Slaa: Jakaya Kikwete ana mkono EPA

Slaa: Jakaya Kikwete ana mkono EPA

Dr Slaa anateswa na mzimu wa kupora wake za watu. ndo maana kutwa kucha yeye kazi ya kuwasema wanaume wenzake tu
Hakuna mahusiano kabisa na ukweli wa kwamba washirika wa Kikwete kwenye kupora fedha za BOT-EPA wana enjoy maisha wayatakayo, bila soni nenda magerezani soma ripoti ya jaji Kisanga na Manento wafungwa na watuhumiwa wanavyokaa magerezani bila hata kesi zao kusomwa na wale wenye kesi za kuku wanavyofungwa vifungo virefu
 
Mkuu, huyu DR naona anazeeka vibaya. ukichanganya na hivyo virobaa na gongo anayokunywa ndo kabisaaaaa!

Kam viroba na gongo vinamsaidia kwa kiasi anavyotetea maslahi ya nchi basi na aendelee kunywa sasa walevi wa rushwa wenye kuhongwa suti na kuuza nchi, ndio unaona wanastahili
 
[h=1]Slaa: JK ana mkono EPA[/h]
  • Adai mfungwa aliyeachiwa kwa msamaha wake alikodi ndege za kampeni za urais CCM

28/01/2014 | Posted by Mwandishi Wetu | Kitaifatangulizi | 0 comments | 593 views

SIKU chache baada ya Jeshi la Magereza nchini kukiri mfanyabiashara, Ajay Somai, aliyetupwa jela miaka miwili kwa

kosa la kukwapua sh bilioni 3.8 kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), amepata

msamaha wa Rais Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod

Slaa, amesema kuwa Rais Kikwete ana mkono na EPA.


Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana katika mikutano ya hadhara iliyofanyika kwa nyakati tofauti katika eneo la Ifunda, Kijiji

cha Mawambala katika Jimbo la Kilolo na Iringa Mjini, ikiwa ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya Operesheni

inayoendelea nchi nzima, iliyopewa jina la ‘M4C- Operesheni Pamoja Daima’.


Huku akisikilizwa kwa makini na maelfu ya wananchi wa maeneo hayo, Dk. Slaa alisema ni jambo la kushangaza kwa

rais kuwaacha watuhumiwa wadogo kama wale wa wizi wa kuku, lakini ameamua kutoa msamaha kwa wezi wakubwa

wa fedha za EPA.



“Hii ni kashfa kwa Rais Kikwete, haiwezekani ukatoa msamaha kwa wezi wakubwa walioiba mabilioni ya fedha halafu

ukawaacha watuhumiwa wa makosa madogo, tena wengine wa kubambikiwa kesi na polisi wakiendelea kusota

gerezani. Hapa lazima kuna mkono wa Kikwete,” alisema Dk. Slaa.


Dk. Slaa ambaye amepata kuwa mgombea urais wa CHADEMA, alisema kuwa mfungwa huyo wa EPA ambaye yuko nje

kwa msamaha wa rais wakati wa kampeni za mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alikodi ndege kwa ajili

ya kampeni za mgombea huyo.


Mbali ya Somai, wezi wengine wa EPA waliopata msamaha huo ni wafungwa namba 24/2011, Farijala Shabani

anayetumikia kifungo cha miaka 11 na mfungwa namba 345/2011, Rajabu Maranda anayetumikia kifungo cha miaka

kumi, ambao nao wamenufaika na msamaha huo wa rais uliotolewa Desemba 9, mwaka jana.


Kwa mujibu wa Dk. Slaa, CHADEMA ikiingia madarakani wezi hao watakamatwa na kurudishwa gerezani na zaidi ya

yote, watalipa fedha walizoziiba.


Mbali na suala la kuachiwa kwa wafungwa wa EPA, Dk. Slaa alisema deni la taifa limezidi kuongezeka ambapo hadi sasa

kila Mtanzania hata yule anayezaliwa leo, ana deni la sh 500,000.


