kingadvisor
Senior Member
- Dec 21, 2011
- 109
- 30
Kutokana na vyama vyote kukosa dira inayoeleweka ya kuongoza Taifa.Naomba wale wapenda ujamaa ambao naamini bado wako wengi waanzishe chama cha kijamaa cha Tanzania (socialist party of Tanzania) chenye lengo la kufuata ujamaa kamili na kuweka raslimali zote mikononi mwa umma badala ya mafisadi wachache wa ndani na nje.
Ubepari kwa Tanzania dalili zinaonyesha hauna uwezekano wa kufanikiwa Tanzania zaidi ya kuleta mitafaruku,vita na migongano kati ya wenye nacho na wasio nacho,kati ya wawekezaji na wananchi wazawa n.k Hali hii yaweza ingiza nchi vitani baadaye.Watanzania walio wengi inaonyesha hawajawa tayari kuupokea mfumo wa ubepari bado wanatamani tiba za bure,shule na vyuo vya bure,ajira za umma bwerere kila kona,Migodi na raslimali zingine kuwa chini ya umma badala ya wawekezaji wa nje,n.k
Wengine wanaweza sema ujamaa umeshindwa nchi nyingine ninachoweza sema sio umeshindwa ubepari ndio umeshindwa kwenye nchi hizo.Kwa mfano chukulia Urusi.Wakati wa ujamaa Urusi lilikuwa taifa moja lenye nguvu kubwa duniani ubepari ulipoingia umeshindwa kulifanya liwe taifa liendelee kuwa moja limesambaratika nchi nyingi kibao.Na nchi nyingine vivyo hivyo zilizokuwa za kijamaa.Umoja huu tulio nao ni sababu ujamaa bado upo kwa mbali japo unapumulia kwenye mashine hospitali.
Ni vizuri wawezao kuanzisha chama hicho cha kijamaa waanzishe na kijitambulishe hivyo kabisa na wadhamirie kulirudisha taifa kwenye ujamaa nina hakika watatoa upinzani wa nguvu uchaguzi ujao na wanaweza ingiza wabunge kibao bungeni.
Watanzania walio wengi siyo siri bado wanaota Nyerere na ujamaa wake na hata waliozaliwa baadaye bado wanaota serikali iwasomeshe vyuoni bure,wale bure, walale bure ajira ziwe kibao serikalini.Turudi tu kwenye ujamaa na azimio la Arusha letu tuokoe nchi yetu isisambaratike na kuwa na migongano ya kijamii (class struggle) isiyoisha.
Mimi nitakuwa mmojawapo wa wanachama.Ila sijui taratibu za kuanzisha wanasheria mtusaidie au wajuzi anzisheni sisi tuje tujiunge.
Ubepari kwa Tanzania dalili zinaonyesha hauna uwezekano wa kufanikiwa Tanzania zaidi ya kuleta mitafaruku,vita na migongano kati ya wenye nacho na wasio nacho,kati ya wawekezaji na wananchi wazawa n.k Hali hii yaweza ingiza nchi vitani baadaye.Watanzania walio wengi inaonyesha hawajawa tayari kuupokea mfumo wa ubepari bado wanatamani tiba za bure,shule na vyuo vya bure,ajira za umma bwerere kila kona,Migodi na raslimali zingine kuwa chini ya umma badala ya wawekezaji wa nje,n.k
Wengine wanaweza sema ujamaa umeshindwa nchi nyingine ninachoweza sema sio umeshindwa ubepari ndio umeshindwa kwenye nchi hizo.Kwa mfano chukulia Urusi.Wakati wa ujamaa Urusi lilikuwa taifa moja lenye nguvu kubwa duniani ubepari ulipoingia umeshindwa kulifanya liwe taifa liendelee kuwa moja limesambaratika nchi nyingi kibao.Na nchi nyingine vivyo hivyo zilizokuwa za kijamaa.Umoja huu tulio nao ni sababu ujamaa bado upo kwa mbali japo unapumulia kwenye mashine hospitali.
Ni vizuri wawezao kuanzisha chama hicho cha kijamaa waanzishe na kijitambulishe hivyo kabisa na wadhamirie kulirudisha taifa kwenye ujamaa nina hakika watatoa upinzani wa nguvu uchaguzi ujao na wanaweza ingiza wabunge kibao bungeni.
Watanzania walio wengi siyo siri bado wanaota Nyerere na ujamaa wake na hata waliozaliwa baadaye bado wanaota serikali iwasomeshe vyuoni bure,wale bure, walale bure ajira ziwe kibao serikalini.Turudi tu kwenye ujamaa na azimio la Arusha letu tuokoe nchi yetu isisambaratike na kuwa na migongano ya kijamii (class struggle) isiyoisha.
Mimi nitakuwa mmojawapo wa wanachama.Ila sijui taratibu za kuanzisha wanasheria mtusaidie au wajuzi anzisheni sisi tuje tujiunge.