Kinachofanya iwe na mziki laini sana ni mpangilio wa Front speakers na hizo surrounds speakers. Mwambie ahakikishe speaker zenye alama L(Left) zote ziko upande mmoja na zenye R(Right) zote ziko upande mmoja pia! Unapochanganya front L & surround R upande mmoja huwa inafanya kama ku-neutralize Bass ya Sub-Woofer hapo! Pia Home theatre za Sony huwa surrounds speakers zinakaa kwenye position ya kuangaliana na Front speakers,sio zote unaweka mahali moja! Surronds weka juu nyuma ya makochi yako ziwe zinapiga kwa nyuma yako.
Pia kama anataka kuongeza Bass ahakikishe ameconnect HDMI na TV yake, then DAV iwe kwenye USB au DVD Mode then afungue SETUP, atapata settings za kurekebisha speakers zote kuanzia za mbele mpaka surrounds na level ya volume anayotaka kwa moja moja...kama asipoelewa nitawawekea video hapa ya namna ya kuiset SONY DAV-DZ650.
Hii system ni nzuri sana ni watu wanashindwa tu kuitumia. USB inachagua sana, inatakiwa uwe na Flash Disk genuine, hizi za hovyo hovyo haiplay kabisa na pia kwa USB inaplay Mp3 format na AAC tu kww AUDIO files wakati Video inaplay only XVID(.avi), ukiweka mp4 itacatch audio tu! Ila upande wa DVD ,audio inaplay Mp3, AAC na .flac formats, na video files upande wa DVD inaplay almost zote as long as umeburn CD yako kwa mfumo wa DVD Video. Ndo maana ikaitwa SONY DVD Hometheatre system. Wamefanya makusudi kuondoa luxury kwenye USB ili iendane na TV yake ya SONY BRAVIA ndo maana kwenye remote ya hiyo home theatre kuna mahali imeandikwa BRAVIA sync, hapo kama una TV ya SONY BRAVIA unakuwa unacontrol kila kitu kwa remote ya Radio.
Pia kwa wale wapenda movies huu ndo mdude wetu sasa, kwenye surrounds control kuna mode inaitwa DOLBY PL, hii ukifungua inaruhusu surrounds zipige kwa 5.1 Dolby stereo channels, kwa kweli utajihisi kama uko Cinema kama umepangilia speaker zako vizuri.
All the best, ila nikuhakikishie hakuna mziki wa maana kama SONY HOME THEATRE
View attachment 1063029
Sent using
Jamii Forums mobile app