza na
kukata simu. Eddy taratibu akaurudisha mkonga
wa simu kwenye sehemu husika kisha akarudi
kwenye sofa alilo kuwa amekaa.
Hadi inatimu majira ya saa tatu kasoro usiku
hapakuwa na jibu lolote walilo weza kulipata juu ya
kutekwa kwa Phidaya. Hata polisi ambao walianza
upelelezi wao hawakuweza kumpata mualifu wala
hawakujua ni wapi muhalifu huyo alipo.
“Kukiwa na chochote, mutanifahamisha, naeleka
chumbani kwangu”
Eddy alizungumza kwa sauti ya unyonge huku
taratibu akinyanyuka na kutoka katika chumba
walipo Shamsa, Madam Mery na Sa Yoo. Kila
mmoja alimtazama Eddy akitoka katika chumba
hicho.
“Mutakula nini?”
Madam Mery alizungumza huku akiwaangali
Shamsa na Sa Yoo.
“Mimi sijisikii njaa”
Shamsa alizungumza huku akinyanyuka na kueleka
katika chumba cha Eddy na kuwaacha Sa Yoo, na
madam Mery alio amua kushuka chini kabisa ya
gorofa la hoteli hiyo kwenye mgahawa mkubwa
kwa ajili ya wageni walio fika kwenye hoteli hiyo.
Shamsa akagonga kwenye chumba cha Eddy mara
kadhaa, baada ya kuona mlango haufunguliwi,
kaingia ndani na kumkuta Eddy akiwa amejilaza
kwenye sofa pasipo kuwasha taa.
“Eddy”
“Mmmmmmm”
“Usiwaze sana”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya unyonge huku
taratibu akikaa sofa la pembeni ya sofa alilo lala
Eddy.
“Ni lazima niwaze, sifahamu ni kitu gani kinacho
endelea kwenye hii dunia”
“Kivipi?”
“Kila kitu ninacho kikusudia kukifanya kwenye
maisha yangu naona kinakwenda kinyume na jinsi
nilivyo taraji kiende”
Eddy alizungumza kwa sauti iliyo jaa huzuni na
unyonge ndani yake huku machozi yakimlenga
lenga.
“Eddy, tambua kwamba kila jambo hutokea kwa
wakati wake. Kuna wakati wa kulia na kunawakati
wa kucheka”
“Sawa Shamsa ila mimi naona ninalia kuliko huko
kucheka. Tazama Junio mwangangu amefariki,
mbaya ameuawa na dada yangu Manka. Mama
amefariki, ameuliwa na baba yangu tena mzazi.
Mke wangu ambaye nilikuwa ninajua amefariki leo
hii namuaona yupo hai, basi nimchukue. Anatokea
mtu anamteka ni nini nitafanya hapa duniani ili
nitulie”
Maneno haya Eddy aliyazungumza huku machozi
yakimwagika, taratibu Shamsa akanyanyuka
kwenye sofa alilo kaa, akakinanyua kichwa cha
Eddy na kukaa kwenye sofa hilo kisha akakaa na
kukiweka kichwa cha Eddy kwenye mapaja yake
yaliyo jazia kiasi.
“Eddy, jinsi unavyo umia wewe ndivyo name pina
ndivyo ninavyo umia”
“Shamsa, hupaswi kuumia tena. Maisha yangu kwa
sasa ninaona hayana thamani yoyote. Nitafanya
chochote nitakacho agizwa ili kumuokoa mke
wangu”
“Bado unathamani kubwa moyoni mwangu Eddy.”
Shamsa alizungumza huku mkono wake wa kulia
akiupitisha pitisha kwenye kifua cha Eddy. Eddy
hakuliweekea maanani jambo hilo, akili yake na
mawazo yake yote yapo kwa mke wake ambaye
hadi sasa hatambui ni wapi alipo. Shamsa
akajikuta akizidi kuipeleka mikono yake yote miwili
kwenye mwili wa Eddy, hadi akaifikisha kiuno cha
Eddy na taratibu akaanza kufungua mkanda wa
suruali.
***
Dokta Ranjiti akaendelea na shuhuli ya kumuingilia
Phidaya, pasipo ridhaa yake japo ni mke wake,
aliye kuwa akiishi naye, ila kwa wakati huo Phidaya
kumbukumbu zake hazikuwepo. Muda wote dokta
Ranjiti anavyo muingilia Phidaya, aliendelea kulia
hadi dokta Ranjiti alipo maliza.
