Ibada ya kwanza
JF-Expert Member
- Mar 21, 2013
- 3,282
- 1,810
Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.
Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".
Sasa kama wanajua sili nyingi mbona hawakutoka paka walipotimliwa?hao wasaliti hawafiki popote?