PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,202
- 8,788
Kwenye taarifa ya TBC1 jana , kulikuwa na habari za kimiujiza kutoka huko Songea, ambapo kuna mahali pamegundulika kuwa na kisima au chanzo cha pesa cha kipekee, na watu wengi wa rika mbalimbali wamehamia hapo na wanajiokotea noti za denomination mbalimbali(shs 500/=,1000/=, 2000/= 5,000/= na 10,000!
Akiripoti tukio hilo la ajabu, mwakilishi wa TBC1 Songea, Gerishon Msigwa aliwasili eneo la tukio, ambapo alihojiana na umati wa watu waliokuwa hapo wakisuburi neema hiyo ya bure, na wengi walikiri kuokota mabunda ya noti, wengine laki moja, wengine 20,000, wengine 5000 na kadhalika, na kwamba ni siku kadha sasa tangu miujiza hiyo ilipoanza kutendeka eneo hilo! ....mwanajamvi ushawahi kubahatika hivi maishani?
Mimi nimejaribu kufikiria juu ya hili suala, nahisi ni aina fulani ya ushirikina, ambapo baadaye utakuja leta madhara kwa baadhi ya watu, hasa wanaozimiliki baada ya kuokotwa!
Ama kweli Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Bombambili huko Songea!
Akiripoti tukio hilo la ajabu, mwakilishi wa TBC1 Songea, Gerishon Msigwa aliwasili eneo la tukio, ambapo alihojiana na umati wa watu waliokuwa hapo wakisuburi neema hiyo ya bure, na wengi walikiri kuokota mabunda ya noti, wengine laki moja, wengine 20,000, wengine 5000 na kadhalika, na kwamba ni siku kadha sasa tangu miujiza hiyo ilipoanza kutendeka eneo hilo! ....mwanajamvi ushawahi kubahatika hivi maishani?
Mimi nimejaribu kufikiria juu ya hili suala, nahisi ni aina fulani ya ushirikina, ambapo baadaye utakuja leta madhara kwa baadhi ya watu, hasa wanaozimiliki baada ya kuokotwa!
Ama kweli Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Bombambili huko Songea!