“Aghaaaaaaaa”
Dokta Ranjiti alishusha pumzi huku akitoa miguno
ya kumaliza mpambano wa ulazima alio ufanya
kwa Phidaya. Kama kawaida yake dokta Ranjiti
akajilaza pembani huku akihema kana kwamba
amekimbia umbali wa mbio nyingi.
“Utamu wako mke wangu bado haujaondoka, bado
tunda lako lina joto kali kama nilivyo liacha”
Dokta Ranjiti alizungumza maneno ambayo yalizidi
kumchoma moyo Phidaya, na kuzidi kuipandisha
hasira ya Phidaya iliyo jijenga mara baada ya
kumbukumbu zake kumrejea”
“Hivi niambie mke wangu ni wapi ulipo kuwa?”
Phidaya hakujibu kitu chochote zaidi ya kukaa
kimya.
“Ukikaa kimya sio swala muhimu, kwako. Ila
nimetambua kwamba kamume kako ka zamani
bado kapo hai. Kitu nitakacho kwenda kukifanya
utasikia”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akishuka kitandani
na kuanza kuvaa nguo zake. Alipo maliza kuvaa
akakaa tena kitandani kwa dharau.
“Huto toka hapa hadi nihakikishe Eddy ANAKUFA”
Phidaya alipo sikia kauli ya dokta Ranjiti, mapigo
yake ya moyo yakaanza kumuenda mbio, woga
ukazidi kumtawala maradufu na ilivyo kuwa wali.
“Tafadhali Ranjiti ninakuomba usimuue Eddy, kwa
maana hajafanya kosa lolote baya kwako”
“Nikumuacha hai atafanya kosa ambalo litakuwa
baya kwangu. Wewe ni wangu na hakuna ambaye
atakutoa wewe mikononi mwangu”
Dokta Ranjiti baada ya kuyazungumza maneno
hayo akanyanyuka kutoka kitandani na kutoka
ndani ya chumba hicho na kumuacha Phidaya
akiendelea kulia.
Dokta Ranjiti baada ya kutoka kwenye chumba
alipo Phidaya moja kwa moja akaeleka kwenye
chumba alipo shikiliwa Rahab.
“Mumempatia chakula?”
Dokta Ranjiti aliwauliza vijana wake kwa luhga ya
kiarabu, alio wakuta nje ya chumba walipo
muhifadhi Rahab.
“Ndio mkuu, ila anaonekana amekata chakula”
“Nifungulieni”
Dokta Ranjiti akafunguliwa mlango na kuingia
ndani akamkuta Rahab hajakula chochote na wala
hajafunguliwa jinsi alivyo kuwa amefungwa tangu
mwanzoni, alipo ingizwa katika chumba hicho.
Dokta Ranjiti akamtazama vizuri Rahab na kujikuta
akistuka na kumsogelea vizuri usoni mwake.
Kumbukumbu zake kwa haraka zikampelaka siku
ya msiba wa Phidaya nchini Tanzania. Aliweza
kumshudia akiletwa na msafara mkubwa na
kuheshimiwa.
“Wewe si mke wa raisi Praygod”
Dokta Ranjiti alizungumza huku macho yakimtoka
na kumuangalia vizuri Rahab, akaanza kumgeuza
geuza Rahab sura yake. Jibu alilo kuwa nalo
kichwani mwake ni sahihi kwani Rahab kweli ni
mke wa raisi Praygod. Dokta Ranjiti akakaa kimya
kwa muda kisha akatoka kwenye chumba hicho
akiwa na wasiwasi mkubwa moyoni mwake japo ni
jasiri ila kosa ambalo anahisi litayagharimu maisha
yake ni kitendo cha kuweza kumteka mke wa raisi.
Japo kuwa haelewi ni kitu gani kinacho endelea
ndani ya Tanzania.
“Nahitaji mumuachie huyu msichana”
“Kwa nini mkuu?”
“Huyu sina kazi naye. Hakikisheni kwamba
munamuachia hapa na kumtelekeza huko mtaani”
Hapakuwa na kijana aliye weza kuipinga amri hiyo
ya bosi wao dokta Rajiti, vijana hao wakaingia
ndani ya chumba walipo Rahab. Wakamvunga
macho yake kwa kitambaa cheusi kisha
wakambeba juu juu na moja kwa moja wakempeka
kwenye gari lao jeusi aina ya Toyota Land Cruser
V8. Safari ikaaza kumpeleka kwenye mtaa mmoja
ambao hauna watu wengi. Bila ya kupoteza muda
wakafungua mlango wa gari lao na kumsukumia
Rahab pembezoni mwa barabara na akaangukia
kwenye nyasi nyingi kisha wakaondoka kwa
mwendo wa kasi pasipo kumfungua kamba na
kitambaa walicho mfunga usoni mwake. Rahab
akaanza kujitahidi kujifungua kamba hizo kwa
bahati nzuri akapita kijana wa kiume aliye amua
kumsaidia Rahab na kumfungua kamba hizo
pamoja na kitambaa alicho fungwa usoni mwake.
