Sonona! imenielemea. Msaada!

Sonona! imenielemea. Msaada!

Duh! Ila hii Dunia Kweli imejaa changamoto 😥

Pole Sana mkuu kwa yote unayopitia Mungu akufanyie wepesi jamani 🙏
 
Mkuu

Hongera sana KWA kuandika!

Hongera KWA kutojiua hadi Sasa!

Hongera kwakua Mama yako mzazi alizaa Mwanamme wa shoka!

Hongera KWA kuwa mpambanaji!

Hongera kwa kuwa wewe ni mtu muhimu Sana Tanzania imewahi kumpata!

Hongera KWA kuuona mwaka huu!

Hongera KWA kuwa wewe ni mshindi wa yote!!


Sasa Basi!


Ingia chumbani mwako umshukuru Mungu umwambie unamshukuru KWA wewe ni mshindi!

Halafu kuhusu wanaokutegemea Hao wagonjwa mwambie hivi

"Ewe Mungu Hawa ni Watoto wako umewaumba wewe !Amua mstakabali waO Sasa hivi ,kama ni mapenzi yako waponye Sasa kama sio mapenzi yako wachukue Sasa na unipe ujasiri wa kuwazika KWA amani na furaha kuu!!!

Ongezea hivi

"Hatma ya Maisha yao ipo kwako mimi hata nikiwahangaikia kiasi Gani siwezi fanya chochote juu ya uhai waO!naomba uamue Sasa unawaponya au unawachukua!

"Inatosha Sasa naomba nipumzike na haya niishi VIZURI KWA furaha tele!!NATAKA HAYO SASA NIMECHOKA!

Baada ya hapo utatoka ukiwa Mpya kabisa!

Asisahau pia kujiombea na yeye mwenyewe ili mwenyezi Mungu aweze kuamua moja kati ya kumponya na matatizo yanayo mwandama au kumchukua mapema ili akapumzike alipoandaliwa.
 
Sijui niandike nini nimeishia Julia tuu na kukumbuka mapito yangu hakika mng wa mbinguni anayo sababu na hatokuacha.Amini wapendwa wako wamekwenda kupumzika na mateso ya hapa Duniani
 
Nimekuwa ni kama sielewi Dunia inavyoenda, mawazo mengi mabaya yanazunguka kichwani mwangu na sijui nitaweza vipi kuiepuka hali hii ambayo inazidi kuweka mizizi na nashindwa kuimudu.

Haya yalianza miaka miwili iliyopita ambapo kwenye familia yetu tulipoipoteza nguzo muhimu, nguzo Baba. Aliondoka na kutuachia wagonjwa wawili ambao wakati wa uwepo wake alipambana kuhakikisha wapo salama. Mdogo wangu alikuwa na kichwa kikubwa na kilijaa maji mara kwa mara, pia alimuacha Mama ambae alikuwa na maradhi makubwa kidogo ambayo yalihitaji pesa nyingi sana kukabiliana nayo. Baada ya msiba huo Wadai wakajitokeza na kuchukua asilimia kubwa ya mali zilizoachwa na ni kweli, kwa sababu ya uhitaji wa pesa wakati huo alijikuta akiingia kwenye madeni makubwa.

Mzigo nikaubeba na ikawa ni mimi na wagonjwa na familia yangu ya mke na watoto wawili. Nilipambana kadri ya uwezo wangu, nikaingia kweny moja ya bank na kukopa kwa dhamana ya kazi, mzigo bado ukawa mgumu kuubeba lakini sikukata tamaa hadi pale ambapo kila njia ikawa haiwezi kunitoa na hapo ndipo kichwa kikajaa mawazo mengi ambayo sasa yamenifikisha kwenu waungwana.

Nikiwa bado kwenye mtanziko wa kifedha, mdogo wangu aliyekuwa mgonjwa aliaga Dunia mwaka Jana mwezi wa nane, likawa tatizo lingine kwa Mama ambae alianza kupata nafuu, alirudi kuugua upya Kwa sababu mdogo wangu alikuwa ni kipenzi chake angalau kuliko sisi wengine.

Mwaka huohuo mwanzoni mwa mwezi wa kumi na mbili binafsi nikaguswa moyo wangu, mwanangu wa miaka sita alifariki kwa homa ya siku mbili, hapo tatizo likaongezeka zaidi Kwa sababu nikawa na kazi ya kumliwaza mke wangu, mama yangu nae akiwa mikononi mwangu.

