Soko la Tandika Lauzwa

Babuji

Senior Member
Nov 27, 2008
197
3
366.jpg


Wafanyabiashara katika soko la Tandika watabidi watafute makazi mengine baada ya mfanyabiashara ambaye jina lake halikutajwa kuuziwa soko hilo na atatumia shilingi milioni 200 kujenga maduka na kuyapangisha kwa wafanyabiashara atakaowatafuta yeye mwenyewe.

Wafanyabiashara katika soko la Tandika jijini Dar es Salaam, wako katika wakati mgumu baada ya mfanyabiashara mmoja ambaye hakupatikana jina lake wala kampuni yake kulilinunua soko hilo.

Barua iliyotoka Halimashauri ya manispaa ya Temeke, ofisi ya afisa Mtendaji kata ya Tandika iliyoandikwa Februari2,2009. yenye kumbukumbu namba TMK/TNK/127/02/09.ikiwa na kichwa cha habari Kisemacho
YAH. KUMTAMBULISHA MWEKEZAJI M/S TECHNICAL DEVOLEPERS.

Barua hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo kwa uongozi wa soko kuwa tayari mtajwa hapo juu ameshinda zabuni ya kujenga maduka katika soko hilo na atajenga kwa miezi 6 na kutafuta wapangaji kwa miezi 6 na kutokana na kutoa pesa zake itachukua muda wa miaka 8 kabla ya mkataba wake kuisha.

Hata hivyo soko hilo ambalo lilijengwa na Mwalimu Nyerere miaka ya 1974 wakazi wa eneo hilo kwa muda wote huo walikuwa wakinufaika na soko hilo kabla ya kukodishwa kwa mfanyabiashara huyo mwaka huu.

Kutokana na kukodishwa kwa soko hilo jumla ya wafanyabiashara ya maduka 150 na wafanyabiashara ya meza 700 watapoteza nafasi zao kwani mkandarasi huyo amepanga kujenga maduka hayo na kutafuta wapangaji wake mwenyewe.

Wafanyabiashara hao wameapa kuwa hawatakuwa tayari kufukuzwa katika soko hilo ambalo ni mali yao hasa kuzingatia wao pia ni wazawa wa hapa nchini.

Kumekuwana vitisho kutoka kwa viongozi wakuu hasa mkuu wa kituo cha Polisi cha Chang'ombe kwa kuwambia wafanyabiashara hao kuwa kila mmoja atakamatwa na kufunguliwa shitaka lake kinyume na sheria.

Mfanyabiashara mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake akiongea na Nifahamishe alisema "Kumekuwa na uonevu mwingi sana hasa anapotokea mtu mmoja mwenye fedha zake kiasi cha kuhonga viongozi na kutusahau sisi wanyonge ambao tupo wengi ". Mfanyabiashara mwingine alisema

Katika bajeti ya serikali ya mwaka 2009/10, serikali ilianisha sehemu zitakazopewa kipaumbele kuwa nikuboresha sehemu za wafanyabishara ikiwemo soko la Tandika ambalo lilipangiwa kujengwa jengo la ghorofa lenye uwezo wa kutoa nafasi kwa watu 2,000 likiwa limewekewa bajeti ya shilingi 2,500,000.00 sasa iweje huyo tajiri aende kinyume na bajeti sisi wafanyabiasha hatutakubali mtu yeyeto kujenga hapa pasipo maelezo ya kutosha".

369.jpg

Msukuma mkokoteni katika soko hilo akisoma kibao kilichowekwa na wafanyabishara katika soko hilo chenye ujumbe usemao kuwa hili ni eneo la wafanyabiashara sokoni Tandika, eneo hili haliuzwi na haliruhusiwi kujengwa.
 
Last edited by a moderator:
Akili na mawazo yaliyovamiwa na ufisadi huwa ni ya kushangaza sana. Kulikuwa na tatizo gani la kutowashirikisha wadau(wafanyabiashara)wa sasa katika mradi huo?
Kabla ya kutafuta wafanyabiashara wapya, ilitakiwa wafanyabiashara wa awali wapewe tena maeneo yao, kabla ya kuanza kutafuta wafanyabiashara wapya!
 
