Soko la Mawenzi Morogoro halina maji

Soko la Mawenzi Morogoro halina maji

Hassanjk

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2023
Posts
550
Reaction score
1,020
Wiki iliyopita nilibahatika kufika Soko kubwa kabisa la jumla mjini Morogoro linaitwa Mawezi

Pamoja na soko hilo kuwa na miundombinu ya kizamani (nafikiri ya miaka 80?) kilicho nishangaza kila Butcher ya kitoweo na hadi maliwatoni watu wameweka madumu ya maji hali iliyopelekea nitake kujua kulikoni

Ndio nikaambiwa, maduka yaliyozunguka soko yakiuza kitoweo cha samaki, kuku na nyama nyingine hayana maji kwa miaka kadhaa sasa huku wamiliki hulazimika kuja na maji yao kutokea nyumbani

Kimsingi wamiliki wa Vibanda/maduka wanaona ni kero, kwani wanasema wanatozo nyingi tu wanalipia za kufika zaidi ya laki moja, tofauti na leseni ya kawaida ya Biashara.
 
Barabara zoote zinazoingia sokoni ni mbovu sana upande ule waliko weka kuku hivi sasa. Sehemu ile ya matunda uchafu umekithiri wakati lile ni soko kubwa la jumla.
 
Panatia kinyaa ukienda kipind Cha mvua hutaman kupasogelea
 
Back
Top Bottom