TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,765
- 4,033
Mwenyekiti wa umoja wa wanawake ((UWT) bi Sophia Simba ameweka hadharani upungufu wa chama cha mapinduzi(CCM) na kukisifia chama cha Democrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa mfumo walionao wa kisasa unaovutia kizazi cha sasa na kupata umaarufu wa ghafla.
Bi Simba ambaye ni Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na watoto alisema hayo jana katika mkutano wa kwanza wa Baraza la UWT katika wilaya ya kinondoni akiwa kama mgeni rasmi ambapo mwenyeji wake alikuwa ni mwenyekiti wa UWT wa wilaya hiyo Bi Anna Makete.
Bi Simba alisema kuwa katika kipindi kifupi kilichopita na sasa,CCM imepoteza umaarufu wake kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo mfumo wao wa sasa, kutoendana na kizazi kipya ambacho asilimia kubwa ni vijana,kuzidiwa na manano ya propaganda za vyama vya upinzani na kusababisha kushindwa kujibu mapigo na kuwa wanyonge,makundi ndani ya chama,ubinafsi pamoja vijana kukosa uwezesho wa ujasiriamali ndani ya chama.
Alitaja sabubu nyingine kuwa ni mfumo uliotumika mwaka jana kuwapata wagombea katika nafasi mbalimbali za uongozi uliochangia kuwapoteza wana CCM pia wananchi kuchelewa kumtambua mgombea wao na mambo mengine madogo madogo.
Akizungumzia umaarufu wa CHADEMA alisema umetokana na mfumo na sera walionayo sasa,DKt Willbrod Slaa kuibua suala la Richmond na Dowans bungeni na kutaka kuvunja mkataba ambao umesababisha nchi kushitakiwa na kutakiwa kulipa mabilioni ya fedha pamoja na njama za wafadhili wa chama hicho kutoka nje ya nchi kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kuking'oa CCM madarakani.
Nyingine ni kupanda kwa gharama za maisha kutokana na sababu mbalimbali ambayo yanamgusa kila mtu alisema kwamba CHADEMA imetumia mwanya huo kufanya maandamano huku wakidai kwamba ni kutokana na CCM kuwepo madarakani.
Bi Simba alisema kuwa kitendo cha CHADEMA kufanya maandamano jijini Mwanza juzi ni kutafuta umaarufu na si vinginevyo huku wakisingizia kupinga malipo ya Dowans na mgawo wa umeme.
Alisema kuwa kilichokuwa kinazungumzwa na viongozi wa CHADEMA juzi kilikuwa tayari kimefikishwa mezani na kinafanyiwa kazi ikiwemo mazungumzo kati ya mmiliki wa Dowans na Serikali ili kuondoa suala la mgawo wa umeme pamoja na mkakati wa kushusha bei ya bidhaa muhimu kama sukari.
Bi Sophia alisema hatua iliyofikia ya kutaka serikali ilipe shs bilioni 94 za Dowans inatokana na mipango ya Dkt.Slaa na wanasiasa wengine kutaka mkataba uvunjwe huku wakijua matatizo yatatokea(Chanzo cha habari:Majira 26/02/2011,pp 1&4).
My take
Naona sasa baadhi ya mawaziri wa JK wanaanza kukubali kuwa CHADEMA inatisha,CCM sasa inabidi wajipange upya vinginevyo watang'olewa madarakani.
Bi Simba ambaye ni Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na watoto alisema hayo jana katika mkutano wa kwanza wa Baraza la UWT katika wilaya ya kinondoni akiwa kama mgeni rasmi ambapo mwenyeji wake alikuwa ni mwenyekiti wa UWT wa wilaya hiyo Bi Anna Makete.
Bi Simba alisema kuwa katika kipindi kifupi kilichopita na sasa,CCM imepoteza umaarufu wake kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo mfumo wao wa sasa, kutoendana na kizazi kipya ambacho asilimia kubwa ni vijana,kuzidiwa na manano ya propaganda za vyama vya upinzani na kusababisha kushindwa kujibu mapigo na kuwa wanyonge,makundi ndani ya chama,ubinafsi pamoja vijana kukosa uwezesho wa ujasiriamali ndani ya chama.
Alitaja sabubu nyingine kuwa ni mfumo uliotumika mwaka jana kuwapata wagombea katika nafasi mbalimbali za uongozi uliochangia kuwapoteza wana CCM pia wananchi kuchelewa kumtambua mgombea wao na mambo mengine madogo madogo.
Akizungumzia umaarufu wa CHADEMA alisema umetokana na mfumo na sera walionayo sasa,DKt Willbrod Slaa kuibua suala la Richmond na Dowans bungeni na kutaka kuvunja mkataba ambao umesababisha nchi kushitakiwa na kutakiwa kulipa mabilioni ya fedha pamoja na njama za wafadhili wa chama hicho kutoka nje ya nchi kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kuking'oa CCM madarakani.
Nyingine ni kupanda kwa gharama za maisha kutokana na sababu mbalimbali ambayo yanamgusa kila mtu alisema kwamba CHADEMA imetumia mwanya huo kufanya maandamano huku wakidai kwamba ni kutokana na CCM kuwepo madarakani.
Bi Simba alisema kuwa kitendo cha CHADEMA kufanya maandamano jijini Mwanza juzi ni kutafuta umaarufu na si vinginevyo huku wakisingizia kupinga malipo ya Dowans na mgawo wa umeme.
Alisema kuwa kilichokuwa kinazungumzwa na viongozi wa CHADEMA juzi kilikuwa tayari kimefikishwa mezani na kinafanyiwa kazi ikiwemo mazungumzo kati ya mmiliki wa Dowans na Serikali ili kuondoa suala la mgawo wa umeme pamoja na mkakati wa kushusha bei ya bidhaa muhimu kama sukari.
Bi Sophia alisema hatua iliyofikia ya kutaka serikali ilipe shs bilioni 94 za Dowans inatokana na mipango ya Dkt.Slaa na wanasiasa wengine kutaka mkataba uvunjwe huku wakijua matatizo yatatokea(Chanzo cha habari:Majira 26/02/2011,pp 1&4).
My take
Naona sasa baadhi ya mawaziri wa JK wanaanza kukubali kuwa CHADEMA inatisha,CCM sasa inabidi wajipange upya vinginevyo watang'olewa madarakani.