William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,464
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbrod Slaa amemshangaa Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana kwa kuanza kulalamika kuhusu bei za Korosho, Ufisadi wakati Chama chake ndicho chenye serikali. Dr Slaa anasema ni bora CCM ikawa upinzani na yenyewe badala ya kuwahadaa wananchi.
Aidha amewashangaa watu wanaodai majina ya mafisadi wakati yeye alishawasilisha kwa DPP majina na akaunti za Mafisadi na watia sahihi wa akaunti hizo lakini serikali imekaa kimya hadi leo.
Slaa pia amewashangaa watu wanaodai CHADEMA ina makundi kwani huo ni uzushi usio na maana na CHADEMA haina muda huo wa kupoteza. Kazi ni moja tu ya kujenga Chama na wakati uchaguzi wa ndani ya Chama ukiwa unaendelea rushwa haitavumilika ndani ya CHADEMA hata kidogo.
Slaa ameyasema hayo katika Baraza la Mashauriano la Mkoa wa Kagera ambalo pia lilihudhuriwa na Wenyeviti na Makatibu wote wa Mikoa wa CHADEMA.
- HUYU mzeee naye anazeeeka vibaya sana dhambi ya mke wa mtu inaanza kumtafuna sasa hajielewi kabisa, anaacha kujishangaa mwenyewe kujilipa hela za wananchi walipa kodi Shillingi Millioni 12 kwa mwezi ambazo wala hazina risiti anajipa tu, leo anamshangaa Kiongozi wa Chama Tawala tena Mkubwa kuliko yeye na aliyechaguliwa na wanachama wote wa CCM, wakati yeye amechaguliwa na Mtei tu, halafu ndio mnasema huyu afanye mdahalo na Kinana, yaani aibu tupu!!
Le Mutuz!!