Wakuu naomba kufahamu ni wapi lilipo soko la ulezi na bei ni sh ngapi kwa gunia. Kuna jamaa yangu ana gunia kama 70 hivi kule Singida anahitaji kuuza.
Naomba kuwasilisha.
Wasaga nafaka wanaweza kuwa wateja wazuri wa bidhaa hii, umenikumbusha uji wa ulezi. Ngoja nimuulize mama mmoja ana mashine za kusagisha nafaka, nione anasemaje.