hivi watoto wa leo bado wanasoma hii hadithi maana kuna mtoto wa ndugu yangu nilimwambia anipigie hadithi za shuleni kwao akaanza hadithi hadithi,nikasema hadith njoo,akaendelea,hapo zamani za kale palitokea padre na shehe walikua wanasafiri ktk basi moja walipofika sehemu ya chakula padre akaagiza kitimoto akamkaribisha shehe,shehe akasema sisi hatutumii hio,padre akamwambia kweli hujui utamu unaoukosa.Mtoto akaendelea kunihadithia eti,walipomaliza kula basi likaendelea na safari na walipofika mwisho wa safari wakaagana kisha shehe akamwambia padre,haya bwana msalimie mkeo,padre akajibu sisi hatuoi,shehe akamwambia kweli hamjui utamu mnaoukosa.
Kisha mtoto akaniuliza,hadithi hii inatufundisha nini,nikamwambia inatufundisha kuwa tanzania ni nchi ambayo waislam na wakristo wake wanapendana.Akacheka akasema umekosea,nikwambie jibu ,ikabidi nimtume kwa kuhofia jibu ambalo angeweza kunipatia.