Mbowe azidi kulia na Katiba mpya



Wakati Dk. Slaa akirusha kombora kwa Rais Kikwete, Mwenyekiti wake wa taifa, Freeman Mbowe, amesema kuwa

Katiba Mpya na bora ni ile itakayopata uhalali kutokana na mchakato wake kuhusisha maoni ya watu badala ya

masilahi ya chama tawala.


Alisema Katiba ya aina hii ndiyo itasaidia taifa kuponya majeraha na kuondoa makovu ambayo wananchi wameumizwa

kwa muda mrefu.



Alisema CHADEMA haitawaangusha Watanzania katika kupigania na kusimamia masuala ya msingi likiwemo suala la

Katiba Mpya, huku akiwataka waiunge mkono wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.



Mbowe alisema CHADEMA inatambua umuhimu wa Katiba mpya kwa mustakabali wa Watanzania na jinsi wananchi

walivyo na matumaini makubwa kuwa itasaidia kuweka mazingira ya fursa za maendeleo kwa mtu, makundi katika jamii

na taifa zima kwa jumla, hivyo watasimama kidete kwa niaba ya Watanzania.


Alisema hayo jana alipokuwa akihutubia mikutano ya hadhara maeneo ya Muleba, Biharamulo, Chato, Nyang’hwale na

Geita, ikiwa ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya operesheni inayoendelea nchi nzima, ikiwa imepewa jina la

‘M4C-Operesheni Pamoja Daima’.


Mbowe ambaye aliingia rasmi kwenye operesheni hiyo tangu Jumamosi wilayani Ngara, alisema kuwa chama chake kwa

kuunganisha nguvu za pamoja kwa kushirikiana na kila Mtanzania, makundi mbalimbali katika jamii na vyama vingine

vya siasa vilivyo tayari kusimamia mchakato wa Katiba kwa niaba ya Watanzania, kitahakikisha uhai wa Tanzania

unapewa kipaumbele kabla ya masilahi ya vyama vya siasa.



“Ndugu zangu wananchi wa Biharamulo juzi nikiwa Ngara nimezungumzia masuala ya Katiba na daftari la wapiga kura,

leo pia sina jinsi, nawiwa kuzungumzia suala hili nyeti la Katiba kwenu. Nimesema na nitarudia kusema tena na tena na

tena, kwamba suala la Katiba ni uhai wa taifa.



“Kutokana na ukweli huo, kwetu sisi CHADEMA na watu wengine wenye mapenzi mema na nchi yetu vikiwemo vyama

vya siasa vilivyo tayari kushirikiana kwa ajili ya jambo hili kubwa linalozidi tofauti zetu zote tunazoweza kuwanazo,

tunalichukulia kuwa ni suala la Katiba mpya iliyo bora na inayozingatia matakwa ya Watanzania, ni suala la kufa na

kupona.


“Kuna vyama vya siasa vinafikiri katiba zao zinaweza kuwa kubwa kuliko Katiba ya nchi. Tunawataka wafikirie mara

mbili sana. Katiba za vyama ni kwa ajili ya vyama hivyo lakini Katiba ya nchi ni kwa ajili ya Watanzania wote nchi

nzima. Kuchezea maoni ya watu kwa ajili ya kulinda masilahi ya chama fulani cha siasa ni dharau inayovuka mipaka ya

kiburi cha utawala,” alisema Mbowe na kuongeza:


“Tunataka Katiba mpya hii iende kuponya majeraha na kuondoa makovu ya muda mrefu yaliyoko ndani ya jamii yetu ya

Watanzania…wote tumeumizwa kwa namna moja ama nyingine, majeraha na makovu hayo yanaweza kupunguzwa au

kumalizwa kabisa na Katiba mpya na bora itakayopata uhalali kutoka kwenu.”
 
Naona siku hizi JF sio kujenga hoja ni matusi na dharau.........jadilini ni vp Mwizi wa bilioni kadhaa anaachiwa huru ndani ya miezi sita sio kumsimanga Slaa,mara kibabu mara Sijui gongo imefanya nini.........tuna shida nyingi watz kwanini mtu apore fedha zetu halafu mshabikie kuachiwa kwake huru bila maelezo ya msingi.......tuamkeni watz tusiwe tunatetea vitu visivyo na msingi huku jamii yetu ikiangamia kwa ukosefu wa elimu bora na matibabu bora ya afya......
 
Hivi slaa anaweza kumnyoshea kidole mtu kwa lolote sibora akae kimya tu kwanza aone aibu kama aliweza kukosea kanisania tena dhambi kubwa kiasi hicho atashindwa nini kuwatendea dhambi binadamu.
 
Mkuu, huyu DR naona anazeeka vibaya. ukichanganya na hivyo virobaa na gongo anayokunywa ndo kabisaaaaa!
Kabisa kabisa mkuu kwa sasa hajielewi kabisa niwakuhurumiwa sana au kumpeleka kwenye maombi.
 
We muuza maji div 5, unaushahidi? Halafu we kazi huna kwa uduni wako wa elimu halafu unamchukia kikwete!

wewe una ujinga wa kuzaliwa maana sioni sababu ya kumtetea muovu.

Mbwa hata ukiibeba mgongoni lazima atatoa ulimi nje.

Kikwete ni MZIGO NO.1
 
Mkuu, Mbona DR SLAA na MBOWE wanatafuna sana fedha za walipa kodi na bado mnawashangilia? pia DR SLAA anapora wake za watu na bado mnampigia makofi. huo si ufisadi?

You will soon be on my "ignore" list. Nimechoka kusoma utumbo wako unaochangia hapa.

Tiba
 
lb7 wanywa gongo inayopikwa kwa madaso yaliyovunda maana wanashabikia pumba tu
 
enyi vijana was buku7 hebu acheni kujtoa ufahamu... simameni kwenye mantiki ya mada
 
Kweli kibabu ni kimechanganyikiwa! Hivi unadai utawakamata watu waliosamehewa magereza na kuwafunga tena! Acha uongo na kutafuta cheap popularity! We utawarudisha kwa sheria ipi? Unajua maana ya Autrofois aquit na autrofois convict? Mbona kizee kinakuwa kiongo namna hii! Na Jk anapotangaza msamaha,kuna kamati na parole body ambayo ndio inachambua kwa ngazi ya wilaya hadi kata kulingana na matatizo aliyonayo mfungwa, hapo Jk anahusikaje? Jamani ndio maana upadri umekushinda we mzee kwa uongo!

Kwani hayo majina hadi yanapelekwa kwa jk unadhani hakuwa na taarifa? Unadhani jina la babu seya lingekuwepo angepitisha? Majina lazima yahakikiwe, tiss wanafahamu na wanamjulisha jk.
 
Hivi slaa anaweza kumnyoshea kidole mtu kwa lolote sibora akae kimya tu kwanza aone aibu kama aliweza kukosea kanisania tena dhambi kubwa kiasi hicho atashindwa nini kuwatendea dhambi binadamu.
Ulikuwa nae siku hiyo au ......:........ Sema tujue wazi.
 
slaa mwenyewe ni mzee wa vimwana esp wake za watu. huo ni ufisadi mbaya kabisa huo
 
mbona forum hii imekuwa ya kitoto hivi?mada mezani ni rais kuwasamee wa epa,sasa hayo ya slaa mara mbowe,mara sijui gongo, ya nini sasa.
hizi simu za january makamba zinaiaribu forum.kwa nini jk ametoa msamaha kwa wezi wa pesa za umma? ina maana hakuna wafungwa ambao walisyahili masamaa huo? hapo kuna kitu bana.
 
Back
Top Bottom