Right Marker
Senior Member
- Apr 30, 2018
- 194
- 624
Miezi kadhaa nyuma nilipokea taarifa kutoka kwa vyanzo vyangu vya taarifa vilivyopo Mbeya mjini vikisema kwamba huko mkoa wa Songwe kuna kundi binafsi linaitwa SONGWE CONNECTION ambalo lina makadirio ya wanachama 3,800.
Taarifa niliyoipokea ni kuwa kuna mkanganyiko wa kimaslahi katika kundi hilo na huenda baadae ikaleta shida. Mara tu nilipopata taarifa hizo niliwatuma watu wangu wafike huko Songwe wafuatilie kwa kina ndipo leo wamekuja na majibu yafuatayo.
1. Ni kundi lenye wanachama 3,800 ambalo linaendeshwa kwa njia ya "Whatsapp Groups" na limegawanywa katika makundi manne kama ifuatavyo.
~ GROUP A (wanachama 1000).
~ GROUP B (wanachama 1000).
~ GROUP C (wanachama 1000).
~ GROUP D (wanachama 800).
2. Kila mwanachama katika wanachama 3800 amejiunga kwenye kundi kwa Tshs 28,000.
(28,000 × 3800 = 106,400,000)
3. Fedha zinazochangishwa kwa wanachama wote zinahifadhiwa benki kwa akaunti yenye jina binafsi, ambapo mpaka sasa hakuna mwanachama anayejua akaunti yao ina kiasi gani cha fedha.
4. Kwavile wanasema ni kundi la kusaidiana katika misiba, mwanachama wa kundi moja lenye wanachama 1000 akifiwa, kila mwanachama ndani ya kundi moja anachanga Tsh 5,000 kisha mfiwa anapewa Tsh 2,500,000.
(5000 × 1000 = 5,000,000).
5. Uchangishaji wa fedha za matukio unafanywa kwa njia mbili. Njia ya kwanza ni njia ya akaunti ya benki (akaunti binafsi). Njia ya pili ni njia ya kutuma kwenye simu binafsi za viongozi.
6. Kila mwanachama anatakiwa kuchanga Tsh 25,000 kwa ajili ya kwenda kuwatazama watu wenye uhitaji maalumu. (25,000 × 1000 = 25,000,000)
7. Kila mwanachama katika kundi moja anatakiwa kuchanga Tshs 75,000 kwa ajili ya kuanzisha mradi wa BarberShop moja. (75,000 × 1000 = 75,000,000)
8. Lakini pia upande wa kundi lingine lenye watu 1000 lilichanga fedha za kununua coaster. Kila mwanachama kati ya wanachama 1000 alichanga Tshs 100,000.
(100,000 × 1000 = 100,000,000).
Mwisho
Baadhi ya wanachama (waliojitoa) wamehofia kwamba huenda likawa ni kundi la kuwanufaisha watu wachache (viongozi wa kundi) huku likitumia mwamvuli wa kutoa misaada.
RIGHT MARKER
DAR ES SALAAM
Taarifa niliyoipokea ni kuwa kuna mkanganyiko wa kimaslahi katika kundi hilo na huenda baadae ikaleta shida. Mara tu nilipopata taarifa hizo niliwatuma watu wangu wafike huko Songwe wafuatilie kwa kina ndipo leo wamekuja na majibu yafuatayo.
1. Ni kundi lenye wanachama 3,800 ambalo linaendeshwa kwa njia ya "Whatsapp Groups" na limegawanywa katika makundi manne kama ifuatavyo.
~ GROUP A (wanachama 1000).
~ GROUP B (wanachama 1000).
~ GROUP C (wanachama 1000).
~ GROUP D (wanachama 800).
2. Kila mwanachama katika wanachama 3800 amejiunga kwenye kundi kwa Tshs 28,000.
(28,000 × 3800 = 106,400,000)
3. Fedha zinazochangishwa kwa wanachama wote zinahifadhiwa benki kwa akaunti yenye jina binafsi, ambapo mpaka sasa hakuna mwanachama anayejua akaunti yao ina kiasi gani cha fedha.
4. Kwavile wanasema ni kundi la kusaidiana katika misiba, mwanachama wa kundi moja lenye wanachama 1000 akifiwa, kila mwanachama ndani ya kundi moja anachanga Tsh 5,000 kisha mfiwa anapewa Tsh 2,500,000.
(5000 × 1000 = 5,000,000).
5. Uchangishaji wa fedha za matukio unafanywa kwa njia mbili. Njia ya kwanza ni njia ya akaunti ya benki (akaunti binafsi). Njia ya pili ni njia ya kutuma kwenye simu binafsi za viongozi.
6. Kila mwanachama anatakiwa kuchanga Tsh 25,000 kwa ajili ya kwenda kuwatazama watu wenye uhitaji maalumu. (25,000 × 1000 = 25,000,000)
7. Kila mwanachama katika kundi moja anatakiwa kuchanga Tshs 75,000 kwa ajili ya kuanzisha mradi wa BarberShop moja. (75,000 × 1000 = 75,000,000)
8. Lakini pia upande wa kundi lingine lenye watu 1000 lilichanga fedha za kununua coaster. Kila mwanachama kati ya wanachama 1000 alichanga Tshs 100,000.
(100,000 × 1000 = 100,000,000).
Mwisho
Baadhi ya wanachama (waliojitoa) wamehofia kwamba huenda likawa ni kundi la kuwanufaisha watu wachache (viongozi wa kundi) huku likitumia mwamvuli wa kutoa misaada.
RIGHT MARKER
DAR ES SALAAM