Mwanamke unakamata nyoka😳 wanawake wa siku hizi hamtaki jiheshimu hata mimi nisingerudi
Mi kituo changu Cha kwanza Cha Kaz kilikuwa Chaka huko iringa,nipo sebuleni namwona huyo kajaa,nikaendelea kula ugali(kifutu afu black) nimwangalie amechagua kukesha wapi sikuhiyo...namwona huyo anaingia chumbani😳 nikajisemea onhoo,wewe utakuwa dume si bure🙄....nilichofanya ni kutoka pale Kwa kunyata na kumzungukia Kwa nyuma...lilikuwa ni suala la kumkamata shingo chap na kumkaba Kwa nguvu....akawa anafura huku kazungusha mwili wake mkononi....roho ikaniambia,hii ngoma ukilegeza tu mkono umekufa....so nikafanya kutaiti Kwa nguvu Ili akose pumzi ...nikaona analegea na mwili wake unatoka mikononi nikajua tayari hapa...nikamtupia chini puu,we bhana wee,Kumbe alikuwa ananizuga tu ili nimwachie...alivyokimbia nami nikakimbilia ndani kujifungia.sijui alikimbilia Chaka gani....lile tukio alilishuhudia mkuu msaidizi ...alikuja kuulizia ombi la kupewa game aliloomba Jana yake....nakumbuka hadi nahama pale hakuwa kanyaga Tena kwangu hata kumchekea alikuwa hataki nimchekee.😏sijui aliwaza Nini🤔🤦