Money Penny
JF-Expert Member
- Jun 20, 2016
- 18,204
- 17,560
- Thread starter
- #201
Wakiwa wanatoka bagamoyo kuwahi bunju ambapo James alitegesha helikopta yake yakuwachukuwa kwenda kenya, uuuwi wakati wanashuka sasa kwenye gari watembee kwenda kwenye ndege James akasikia bonge la ngumi, taaaaah! Akaanguka chini, Doreen kashikiliwa na majitu yenye miraba 4, James akapigwa hakuna mfano, Doreen akabakia analia tu, James jamani mwacheni tafadhali James anamlilia, mara gari inaingia uuuwi Don Lucifer! Akashuka zake kwenye gari akamwangalia msaliti wake James na Doreen akamfuata James, akawaambia ma body guard wake wamsimamishe, amsha na wewe James akiwa amejaa madamu, uso hautizamiki, ni sheedah!
Lucifer: unampeleka wapi mke wangu? Unataka kumtorosha kwenda wapi labda?!
James: kimya!
Lucifer: mfungeni pingu mpelekeni alipokuwa Safaree kwa mwezi mzima, ila apewe chakula na uso anawishwe
Body guards hao wakamwingiza kwenye gari haoo wakaondoka akabakia Lucifer na Doreen na dereva wa Lucifer kwenye gari
Doreen akamfuata Lucifer akaanza kumpiga mangumi ya kifua! Kwanini umenidanganya, huku analia, kwanini unamjeruhi James amekufanya nini sasa?! Mimi sikupendi kwa kunidanganya kwanini lakini Lucifer umeamua kuniharibia maisha lakini kwanini?! Akalia wee Lucifer anamwangalia tu, Doreen akalia mpaka akaanguka chini, akazimia, Lucifer akambeba akamwingiza kwenye gari haooo wakaondoka.
Safaree nae kozi ikakaribia kusiha akafurahi sana nini maskini, anauhakika wa kufaulu mitihani Safaree amekuwa sober, havuti tena bangi, hanywi pombe tena, anatafuta nafasi ya pili na kurudisha uaminifu kwa Lucifer ah! Boss wake akampenda sana akaandika ripoti nzuri kwa Lucifer, Lucifer alipoiona akacheka tu, kweli au uongo akawa anajiuliza.
Carrie akawa analea mtoto, sasa ana miezi 10, George amesharudishwa kazini Carrie akawa anaboreka kukaa bondeni nini, hana marafiki akawa anaenda na mwanae kutembea, hana dada wa kazi muda wote yupo na mwanae, wakati mwengine mama mkwe akija anakaa na mjukuu wake nini, Carrie ndio anapumua. George akawa amepona kabisaa hana shida tena, Doreen akazindua mechi, wanampeleka mtoto kwa mama mkwe, mechi inapigwa kwenye gari, nyumbani, yani ile ya kulipiza kisasi... wanajikumbushia enzi za ujana wao kabla hajampata Junior wao. Carrie akafurahi, maana alikaa mkavu kama gogo kwa muda akisubiri mume atengemae. George akammilikisha mali zake zote Carrie na mwanae, akamwonyesha mali ambazo alizificha wakiwa kwenye uchumba Carrie moyoni anasema kweli sitakufa maskini, cha! Kumbe nimelala maskini nimeamka tajiri yeleuuuuwi mmachame nimehit BINGO! Akaambiwa kuwa mtoto akianza shule day care nini, itabidi waende Switzerland akamtambulishe kwenye restaurant yao ambayo wanamiliki hisa na mzungu. Carrie akafurahi sana kha! Kweli Bingo ni Bingo!