Iko siku utaamka asubuhi na kukuta kibao nyumbani kwako kwamba wewe na familia yako mmeshauzwa kwa mwekezaji toka India au Indonesia au Pakstani au Arabuni.
Hii ndio nchi yetu wadanganyika. Tukomae au tukubali kuuzwa wima wima.
 
kwikwikwikwikwi tz bwana.....halijaisha la dowanslinaibuka lingine.....kama tumerogwa
 
Iko siku utaamka asubuhi na kukuta kibao nyumbani kwako kwamba wewe na familia yako mmeshauzwa kwa mwekezaji toka India au Indonesia au Pakstani au Arabuni.
Hii ndio nchi yetu wadanganyika. Tukomae au tukubali kuuzwa wima wima.

Kazi kweli kweli!
 
Hivi Mhe. Raisi anajua hili au kama kawaida funika kombe? Na hiyo bajeti waliyoweka ya soko imeenda wapi? Hivi Kikwete yupo kweli na anajali wa-Tanzania?
 
Hivi Mhe. Raisi anajua hili au kama kawaida funika kombe? Na hiyo bajeti waliyoweka ya soko imeenda wapi? Hivi Kikwete yupo kweli na anajali wa-Tanzania?

Lusajo wasalaamu,

Tena haya yanafanyika Dar Es Salaam, sasa wale waliko huko pangu pakavu sijui mambo yakoje? Unajua tulianzia kwenye mbuga kama Loliondo wakaja Waazabe na Mwarabu sasa yamepiga hodi. Kesho, itakuwa Huduma za jamii kupewa mwekezaji.

Naomba kuuliza, diwani wa eneo hilo yuko wapi? mbunge wa eneo hilo yuko wapi? Kama ni mwekezaji kwa nini hawakuwapa kipaumbele wafanyabiashara katika kuliendeleza hilo soko? Wizi mtupu na hasa Ukichukulia hilo soko linazalisha kodi ya kutosha katika manispaa ya Temeke.

Shadow
 
Hivi Mhe. Raisi anajua hili au kama kawaida funika kombe? Na hiyo bajeti waliyoweka ya soko imeenda wapi? Hivi Kikwete yupo kweli na anajali wa-Tanzania?

Afanye Mangapi? Mpk kesi za bata. Kwanini wasishurutishwe waliochini yake wenye kuhusika na hili?
 
Afanye Mangapi? Mpk kesi za bata. Kwanini wasishurutishwe waliochini yake wenye kuhusika na hili?

Nilikuwa nauliza tuu kama anajua? Maana ni wengine aliowateua ndio wanafanya haya. Hao wabunge na madiwani kwa sababu wanachaguliwa na wananchi sina shaka hukumu yao itakuja.
 
366.jpg


Wafanyabiashara katika soko la Tandika watabidi watafute makazi mengine baada ya mfanyabiashara ambaye jina lake halikutajwa kuuziwa soko hilo na atatumia shilingi milioni 200 kujenga maduka na kuyapangisha kwa wafanyabiashara atakaowatafuta yeye mwenyewe.

Wafanyabiashara katika soko la Tandika jijini Dar es Salaam, wako katika wakati mgumu baada ya mfanyabiashara mmoja ambaye hakupatikana jina lake wala kampuni yake kulilinunua soko hilo.

Barua iliyotoka Halimashauri ya manispaa ya Temeke, ofisi ya afisa Mtendaji kata ya Tandika iliyoandikwa Februari2,2009. yenye kumbukumbu namba TMK/TNK/127/02/09.ikiwa na kichwa cha habari Kisemacho
YAH. KUMTAMBULISHA MWEKEZAJI M/S TECHNICAL DEVOLEPERS.

Barua hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo kwa uongozi wa soko kuwa tayari mtajwa hapo juu ameshinda zabuni ya kujenga maduka katika soko hilo na atajenga kwa miezi 6 na kutafuta wapangaji kwa miezi 6 na kutokana na kutoa pesa zake itachukua muda wa miaka 8 kabla ya mkataba wake kuisha.

