Chadema kama taasisi imepata jeraha kubwa. Jeraha hili linahitaji tiba madhubuti ili lisikigharimu chama. Maana viongozi waliopo ACT wanajua siri zote za chadema. Walikuwa wanashiriki vikao vya ndani kabisa vya chama. Ni sawa na kuachana na mke/mume. Hakuna wa kujivuna. Bali akili lazima itulie ili kuendelea na maisha mapya. Na usipo kaa vema utaishia kunywa pombe au kufanya ukahaba kwa kuchanganyikiwa.
Na ndiyo maana kwa mnaofuatilia kinachoendelea ukumbi wa Diamond Jubilee. Kuna mwanadada muigizaji alipotupa dogo linaloilenga chadema ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe. Nitanikuu "kumpiga chura teke ni kumpunguzia safari".
kwa ujumla wewe hujafanya tafakuri vizuri ujiulize hapa nani kaumbuka,
chadema waliwasimamisha na hatimae kuwafukuza uanachama viongozi wao watatu ambao ni kitila mkumbo proffesa na mkufunzi wa chuo kikuu cha daresalaam,samson mwigamba aliyekuwa kiongozi wa chama hicho mkoani arusha na aliyekuwa naibu katibu mkuu cdm taifa kwa tuhuma za kuunda mtandao wa usaliti ndani ya chadema.
nyaraka na ushahidi wa wazi uliwekwa hadharani na wawili kati ya hao walikiri isipokuwa aliyekuwa katibu mkuu naibu ndugu ZZk,hatimae waliokiri kufukuzwa ndani ya chama kwa usaliti huku zzk yeye akikimbilia mahakamanikuzuia chama kisimjadili uanachama wake.jambo ambalo lilimfanya kuwa mbunge wa mahakama.hadi hukumu ya shauri lake ilipotolewa wiki chache zilizopita.jambo lililopelekea zzk kutangaza rasmi kuachia ubunge wake ikiwa ni baada ya kauli ya mwanasheria wa cdm Tundu lissu kutoa tamko la chama kwamba zzk alikwisha jifukuzisha chamani tangu alipokiuka katiba ya cdm,kwa kukishitaki chama mahakamani.
wakati wote hayo yakijili kwa upande wa zzk,huku kina mwigamba,kitila na nyakarungu wakajiunga na chama kilichokuwa kikisubiri usajili cha ACT.lakini muda mfupi nako kukatifuka kwa kile kilichotajwa na aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho bwana limbu kama ni kuvamiwa na kuporwa madaraka na kina mkumbo jambo lililowapeleka mahakamani na kuamriwa kinyemela kwa sintofahamu na msajili wa vyama nchini,jambo ambalo bwana kadawi limbu analilaamikia hadi sasa na akiwa na shauri mahakamani.
mojawapo ya madai yake akiongea na vyombo vya habari na kunukuriwa na vyombo kadhaa vya habari nchini ni pamoja na akaunti ya ACT kuingiziwa fedha na vyanzo asivyovifahamu ikiwamo pamoja na vifaa kama magari nk.
imemchukua zzk siku nne tu kuteuliwa kuwa kiongozi mkuu wa ACT,cheo ambacho ni kipya katika medani ya siasa nchini mwetu.madaraka ya kiuongozi yaliyoainishwa kwa kiongozi mkuu ni pamoja na kushauri chama,msemaji mkuu wa chama na pia mteuzi wa moja kwa moja wa nyadhifa mbalimbali za kiuongozi ndani ya chama chake.
tafakuri
kama chadema walikuwa waongo ni kwa vp haya yametokea?
tena amemteua mama kwa kisingizio cha kuwaenzi kina mama,wakati kiuhalisia amemuweka pale kutomuweka mtu anayeweza kumletea pingamizi kwenye baadhi ya maamuzi na au anayeweza kukaa kimya pale atakapoona baadhi ya mienendo isiyokubalika ndani ya chama chake.
ile janja ya kutaja mali anazodai kuziweka na madeni tunahitaji kuliona na lile la fedha za nssf alizowaamuru kuilipa kampuni ya lekadutigite anayoimiliki pamoja na magari aliyopewa na nimrod mkono,pia atutajie zile alizowekewa na TISS kwenye akaunti za nje kama alivyowahi kutuhumiwa na cdm.
kwa hiyo hapa amewasaidia cdm kwenye macho ya jamii kuzielewa mbichi na mbivu kwa usaliti wake:juggle:
pia tunashangaa kitila mkumbo kuendelea kuhama na kuvuruga vyama vya upinzani huku akiwa ni mtumishi wa serikali bila serikali kuchukua hatua zozote,wakati watu kama kina baregu yaliwafanya wapoteze ajira zao toka vyuo hivyo hivyo vya serikali