Adrienne na Shawn wakarudi zao Oysterbay kwenye nyumba yao ambayo walipangisha walipoenda uingereza wakapangisha nyumba yao mpaka wanarudi kodi ya mpangaji ikawa imekeesha wakarudi. Sia na Shawn Junior wamekua wakubwa wana mwaka sasa wanatembea wazuri hao kama mashombe shombe, wazuri ukiwaangalia unawatamani
Chanel na Pedeshee wapo kwenye nyumba yao Kunduchi, wameshazoea maisha, wameshazoeana, wanapendana, Chanel amemaliza shule yake ya QT anajiandaa kwenda kufanya diploma ya biashara, akapata chuo posta akawa anasoma diploma yake. Siku akaenda kilipa ada yake bank CRDB, amemaliza anatoka wakagongana na Mark, kuja kushtuka ni Mark wakacheka pale wanasalimiana, wanajuliana hali kama hawajagombana, wakasalimiana pale Chanel akamtania nimekumiss kweli, Mark akamwambia hata mimi pia, lini tunafanya uzinduzi kurudisha penzi, Chanel akawa anacheka tu Mark bwana hauachi tu, Mark akamwuliza bado upo na yule Emolo wako? CHANEL akamjibu anaitwa Marion bwana acha dharau! Wakawa wanacheka hapo, Mark anamwambia naona shemeji anakutunza umependeza sana naona umenenepa kabisaa au una mimba?! Chanel akamjibu asante tupo bwana, mara anaona kadada kadogo kadogo keupe kana ngozi kama ya Chanel anamsemesha, Mark nimemaliza tuondoke tukawachukue watoto Airport. Chanel akashangaa, akatambulishwa huyu mke wangu anaitwa Irene, ni mmeru mwenzio, Chanel akacheka nimefurahi kukufahamu Irene, haya nawatakia siku njema, akaondoka Chanel, Mark akageuka anamwangalia tu mtoto Jojo anaondoka. Uuuwi!
Huku kwa Don Lucifer mambo nayo yakawa kama kuzimu, tangu wamebambwa Bunju ni miezi 2 sasa imepita Doreen hataki kuongea, kuoga, kula, amekaa tu kitandani. Lucifer akawa anamhudumia kwa kila kitu, usiku Lucifer akiwa amelala Doreen anaamka anaenda kwenye shimo alilofungiwa James anaanza kumwongelesha, kiiila siku kea muda wa miezi 2 usiku wa manane, ma body guard wakamwambia Lucifer kitendo cha Doreen, Lucifer akawaambia muacheni afanye anachotaka na akitaka mumfungue James fungueni lakini asitoke hapa ndani. baada ya miezi 3 Doreen akakaa sawa akaamwabia Lucifer nipeleke kwa James, Lucifer akamwonea huruma akaamua ampeleke maana Doreen alishamwambia nakupa nafasi ya mwisho, Doreen akaoga akajipamba na kujipara mwenyewe, akamkumbatia Lucifer akamwambia asante kwa kunitunza, akambusu mdomoni, akamshika mkono akamwambia twende kwa James, kufika kwa James, walishamfungua kabla washamsafisha wakamvalisha suti nzuri kapendeza wakakutana Library ya Lucifer wakawa wanaongea wa4 na body guard
Doreen kumwona James akamkimbilia akamkumbatia, James anaogopa mara body guard anataka kusogea awaachanishe, Lucifer akamkataza. Doreen akambusu James mdomoni kwa muda mrefu, eh Lucifer roho inamuuma anavumilia anajua ameshaharibu na atamkosa Doreen. Baadae Doreen akafura machozi, wakakaa kwenye kiti, Lucifer akaja akaaa kwenye kiti chake, wakaanza kuongea