Nikiwa bado sijapona vizuri maumivu ya wapendwa wangu, mwezi huu tareh 20 nikapoteza tena mwanangu wa mwisho wa miaka minne. Hakika hapa nilipo kila wazo baya naona sahihi... Huku Mama mgonjwa, sasa ni mke wangu nae hayupo Sawa, anazimia kila mara. Nimejibeba kijasiri Sana lakini naona kama akili imeganda hivi.

Nahitaji ushauri wenu wa hali na mali nijue najiondoaje kwenye hali hii.... Mwenye kuweza kunipigia namba yangu ni 0785256311.

Mungu awabariki
Pole sana muombe mungu atakusaidia
 
mwezi huu tareh 20 nikapoteza tena mwanangu wa mwisho wa miaka minne
Pole sana mkuu Mungu akufanyie wepesi.
Naona hapo umepitiwa, huu ni mwezi wa pili tarehe za mwanzo. Urekebishe ili kuweka kumbukumbu vizuri.
 
1. Muombe mungu
2. Nenda kwa mchungaji akuongoze kwenye maombi yako na familia ili Mungu akuvushe kwenye hlo jaribu na kama mazindiko yatoke
3. Nenda hospital kwa psychologist
Akusaidie kisakolojia
4. Ukiwa kama mtoto wa kiume unapaswa kuvumilia na kutokata tamaa kwan ww ndio msaada wa pekee wa kuisadia familia yako upo vitani haupaswi kukimbia uwanja wa mapambano pambana kufa kupona mpk uibuke mshindi kwa familia yako ili ujenge heshima na uwe mfano kwa wanaopitia kama unayoyapitia. MUNGU AKUSAIDIE NA KUKUONGOZA KWENYE HILO JARIBU
 
- maisha safari ndefu sana
-Kesho ni fumbo
  • chochote kinaweza kutokea.
  • usipange sana mipango
-
pia usihesabu mabaya! maana mabaya yanaongozanaga kama mabehewa ya treni, Muburi 3:1 -8
Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake: kuna wakati wa kulia/kucheka wakati wa kupata/kupoteza ...wakati wa vita/amani..
Ulizaliwa pekeako, hukuja na mtu hatma yako ni yako! ni vile hatujiandai kuyakabili magumu tunajisahau sana..ila yote hayo hayana budi kutokea, yameshatokea jikaze mwanaume mambo ni magumu ila jikaze beba familia iliyobaki bado Mungu anampango na nyinyi... kama rdhiki inapatikana Mshukuru Mungu usonge mbele , hata usiku uweje patakucha tu hata pakikucha uko juu ya mawe ila pamekucha tayari... kwasasa unaweza usijue chanzo ila Move on ..

watakaovumilia mpaka mwisho ndio watakombolewa
 
Pole sana Mkuu.

Wewe ni jasiri sana, ipo siku Furaha yako itarejea na Familia itastawi tena..
 
Pole sana ndugu, hebu rudi magotini kwa kwa maombi ya mfungo. Omba kwa imani yako na muombe Mungu akutakase na atakase familia yenu.

Kama una chochote kitu nunua vyakula vyakula chagua kituo cha watoto wa mazingira magumu katoa hiyo sadaka yako na muombe Mungu akuguse kupitia sadaka hiyo.

Tafuta mtumishi wa Mungu unayeona ana nguvu za kiroho kushinda za kwako, mweleze na akuwekee mkono akuombee. NB: watumishi wa Mungu wenye nguvu sio hawa wamiliki wa makanisa haya makubwa makubwa.

Kuhusu mikopo inabidi ulisolve kibinadamu, kwa kubadili kazi yako ya sasa kama inawezekana, au kama una chochote muwekezee wife afanye aingize hata kidogo mjikwamue na mikopo.
 
Siku Mwenyezi Mungu atakufunulia yote yalojificha !

Kama uko honestly hujawaumiza watu kama makosa ni haya ya bahati mbaya ya kibinadamu Mungu atakuhurumia na kukusamehe na kukupa fidia ya ulowapoteza.

Achekae mwisho hucheka sana.

Mwenyezi Mungu atakufuta machozi yako.

Mtafakali yeye na kutenda mema.

Jivike subira na ustahamilivu Mkuu.

Imeandikwa;

“Kheri wanao subiri “
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom