Siku ile aliyotoa hotuba Dr. Nchimbi kwamba Watanzania wapiganie Katiba mpya, sikumwelewa vizuri, lakini kwa sasa nadhani nimemwelewa kwa kwa asilimia kubwa.
Mambo makuu matatu aliyoyasema ambayo yamenifanya nimwelewe ni kama vile:-
1. Mmemwalika mtu anayefanana fanana na kazi yenu(kutetea haki za binadamu)
2. Mwenye mamlaka ya mwisho kuleta katiba ni Rais pekee yake.
3. Mnataka niwasmbie nini ili mnielewe?
Kutokana na kauli hizo, mimi nadhani alimaanisha kwamba:-
1. Bila kujitoa sadaka kupambania Katiba mpya, hakuna Rais atakayekuja kutoa Katiba mpya kwa hiari. Ndo maana alisema, Katiba hii inampa Rais madaraka makubwa mno.
2. Watanzania wote kwa Umoja wao, kwenye suala linalohusu Katiba wajitahidi kuweka mbali tofauti zao za kiitikadi na waungane pamoja kupigania Katiba mpya. Hapo alisema, tupate Katiba ambayo itamlinda mtu yeyote na wa itikadi yoyote ile, yaani awe CHADEMA, CCM, CUF, Mkristo, Mwislam, Mpagani nk.
Kwa hiyo, mimi nadhani imebaki kazi kwetu kuungana pamoja watu wa vyama vyote, Taasisi zote, makabila yote, kanda zote, rika zote, jinsi zote kupambana kufa au kupona kuwakumbusha watawala kuhusu upatikanaji wa Katiba mpya.
Mungu atuamshe, atuondolee ujinga na woga na atupe ujasiri usio kifani kupigania Katiba mpya.
Mambo makuu matatu aliyoyasema ambayo yamenifanya nimwelewe ni kama vile:-
1. Mmemwalika mtu anayefanana fanana na kazi yenu(kutetea haki za binadamu)
2. Mwenye mamlaka ya mwisho kuleta katiba ni Rais pekee yake.
3. Mnataka niwasmbie nini ili mnielewe?
Kutokana na kauli hizo, mimi nadhani alimaanisha kwamba:-
1. Bila kujitoa sadaka kupambania Katiba mpya, hakuna Rais atakayekuja kutoa Katiba mpya kwa hiari. Ndo maana alisema, Katiba hii inampa Rais madaraka makubwa mno.
2. Watanzania wote kwa Umoja wao, kwenye suala linalohusu Katiba wajitahidi kuweka mbali tofauti zao za kiitikadi na waungane pamoja kupigania Katiba mpya. Hapo alisema, tupate Katiba ambayo itamlinda mtu yeyote na wa itikadi yoyote ile, yaani awe CHADEMA, CCM, CUF, Mkristo, Mwislam, Mpagani nk.
Kwa hiyo, mimi nadhani imebaki kazi kwetu kuungana pamoja watu wa vyama vyote, Taasisi zote, makabila yote, kanda zote, rika zote, jinsi zote kupambana kufa au kupona kuwakumbusha watawala kuhusu upatikanaji wa Katiba mpya.
Mungu atuamshe, atuondolee ujinga na woga na atupe ujasiri usio kifani kupigania Katiba mpya.