Doreen akamwambia Lucifer, dhambi zooote alizofanya James naomba umsamehe, mimo ndio nilimwambia aje anitoroshe, niliiba namba yake ya Mexico kwenye simu yako nikawa naongea nae, bila wewe kujua, mimi ndio nilitaka kutoroka nae baada ya kujua umenidanganya nadhani upendo wangu kwa James haukuisha kwasababu sio rahisi mwanaume aliekubikiri ukamsahau ghafla hali ni wewe unetutenganisha, naomba umsamehe arudi kazini tafadhali, kwa niaba yangu dhambi zake naomba nilipe mimi? Kama unataka kumuua niue mimi, usimfanye ubaya muache aendelee na maisha yake, nampenda sana James nafasi yake hautakaa uje uichukue Lucifer kwenye moyo wangu, haitakaa itokee. Lakini si unakumbuka ahadi yetu kabla sijakukubalia univishe pete?! Umenikosea sana na ningeondoka lakini nimekubali kukaa kwako miezi 2 hata sijui kwangu kunafananaje. Akasimama pembeni akaendelea kuongea Wala sitaki kujua kwanini ninyi wawili mlinichezea kama mlivyofanya?! Wote mmeniudhi na michezo yenu ya kijinga. Lakini James mimi kama Doreen nimeamua kubaki na Lucifer, hata kama simpendi, lakini nimechagua kukaa nae na kuishi nae, wewe endelea na maisha yako popote duniani, fanya kila unachotaka ikiwezekana unisahau kama ambavyo na mimi nimejitahidi kukusahau. Hapo James roho inamuuma kama nini anatamani auawe tu, hawezi kuangalia Lucifer anashinda hivi hivi yeye akiwa hai!
Lucifer akamwambia James nimekusamehe kama mke wangu anavyotaka, nakuhamishia kikazi Afrika ya Kusini! Mpaka hapo utakapoambiwa vinginevyo! Akapewa kila kitu akaambiwa aondoke usiku ule ule kwenda kufanya kazi, akamkumbatia Doreen akamnong'oneza tutaonana bondeni nina uhakika, akambusu mashavuni akaondoka, Doreen akaanza kulia anamwangalia tu akakimbia nje kwa James akaingia nae kwenye gari kuelekea airport, Lucifer hakumzuia, si unajua ile misemo ya zamani, ukimpenda mtu mwache aende akirudi ujue ni wa kwako tu.
Kwenye gari watu hawataku kuachiana, nahisi walimpa tabu dereva maana sio kwa ile mechi ilopigwa kwenye gari, James akawa anashangaa Doreen imekuwaje hamwogopi hata Don! Maana pale nimechezea mauti katikati ta mlango wa dunua na ahera! Akaona basi ngoja nijiongeze tu kwani Tsh ngapi?! Umo umo kwenye gari uzinduzi kati ya Doreen na James ukaanza mpaka wamefika airport, washafungana goal 1 moja, ndege ikawa bado haijafikia muda wa James kuingia ndani, Doreen akamvuta James mpaka choo cha akina kaka, eh mechi ingine tena, watu wakija wanashangaa mechi za chooni, uuwi, Doreen yupo buzy anakula utamu wa James na mwezetu James nae anahakikisha anampatia dozi ya kisawa sawa! ili amsahau Lucifer! Lakini Lucifer ni Lucifer tu! Nafasi yake haibadilishwi na mtu mwengine! Muda ukapita ikabidi waachane Doreen akachukua Perfume akampaka James ili asiwe ananukia maupwiru kwenye ndege, akambusu kwa mara ya mwisho akamwambia nakupenda nakutakia maisha mema ni vema nibaki na Lucifee kulinda uhai wako tu, maana uhai wako haustahili kupotezwa kwasababu yangu. JAMES akaondoka kwenda kuingia kwenye ndege Doreen analia tu akarudi kwenye gari akarudishwa nyumbani kwa Lucifer. Kufika kwa Lucifer, hakutaka kuongea akaingia kitandani akalala, Lucifer hakumsemesha kitu, Asubuhi akaamka akajiandaa akamfuata Lucifer na kumwuliza kazo yangu ipo?! Lucifer akamwambia ipo, akarudi kujiandaa na breakfast, wakiwa wanakunywa chai, Doreen akaanza kusikia kichefu chefu, akatapika hapo hapo mezani, mmh! Au ni haya mayai yananitia kichefuchefu mbona naskia vibaya, akasimama alete kitambaa kufuta matapishi, akaanza kusikia kizungu zungu, akaanguka chini. Akapelekwa hospitali, majibu kutoka Doreen mjamzito wa miezi 4. LUCIFER akafurahi lakini Doreen hakufurahi, sio kwa ugaidi ule Lucifee alomfanyia James
ITAENDELEA ALHAMISI SAA 5 USIKU
Lucifer: unampeleka wapi mke wangu? Unataka kumtorosha kwenda wapi labda?!
James: kimya!
Lucifer: mfungeni pingu mpelekeni alipokuwa Safaree kwa mwezi mzima, ila apewe chakula na uso anawishwe
Body guards hao wakamwingiza kwenye gari haoo wakaondoka akabakia Lucifer na Doreen na dereva wa Lucifer kwenye gari
Doreen akamfuata Lucifer akaanza kumpiga mangumi ya kifua! Kwanini umenidanganya, huku analia, kwanini unamjeruhi James amekufanya nini sasa?! Mimi sikupendi kwa kunidanganya kwanini lakini Lucifer umeamua kuniharibia maisha lakini kwanini?! Akalia wee Lucifer anamwangalia tu, Doreen akalia mpaka akaanguka chini, akazimia, Lucifer akambeba akamwingiza kwenye gari haooo wakaondoka.
Safaree nae kozi ikakaribia kusiha akafurahi sana nini maskini, anauhakika wa kufaulu mitihani Safaree amekuwa sober, havuti tena bangi, hanywi pombe tena, anatafuta nafasi ya pili na kurudisha uaminifu kwa Lucifer ah! Boss wake akampenda sana akaandika ripoti nzuri kwa Lucifer, Lucifer alipoiona akacheka tu, kweli au uongo akawa anajiuliza.
Carrie akawa analea mtoto, sasa ana miezi 10, George amesharudishwa kazini Carrie akawa anaboreka kukaa bondeni nini, hana marafiki akawa anaenda na mwanae kutembea, hana dada wa kazi muda wote yupo na mwanae, wakati mwengine mama mkwe akija anakaa na mjukuu wake nini, Carrie ndio anapumua. George akawa amepona kabisaa hana shida tena, Doreen akazindua mechi, wanampeleka mtoto kwa mama mkwe, mechi inapigwa kwenye gari, nyumbani, yani ile ya kulipiza kisasi... wanajikumbushia enzi za ujana wao kabla hajampata Junior wao. Carrie akafurahi, maana alikaa mkavu kama gogo kwa muda akisubiri mume atengemae. George akammilikisha mali zake zote Carrie na mwanae, akamwonyesha mali ambazo alizificha wakiwa kwenye uchumba Carrie moyoni anasema kweli sitakufa maskini, cha! Kumbe nimelala maskini nimeamka tajiri yeleuuuuwi mmachame nimehit BINGO! Akaambiwa kuwa mtoto akianza shule day care nini, itabidi waende Switzerland akamtambulishe kwenye restaurant yao ambayo wanamiliki hisa na mzungu. Carrie akafurahi sana kha! Kweli Bingo ni Bingo!
Adrienne na Shawn wakarudi zao Oysterbay kwenye nyumba yao ambayo walipangisha walipoenda uingereza wakapangisha nyumba yao mpaka wanarudi kodi ya mpangaji ikawa imekeesha wakarudi. Sia na Shawn Junior wamekua wakubwa wana mwaka sasa wanatembea wazuri hao kama mashombe shombe, wazuri ukiwaangalia unawatamani
Chanel na Pedeshee wapo kwenye nyumba yao Kunduchi, wameshazoea maisha, wameshazoeana, wanapendana, Chanel amemaliza shule yake ya QT anajiandaa kwenda kufanya diploma ya biashara, akapata chuo posta akawa anasoma diploma yake. Siku akaenda kilipa ada yake bank CRDB, amemaliza anatoka wakagongana na Mark, kuja kushtuka ni Mark wakacheka pale wanasalimiana, wanajuliana hali kama hawajagombana, wakasalimiana pale Chanel akamtania nimekumiss kweli, Mark akamwambia hata mimi pia, lini tunafanya uzinduzi kurudisha penzi, Chanel akawa anacheka tu Mark bwana hauachi tu, Mark akamwuliza bado upo na yule Emolo wako? CHANEL akamjibu anaitwa Marion bwana acha dharau! Wakawa wanacheka hapo, Mark anamwambia naona shemeji anakutunza umependeza sana naona umenenepa kabisaa au una mimba?! Chanel akamjibu asante tupo bwana, mara anaona kadada kadogo kadogo keupe kana ngozi kama ya Chanel anamsemesha, Mark nimemaliza tuondoke tukawachukue watoto Airport. Chanel akashangaa, akatambulishwa huyu mke wangu anaitwa Irene, ni mmeru mwenzio, Chanel akacheka nimefurahi kukufahamu Irene, haya nawatakia siku njema, akaondoka Chanel, Mark akageuka anamwangalia tu mtoto Jojo anaondoka. Uuuwi!
Huku kwa Don Lucifer mambo nayo yakawa kama kuzimu, tangu wamebambwa Bunju ni miezi 2 sasa imepita Doreen hataki kuongea, kuoga, kula, amekaa tu kitandani. Lucifer akawa anamhudumia kwa kila kitu, usiku Lucifer akiwa amelala Doreen anaamka anaenda kwenye shimo alilofungiwa James anaanza kumwongelesha, kiiila siku kea muda wa miezi 2 usiku wa manane, ma body guard wakamwambia Lucifer kitendo cha Doreen, Lucifer akawaambia muacheni afanye anachotaka na akitaka mumfungue James fungueni lakini asitoke hapa ndani. baada ya miezi 3 Doreen akakaa sawa akaamwabia Lucifer nipeleke kwa James, Lucifer akamwonea huruma akaamua ampeleke maana Doreen alishamwambia nakupa nafasi ya mwisho, Doreen akaoga akajipamba na kujipara mwenyewe, akamkumbatia Lucifer akamwambia asante kwa kunitunza, akambusu mdomoni, akamshika mkono akamwambia twende kwa James, kufika kwa James, walishamfungua kabla washamsafisha wakamvalisha suti nzuri kapendeza wakakutana Library ya Lucifer wakawa wanaongea wa4 na body guard
Doreen kumwona James akamkimbilia akamkumbatia, James anaogopa mara body guard anataka kusogea awaachanishe, Lucifer akamkataza. Doreen akambusu James mdomoni kwa muda mrefu, eh Lucifer roho inamuuma anavumilia anajua ameshaharibu na atamkosa Doreen. Baadae Doreen akafura machozi, wakakaa kwenye kiti, Lucifer akaja akaaa kwenye kiti chake, wakaanza kuongea
Doreen akamwambia Lucifer, dhambi zooote alizofanya James naomba umsamehe, mimo ndio nilimwambia aje anitoroshe, niliiba namba yake ya Mexico kwenye simu yako nikawa naongea nae, bila wewe kujua, mimi ndio nilitaka kutoroka nae baada ya kujua umenidanganya nadhani upendo wangu kwa James haukuisha kwasababu sio rahisi mwanaume aliekubikiri ukamsahau ghafla hali ni wewe unetutenganisha, naomba umsamehe arudi kazini tafadhali, kwa niaba yangu dhambi zake naomba nilipe mimi? Kama unataka kumuua niue mimi, usimfanye ubaya muache aendelee na maisha yake, nampenda sana James nafasi yake hautakaa uje uichukue Lucifer kwenye moyo wangu, haitakaa itokee. Lakini si unakumbuka ahadi yetu kabla sijakukubalia univishe pete?! Umenikosea sana na ningeondoka lakini nimekubali kukaa kwako miezi 2 hata sijui kwangu kunafananaje. Akasimama pembeni akaendelea kuongea Wala sitaki kujua kwanini ninyi wawili mlinichezea kama mlivyofanya?! Wote mmeniudhi na michezo yenu ya kijinga. Lakini James mimi kama Doreen nimeamua kubaki na Lucifer, hata kama simpendi, lakini nimechagua kukaa nae na kuishi nae, wewe endelea na maisha yako popote duniani, fanya kila unachotaka ikiwezekana unisahau kama ambavyo na mimi nimejitahidi kukusahau. Hapo James roho inamuuma kama nini anatamani auawe tu, hawezi kuangalia Lucifer anashinda hivi hivi yeye akiwa hai!