Hata hivyo soko hilo ambalo lilijengwa na Mwalimu Nyerere miaka ya 1974 wakazi wa eneo hilo kwa muda wote huo walikuwa wakinufaika na soko hilo kabla ya kukodishwa kwa mfanyabiashara huyo mwaka huu.

Kutokana na kukodishwa kwa soko hilo jumla ya wafanyabiashara ya maduka 150 na wafanyabiashara ya meza 700 watapoteza nafasi zao kwani mkandarasi huyo amepanga kujenga maduka hayo na kutafuta wapangaji wake mwenyewe.

Wafanyabiashara hao wameapa kuwa hawatakuwa tayari kufukuzwa katika soko hilo ambalo ni mali yao hasa kuzingatia wao pia ni wazawa wa hapa nchini.

Kumekuwana vitisho kutoka kwa viongozi wakuu hasa mkuu wa kituo cha Polisi cha Chang'ombe kwa kuwambia wafanyabiashara hao kuwa kila mmoja atakamatwa na kufunguliwa shitaka lake kinyume na sheria.

Mfanyabiashara mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake akiongea na Nifahamishe alisema "Kumekuwa na uonevu mwingi sana hasa anapotokea mtu mmoja mwenye fedha zake kiasi cha kuhonga viongozi na kutusahau sisi wanyonge ambao tupo wengi ". Mfanyabiashara mwingine alisema

Katika bajeti ya serikali ya mwaka 2009/10, serikali ilianisha sehemu zitakazopewa kipaumbele kuwa nikuboresha sehemu za wafanyabishara ikiwemo soko la Tandika ambalo lilipangiwa kujengwa jengo la ghorofa lenye uwezo wa kutoa nafasi kwa watu 2,000 likiwa limewekewa bajeti ya shilingi 2,500,000.00 sasa iweje huyo tajiri aende kinyume na bajeti sisi wafanyabiasha hatutakubali mtu yeyeto kujenga hapa pasipo maelezo ya kutosha".

369.jpg

Msukuma mkokoteni katika soko hilo akisoma kibao kilichowekwa na wafanyabishara katika soko hilo chenye ujumbe usemao kuwa hili ni eneo la wafanyabiashara sokoni Tandika, eneo hili haliuzwi na haliruhusiwi kujengwa.

Bado tutashuhudia mengi ya kutukandamiza wanyoge tukiwa ndani ya nchi tuliozaliwa kabla ya sisi wananchi wenywe tukatowa msimamo wa pamoja na kusema basi basi hatukubali tena ukandamizaji huu na unyanyasaji kwa maslahi ya kundi moja (ipitayo sio ndwele ndwele ijayo)
 
........ha ha haaaaaaa, this is real terrible and is when I say our plans do not commensurate with our strategies and thus being a key to our failures. Is true the market might have been in a bad situation and may be they wanted to face-lift it. However, the feasible approach to handle the same in this world of insatiable resources is to involve the public sector through the so called Private Finance Institution 'PFI'. This approach retains the ownership of the asset to the government but seeks financing sources from the private sector. I believe this could have been the right approach to modernise the market while retaining ownership to the government and thus address the socio-economic challenges currently facing.

Essentially, private sectors can and strongly incouraged to participate in similar projects but their involvement should be limited to BOT, BOOT or PPP forms of PFI approach. Giving private sector, to dictate how best to use the facility will always lead to distortion taking into account that the ecomomy is not perfect contestable.
 
Akili na mawazo yaliyovamiwa na ufisadi huwa ni ya kushangaza sana. Kulikuwa na tatizo gani la kutowashirikisha wadau(wafanyabiashara)wa sasa katika mradi huo?
Kabla ya kutafuta wafanyabiashara wapya, ilitakiwa wafanyabiashara wa awali wapewe tena maeneo yao, kabla ya kuanza kutafuta wafanyabiashara wapya!

Idea ya Halmshauri sio mbaya...ni njia mojawapo ya ku-modernise infrastructures kama tukiwa na watu makini........

Kibs you have a good point....Je washika dau walishirikishwa?.....unajua tena mambo ya sense of ownership.....
 
Kama ni kupaweka pawe pa kisasa sioni tatizo hapo.Pale Tandika ndio chimbuko la magonjwa yote ya kuambukiza(kipindupindu na wenzake) bila kusahau hata huduma ya choo kuipata ni kasheshe.Hii ni changamoto tutaendelea kutegemea biashara ya meza mpaka lini?
 
Kama ni kupaweka pawe pa kisasa sioni tatizo hapo.Pale Tandika ndio chimbuko la magonjwa yote ya kuambukiza(kipindupindu na wenzake) bila kusahau hata huduma ya choo kuipata ni kasheshe.Hii ni changamoto tutaendelea kutegemea biashara ya meza mpaka lini?

Mujuni2,

I respectively disagree with you in one point.

Pamoja na nia njema ya kutaka kuboresha hilo soko lakini 'process' yote inawezekana ikawa inatia shaka. Nachelea kuhukumu katika hilo kwani sina mchanganuo wowote kusaupport mawazo yako.

Baada ya kusema hayo, naomba nitumie 'hypothetica case' kwamba: kama huo mchanganuo haukuwawausisha wadau wote wa soko hilo ambao ndio waathirika wakuu wa mabadiliko yoyote basi huo mchanganuo utakuwa haukuendana na sheria na taratibu za uongozi(sheria za utawa bora) hasa katika suala la kushirikishwa( Consultation).


Vile vile suala kama liko katika hali ya 'ujanja ujanja' manake hapo naona ni barua ya Kiongozi wa ngazi ya chini katika manispaa ya Temeke ambaye ametoa hiyo ilani na si Mkurugenzi au kwa niaba ya Mkurugenzi. Swali la kujiuliza, hiyo barua inabaraka za Uongozi wa Manispaa ya Temeke? au ndio mambo ya kuyajaribu maji (testing the water)? Ni Kikako gani cha madiwani kirichoridhia maamuzi ya kumpitisha huyo mwekezezaji kupaendeleza hapo? Je wadau waliopo wametafutiwa maeneo mbadala?

Mwisho huwa na wasiwasi sana na viongozi wa hizi manispaa wawe wa kuchaguliwa au civil servants. Vituko vya Kimbisa na mataa ya barabarani ya bei powa mpaka ukandarasi wa ukusanyaji taka jijini unaonyesha ya kwamba viongozi wetu wa manispaa na majiji yetu wako underserious doubt.

Mh. Rais nakupa pole sana manke waweza kutoboa viatu ukizunguka kuzima mioto kila kona ya Tanzania.

Shadow.
 
Kama ni kupaweka pawe pa kisasa sioni tatizo hapo.Pale Tandika ndio chimbuko la magonjwa yote ya kuambukiza(kipindupindu na wenzake) bila kusahau hata huduma ya choo kuipata ni kasheshe.Hii ni changamoto tutaendelea kutegemea biashara ya meza mpaka lini?
 
mkuu wa wilaya ya temeke anafanya nini? Wafanya biashara hao kwa nini wasichome moto ofisi ya kata? Huyo mtendaji wa kata kwa nini asichapwe bakora?? Ah!! mpaka inachefua, hivi watanzania hatuwezi kufanya chochote mpaka muwape wageni??
Uzembe umetujaa!!
 
Hivi hii nchi bado ni yetu kweli jamani au tumekwishauzwa pia? Hao wafanyabiashara wako hapo toka 1974 ghafla unaamka asubuhi na kuwaambia soko amepewa mwekezaji ajenge then AAMUWE MWENYEWE NANI WA KUMPANGISHA KWA MIAKA 8 huu si zaidi ya uwendawazimu? Kipi kilizuia kuwashirikisha wenye soko ambao kupitia umoja wao I'm sure wangesaidiwa kuandaa proposals then wangepata hizo m 200.Kuna mmoja kamtaka Kikwete in my opinion yuko very right. Familia ikishakosa baba mpaka huko chini nI matatizo matupu. Sasa kama huko juu kuna MIRICHMOND na sasa DOWANS kwanini huko chini madiwani nao wasipige bao? Nyie madiwani mliohusika rais anawajuwa wote msipobadilika atawaumbua kwa boss wenu mkurugenzi nyie?!!? Haya mi simo.
 
Back
Top Bottom