“Asante”
Rahab alizungumza huku akijipangusa pangusa
majani yaliyoshikamana na nguo zake. Kutokana
na kijana huyo kuzungumza kiarabu na Rahab
haifahamu lugha hiyo ikamlazimu Rahab
kumshukuru kwa vitendo kijana huyo ambaye naye
pia alijibu kwa vitendo. Kwa bahati nzuri katika
eneo hilo ambalo Rahab alitelekezwa, aliweza
kulifahamu kwani ni moja ya maeneo ambayo
hupita asubuhi anapo kimbia akichukua mazoezi
ya viungo.
***
Wasiwasi ukaanza kumtawala Raisi Praygod
ambaye kila alipo itazama simu yake hapakuwa na
simu yoyote ambayo imeingia kutoka kwa mke
wake, ambaye walikubaliana baada ya kufika
hotelini na kukutana na Eddy wawasiliane. Akaanza
kuipiga namba ya simu ya mke wake Rahab, kwa
bahati mbaya ikawa haipatikani jambo lililo zidi
kukiumiza kichwa cheke. Masaa yakazidi kukatika
pasipo Rahab kurudi nyumbani. Kwa haraka
akakumbuka kwamba kuna namba ambayo mke
wake aliweza kuwasiliana na watu ambao
wanakwenda kuonana nao. Kwa haraka akaitazama
kwenye simu yake na kuipiga, kwani Rahab
alimpatia namba hiyo kipindi alipokuwa anaondoka
eneo hilo.
Namba ya simu hiyo kwa bahati nzuri inaita, baada
ya muda ikapokelewa, ila mtu aliye ipokea
hakuzungumza chochote hata pale alipo jaribu
kuzungumza neon Hallo
Sauti nzito ya kiume ilimuuliza kwa lugha ya
Kiswahili kwamba yeye ni nani. Ikamlazimu dokta
Ranjiti kuomba msamaha kwamba amekosea
namba. Raisi Praygod alizungumza hivyo baada ya
kumuona Rahab akiingia ndani, huku jasho
likimwagika. Kwa haraka akakata simu na kwenda
kumlaki mke wake.
“Phidaya ametekwa”
Rahab alizungumza huku akihema, akiwa
amemkumbatia mume wake, kipenzi.
“Ametekwa………..?”
“Ndio ametekwa na mwanaume mmoja ambaye
sina kumbukumbu naye. Ila alipo niona mimi
akanikumbuka na kujikuta akiniachia mimi huru”
Rahab alizungumza huku akihema, hii ni kutokna
na kukimbia kwa umbali mrefu.
“Huyo mtu ana asili gani?”
“Kivipi?”
“Namaanisha kwamba ni muafrika, mzungu au?”
“Ni muarabu”
Raisi Praygod alijikuta akibaki na mshangao
mkubwa kwani hakujua ni nani aliye tekeleza agizo
la Phidaya kutekwa.
“Au labda ndio huyo mume wake ambaye
alitueleza?”
“Ndio sasa nimepata picha, itabidi tuhakikishe
tunamuokoa Phidaya”
“Sasa unapakumbua sehemu alipo kuwa
amewapeleka?”
“Hapana ila nitahakikisha kwamba tunamkomboa”
***
“Shamsa stop”
Eddy alisimama na kutoka mikononi mwa Shamsa
ambaye alisha fanikiwa kuufungua mkanda wa
suruali pamoja na kifungo cha suruali.
“Kumbuka kwamba mimi ni baba yako”
“Hapana Eddy wewe si baba yangu. Mimi nimesha
kuwa na nina hisia za kupenda kama wanawake
wengine na siwezi kuendelea kuzidanganya hisia
zangu kwamba wewe ni baba yangu wakati tayari
nimesha weza kuonja mate yake.”
Shamsa alizungumza kwa kujiamini na kumfanya
Eddy abaki akiwa ameduwaa asijue amjibu nini
Shamsa.
ITAENDELEA
USIKOSE SEHEMU YA 69 YA SIMUHILI HII.