Lucifer akamwambia James nimekusamehe kama mke wangu anavyotaka, nakuhamishia kikazi Afrika ya Kusini! Mpaka hapo utakapoambiwa vinginevyo! Akapewa kila kitu akaambiwa aondoke usiku ule ule kwenda kufanya kazi, akamkumbatia Doreen akamnong'oneza tutaonana bondeni nina uhakika, akambusu mashavuni akaondoka, Doreen akaanza kulia anamwangalia tu akakimbia nje kwa James akaingia nae kwenye gari kuelekea airport, Lucifer hakumzuia, si unajua ile misemo ya zamani, ukimpenda mtu mwache aende akirudi ujue ni wa kwako tu.
Kwenye gari watu hawataku kuachiana, nahisi walimpa tabu dereva maana sio kwa ile mechi ilopigwa kwenye gari, James akawa anashangaa Doreen imekuwaje hamwogopi hata Don! Maana pale nimechezea mauti katikati ta mlango wa dunua na ahera! Akaona basi ngoja nijiongeze tu kwani Tsh ngapi?! Umo umo kwenye gari uzinduzi kati ya Doreen na James ukaanza mpaka wamefika airport, washafungana goal 1 moja, ndege ikawa bado haijafikia muda wa James kuingia ndani, Doreen akamvuta James mpaka choo cha akina kaka, eh mechi ingine tena, watu wakija wanashangaa mechi za chooni, uuwi, Doreen yupo buzy anakula utamu wa James na mwezetu James nae anahakikisha anampatia dozi ya kisawa sawa! ili amsahau Lucifer! Lakini Lucifer ni Lucifer tu! Nafasi yake haibadilishwi na mtu mwengine! Muda ukapita ikabidi waachane Doreen akachukua Perfume akampaka James ili asiwe ananukia maupwiru kwenye ndege, akambusu kwa mara ya mwisho akamwambia nakupenda nakutakia maisha mema ni vema nibaki na Lucifee kulinda uhai wako tu, maana uhai wako haustahili kupotezwa kwasababu yangu. JAMES akaondoka kwenda kuingia kwenye ndege Doreen analia tu akarudi kwenye gari akarudishwa nyumbani kwa Lucifer. Kufika kwa Lucifer, hakutaka kuongea akaingia kitandani akalala, Lucifer hakumsemesha kitu, Asubuhi akaamka akajiandaa akamfuata Lucifer na kumwuliza kazo yangu ipo?! Lucifer akamwambia ipo, akarudi kujiandaa na breakfast, wakiwa wanakunywa chai, Doreen akaanza kusikia kichefu chefu, akatapika hapo hapo mezani, mmh! Au ni haya mayai yananitia kichefuchefu mbona naskia vibaya, akasimama alete kitambaa kufuta matapishi, akaanza kusikia kizungu zungu, akaanguka chini. Akapelekwa hospitali, majibu kutoka Doreen mjamzito wa miezi 4. LUCIFER akafurahi lakini Doreen hakufurahi, sio kwa ugaidi ule Lucifee alomfanyia James
ITAENDELEA ALHAMISI SAA 5 USIKU