Mess
JF-Expert Member
- Mar 2, 2009
- 661
- 181
Mwanzoni mwa mwezi huu kuna jamaa alitoka kwenye mizunguko yake ya maisha (anakaa majohe kwa mkolemba) alipofika pale kwa mkolemba alikodi piki piki na yule dereva wa piki piki alimbeba na kumfikisha nyumbani kwake. Yule bwana kwa bahati mbaya hakuwa na change akamwambia mwendesha piki piki kuwa shemeji yako anaoga karibu ndani umsubiri tukulipe, yule bwana wa piki piki akaondoka na alipofika kijiweni akawaambia wenzake kuwa nilitaka kupolwa piki piki ila alieleza jinsi mkasa huo ulivyotokea.
Hamadi yule bwana alikuwa na piki piki yake na akawa ameongea na mkewe kuwa twende pale kuna mtu wa piki piki aliyenileta sikumlipa tukamlipe ile kabla hajafika vizuri yule dogo akasema mwizi wa piki piki huyu hapa jamani ni kuwa yule mtu walimpiga kweli na sidhani kama alipona. Mimi nilifika baadae hapo nikawauliza watu wa piki piki nikaona kama kila mtu anakimbia kuongelea lile swala kama vile waliona kuwa walifanya kosa. Lakini mke wa yule bwana alitoa maelezo mazuri sana. Polisi walipokuja waliambiwa kuna mwizi wa piki piki kapigwa pale walifika wakachukua mwili bila kuhoji watu wa piki piki, kama waliwahoji basi itakuwa siku nyingine ambayo haikuwa ile.
My take: Serikali iliangalie sana hili kundi la waendesha piki piki na wapewe mafunzo jinsi ya kutenda kazi yao, na polisi wakifika wawashike watu ambao wanaweza saidia upelelezi, mara nyingi tumeona polisi wakiambiwa mwizi huwa hawahangaiki kuchukua malelezo.
Hamadi yule bwana alikuwa na piki piki yake na akawa ameongea na mkewe kuwa twende pale kuna mtu wa piki piki aliyenileta sikumlipa tukamlipe ile kabla hajafika vizuri yule dogo akasema mwizi wa piki piki huyu hapa jamani ni kuwa yule mtu walimpiga kweli na sidhani kama alipona. Mimi nilifika baadae hapo nikawauliza watu wa piki piki nikaona kama kila mtu anakimbia kuongelea lile swala kama vile waliona kuwa walifanya kosa. Lakini mke wa yule bwana alitoa maelezo mazuri sana. Polisi walipokuja waliambiwa kuna mwizi wa piki piki kapigwa pale walifika wakachukua mwili bila kuhoji watu wa piki piki, kama waliwahoji basi itakuwa siku nyingine ambayo haikuwa ile.
My take: Serikali iliangalie sana hili kundi la waendesha piki piki na wapewe mafunzo jinsi ya kutenda kazi yao, na polisi wakifika wawashike watu ambao wanaweza saidia upelelezi, mara nyingi tumeona polisi wakiambiwa mwizi huwa hawahangaiki kuchukua malelezo.