Skrill online payments. Msaada tutani

Skrill online payments. Msaada tutani

Godee jr

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2012
Posts
1,906
Reaction score
2,699
Habari wakuu. Natarajia kupokea pesa toka nje ya nchi na moja ya njia ambazo mteja Wangu anatumia kulipa ni Skrill na pay pall.
Nimeshafungua account ya Skrill ila naomba kupata uzoefu ni jinsi gani nitaweza kuamisha pesa toka Skrill kuzileta kwenye account yangu ya bank.
Na je itachukua muda gani kumalizika hiyo transaction nikimaanisha tangu kutumwa kwa pesa hadi kumalizika kwa taratibu za kuamishia pesa kwenye bank account yangu na Mimi kuweza kuitumia.
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu wakuu

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Nimeshafungua account ya Skrill ila naomba kupata uzoefu ni jinsi gani nitaweza kuamisha pesa toka Skrill kuzileta kwenye account yangu ya bank.
Kwa kuwa tayari umefungua account ya skrill, kinachofuata ni ku_Link
(a) Card yako ya benki ambayo tayari iko activated kufanya miamala mtandaoni au
(b) Account number ya benk husika - Inatakiwa uwe unafahamu SwiftCode ya hiyo benki unayotumia

upload_2017-7-16_20-0-42.png


Baada ya kuwa fedha imeingia, Click withdraw ambapo utakuwa na option mbili za kutoa fedha

upload_2017-7-16_20-1-44.png

Na je itachukua muda gani kumalizika hiyo transaction nikimaanisha tangu kutumwa kwa pesa hadi kumalizika kwa taratibu za kuamishia pesa kwenye bank account yangu na Mimi kuweza kuitumia.

1. Kutoa kupita account number yako
- Fedha huchukua kati ya siku 2 - 5,
- makato ni USD 6.31 bila kujali kiasi chafedha unachotoa.

2. Iwapo utatoa kupitia Card yako
- Huchukua zaidi ya siku 6
- Makato ni asilimia 7.5 ya kiasi cha fedha utakachotoa

NB:- Njia ya haraka zaidi ni kutumia MPESA KENYA ambapo fedha unaipata within 30seconds kutoka account yako ya skrill kwenda namba ya mpesa kenya.

Kwa bahati mbaya hii huduma ya Skrill vs MPESA TZ, au mtandao mwingine wa simu, haipo kwa sasa.
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu wakuu

KARIBU
 
Halafu utazipataje toka huko mpesa Kenya

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Kwa kuwa tayari umefungua account ya skrill, kinachofuata ni ku_Link
(a) Card yako ya benki ambayo tayari iko activated kufanya miamala mtandaoni au
(b) Account number ya benk husika - Inatakiwa uwe unafahamu SwiftCode ya hiyo benki unayotumia

View attachment 543772

Baada ya kuwa fedha imeingia, Click withdraw ambapo utakuwa na option mbili za kutoa fedha

View attachment 543776


1. Kutoa kupita account number yako
- Fedha huchukua kati ya siku 2 - 5,
- makato ni USD 6.31 bila kujali kiasi chafedha unachotoa.

2. Iwapo utatoa kupitia Card yako
- Huchukua zaidi ya siku 6
- Makato ni asilimia 7.5 ya kiasi cha fedha utakachotoa

NB:- Njia ya haraka zaidi ni kutumia MPESA KENYA ambapo fedha unaipata within 30seconds kutoka account yako ya skrill kwenda namba ya mpesa kenya.

Kwa bahati mbaya hii huduma ya Skrill vs MPESA TZ, au mtandao mwingine wa simu, haipo kwa sasa.


KARIBU
Nashukuru sana kwa ufafanuzi wako mkuu

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Halafu utazipataje toka huko mpesa Kenya

Post sent using JamiiForums mobile app
Hiyo no rahisi sana kama upo maeneo ya mpakani

Post sent using JamiiForums mobile app
Unaweza kumtumia ndugu/ jamaa / rafiki ambaye ana laini ya kenya.

Unahamisha fedha toka account yako ya skrill kwenda namba yake.

Naye anahamisha toka namba yake (mpesa kenya) kuja Namba yako ya MPESA Tanzania.
 
Unaweza kumtumia ndugu/ jamaa / rafiki ambaye ana laini ya kenya.

Unahamisha fedha toka account yako ya skrill kwenda namba yake.

Naye anahamisha toka namba yake (mpesa kenya) kuja Namba yako ya MPESA Tanzania.

natoaje pesa kutoka Skrill kwenda Mpesa Kenya?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom