Soko la zao la Beetroots

Soko la zao la Beetroots

INSONSILE

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
1,866
Reaction score
2,727
Habarini wana JF.
Naomba kujua soko la zao la beetroot. Mmea huu ingawa hausikiki sana miongoni mwa watanzania, ukijaribu kwenda sokoni unakuta inauzwa ghali kuliko mboga mboga zingine. Nimewaza hivi mtu akiingia shamba akalima kwa wingi vipi soko lake likoje especially kwa Dar? Mimi nipo mkoani lakini nimewaza kama nitalima na nitasafirisha kwa wingi, je soko lake lina uhakika kwa Dar? au kwa export? Naambatanisha picha kwa wale wasioelewa vizuri
 

Attachments

  • Beetroots 1.jpg
    Beetroots 1.jpg
    7 KB · Views: 26
Kwa kiswahili linaitwaje?!
Viazi damu. sina hakika ndo kiswahili fasaha /halisi nimewahi lima ila nilkuwa na tenda na company ya AKO hii ndo ilikuwa inaninunulia tofauti na hapo nilijaribu kupeleka cdt kahama sokoni wateja hamna halafu bei ya chini nikaacha ni zao linalo hitaji maji na mbolea tu mada ni kidogo sana unaweza lima hadi ukaivisha hujapiga dawa yoyote
 
Habarini wana JF.
Naomba kujua soko la zao la beetroot. Mmea huu ingawa hausikiki sana miongoni mwa watanzania, ukijaribu kwenda sokoni unakuta inauzwa ghali kuliko mboga mboga zingine. Nimewaza hivi mtu akiingia shamba akalima kwa wingi vipi soko lake likoje especially kwa Dar? Mimi nipo mkoani lakini nimewaza kama nitalima na nitasafirisha kwa wingi, je soko lake lina uhakika kwa Dar? au kwa export? Naambatanisha picha kwa wale wasioelewa vizuri
Hapa Sokomatola vipo vipo, ila bei ni mlima kama ulivyosema
 
Hapa Sokomatola vipo vipo, ila bei ni mlima kama ulivyosema
mimi nimeshafanya pilot project ya kulima beetroots. Vilikubali ile balaa vilikuwa vikubwa vilistawi balaa. Ila changamoto ya kilimo cha bongo bila soko lililonyooka minasita aisee. Unaweza kutandika ekari nzima ukitarajia mahesabu flani alafu muda wa kuvuna unakuta watu wanajikanyaga kanyaga tuu, unaishia kuuza kwa hasara.
 
Back
Top Bottom