Soko la dunia lipo nchi gani

Hapo sasa mkuu unachanganya, hiyo bei ya hiyo bidhaa fulani uliyosema unadhani inapatikana vipi? Location hapo ni muhimu maana bei inatokana na mizania ya demand and supply. Sasa unavosema soko la dunia ni 'term' bila location sikuelewi kabisa.
 
Je soko la dunia la tanzanite lipo wapi?
 
Soko la mahindi linalojulikana hapa kwetu ni la kibaigwa, lakini ni nini kinachopanga bei ya hilo soko? Ni mahindi yanayopatikana hapo kibaigwa, soko la mahindi la tunduma, la songea na masoko mengine ya mahindi ukilinganisha na idadi ya wateja wanaotaka hayo mahindi ( supply and demand). Kwa hiyo kinadharia soko la kitu fulani la dunia lipo mahali maarufu palipoanza kuuza hiyo bidhaa duniani, lakini bei yake inaathiriwa na upatikana wa hiyo bidhaa kwenye sehemu zingine duniani

Stay home, stay safe
Corona kills
 
Ndo mana nazidi kusisitiza, 'Location' ni kitu muhimu sana unapotamka soko la dunia kwa sababu unaweza kuwa na utofauti wa bei kwa bidhaa moja.

Mfano katika soko la dunia la mafuta kuna standard mbili i) Brent Crude Oil (Ambayo ipo determined na soko la mafuta la ulaya kaskazini) na ii) WTI Crude Oil (Ambayo ni standard ya kupanga bei ya mafuta ya America Kaskazini).

Ipo hivo kwa bidhaa nyingi tu,
 
Je soko la dunia la tanzanite lipo wapi?
Ki utaratibu linapswa kuwa Tanzania ila kwa sababu ya uboya wetu imekuwa siyo.. kipindi cha nyuma naskia lilikuwa nchi moja ya Scandnavia kama sio Uholanzi ambapo wengi wa wamiliki wa Tanzanite walikuwa wakisafiri kuiuza huko maana ndo kulikuwa na wanunuzi
 
Mkuu umemwelekeza vizuri ila akasome economics aache uvivu au agoogle aache uvivu , soko ni physical geographical area pia ni situations ndo maana kuna masoko yapo online kama online stores na other online retailers kama Amazon na Alibaba yote ayo ni masoko, wanaposema soko la dunia wanaamanisha ni soko la bidhaa ambazo upangiwa bei zake na mataifa mbalimbali au umoja wa wazalishaji bidhaa izo , kwa mfano OPEC ambayo ni umoja wa nchi zinazozalisha petroleum upanga bei za petrol , diesel na mazao yote ya crude oil sasa zile bei wanazopangwa huitwa bei ya petrol katika soko la dunia, maana yake ni usawa wa bei ya bidhaa katika nchi zote.
 
Kuna utofauti gan Kat ya jibu lako na maelezo ya mdau hapo juu?
 
The world market is a context. It is not a place, a country or a building.
 
Ndiyo kuna utofauti wa bei sikatai. Lakini kumbuka vile vile bei inaweza kuwa moja. Kulingana na mfano wako bei ya mchele inaweza kuwa sawa pale India na Thailand. Hivyo atakayenunua mcehele India si bado atakuwa ana-refer 'soko la dunia''?
 
Hapo sasa mkuu unachanganya, hiyo bei ya hiyo bidhaa fulani uliyosema unadhani inapatikana vipi? Location hapo ni muhimu maana bei inatokana na mizania ya demand and supply. Sasa unavosema soko la dunia ni 'term' bila location sikuelewi kabisa.
Nina maana bei inaweza kuwa sawa sehemu mbalimbali za dunia hivyo unasema soko la dunia unakuwa unamaanisha sehemu zote ile bidhaa inakopatikana kwa ile bei.
 

Ndiyo utoe majibu sasa mkuu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kupata jibu la swali lako lazima ufahamu soko (market) ni nini.

Soko ni mahali wanapokutana watu kununua na kuuza bidhaa. Hii ni definition rahisi zaidi lakini soko lina mambo mengi ukiacha kubadilishana bidhaa. Ili kuwepo na harmony katika kubadilishana huko bidhaa lazima kuwepo na factors kadhaa ambazo zinawezesha ununuzi na uuzaji huo wa bidhaa nazo ni hizi hapa chini zinaelezwa kwenye hii definition ya market.

A market is one of the many varieties of systems, institutions, procedures, social relations and infrastructures whereby parties engage in exchange.

(Kwamba soko ni muunganiko wa mifumo, taasisi, kanuni, uhusiano wa kijamii na miundombinu inayowezesha watu (nchi) kubadilishana bidhaa) tafsiri sio rasmi sana, kiswahili kigumu.

Hivyo basi soko la dunia ni aggregate (muunganiko) wa masoko yote ya nchi tofauti unaoletwa na mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya nchi hizo.
 
Nitatumia kueleza upate picha kuhusu soko la dunia kwa kuielezea bidhaa maarufu ya dhahabu.Bidha hii ktk soko la dunia(rejea maelezo ya post 35) ambalo wewe mnunuzi au muuzaji ukiwa popote duniani unaweza shiriki kwa njia ya mtandao kwa kutmia platform ambayo broker atakupatia , unaweza analyse kwa kutumia chart bidhaa husika na ukafahamu kwamba inaweza kuwa ktk kupanda au kushuka hivyo ununue au uuze. Kwa kuifutilia dhahabu tangu mwaka jana imekuwa inapanda bei ktk soko la dunia na nimejaribu kuanalyse chart ya miaka mingi sana, naona kuna dalili ya kupanda kufikia record ya 1980 kisha bei itaanza kuporomoka( anlysis ya market sio kitu rahisi, kuna namna nyingi za kuanalyse market ila mimi ni strictly Technical Analyst)
 
Bidhaa tofauti soko tofauti. Majani chai kuna soko kubwa Mombasa
 
Kwa hiyo soko la dunia la nyungu lipo Tanzania au sio, kweli asante serikali ya awamu ya tano kwa kuzalisha nyungu

Au Modds mnasemaje?
 
Soko la dunia la mahindi lipo kibaigwa moro, kama hutaki logout.
 
Mku nimekulewa sana ila mbona kwa sasa dhahabu bei yake imepanda almost $1700 per ounce kwenye soko la dunia lakini kwa wachimbaji wadogo bei imeshuka sababu wansema ni huu ugonjwa CORONA sasa kama mahali inapopatikana kwa wingi bei c ingeshuka kwa kuwa masoko hayo ya dunia hayafikiki hasa Tz as an example
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…