Siyo kila mchezaji mkubwa anaweza kuwa kocha mwenye mafanikio

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,136
7,904
Mara kadhaa niliwahi kuahidi kuleta uzi unaohusiana na mada hii, leo nimetulia kidogo nimeukumbuka. Ngoja nitiririke.

Kuna hii kasumba iliyojengeka kwenye mpira kudhani kuwa mchezaji yoyote hasa akitokea kupata mafanikio fulani kama mchezaji anaweza kuja kuwa kocha mzuri pale atakapostaafu. Mimi binafsi naamini IQ ya mchezaji ndiyo itakayoamua kama mchezaji atakuja kuwa kocha mzuri. Mchezaji anaweza kuwa alikuwa anafunga sanaa enzi za uchezaji wake kama kina Ole Gunar Solskjaer na bado asiweze kuja kuwa kocha mzuri. Ukocha siyo kama ukuu wa wilaya kwamba unaweza mwenyewe kuficha au mamlaka zinaweza kukubeba na kuficha madhaifu yako siku zikasonga.

Huko nje mifano ipo mingi sana ya wachezaji ambao enzi za uchezaji wao walikuwa mahiri sana ila walipoenda kwenye ukocha ilikuwa ni majanga matupu. Alan Shearer ambaye bado anashikilia rekodi za ufungaji bora huko Uingereza ila alipewa timu aifundishe ikashuka daraja.

Sir Bobby Charlton anayeaminika ni mchezaji bora wa muda wote kutokea pale Uingereza, huyu naye alipewa timu akaishusha daraja. Thiery Henry ana mafaniko mengi sana ya binafsi kama mchezaji na alizoipatia klabu zake na timu yake ya taifa na baada ya kustaafu alipewa mikoba ya ukocha katika timu ya AS Monaco, ila baada ya miezi 3 akafukuzwa baada ya kuitumikia kwa mechi 20 tu huku 11 akiwa amepoteza.

Kuna Tony Adams, mmoja wa wachezaji wanaoheshimika mno huko Uingereza hadi wamemjengea sanamu yake pale nje ya uwanja wa Arsenal wa Emirates ambayo aliitumikia kwa miaka 22 kama mchezaji. Huyu baada ya kustaafu, timu mbili alizofundisha amezishusha daraja.

Kuna Paul Gascoigne "Gaza" na Stoichkov. Kuna Paul Scholes na mwenzake Gary Neville, wote wawili zao la Alex Ferguson pale Man United lakini wote walishindwa vibaya sana katika ukocha. Kuna Lothar Matthaus, legend wa Ujerumani ambaye timu yake ya Celta Vigo ilishuka daraja ikiwa katika mikono yake ya ukocha. Hapo sijamtaja Diego Maradona, legend mwingine wa soka ila zama zake kama kocha zilikuwa ni za visanga tu.

Tanzania tumeshuhudia wachezaji kadhaa wa zamani waliowahi kuchezea timu kubwa mfano za Simba na Yanga ambao walikuja kuwa makocha. Mifano inayonijia haraka ni Fred Felix "Minziro" huyu amefundisha kwa muda mrefu sana ila hana rekodi yoyote ya kujivunia. Kuna Mohamed Hussein "Mmachinga" mchezaji ambaye kama liivyo kwa Alan Shearer bado anashikilia rekodi katika ufungaji bora katika ligi kuu ila mpaka leo hana mafanikio yoyote katika ukocha. Sina uhakika kama Mmachinga ameshawahi kufundisha ligi kuu ila mara ya mwisho nimemuona anafundisha kwenye bonanza kwenye kombe ya Ramadhani.

Kuna Jamhuri Kihwelo, naye baada ya kufundisha kwa muda mrefu hana lolote la kujivunia katika ukocha pamoja na kwamba enzi zake za uchezaji alipewa sifa kedekede. Kuna Joseph Lazaro na Juma Mgunda ambao naona kama bado wanajitafuta. Selemani Matola amekuwa chini ya miamvuli ya makocha wengine, hatujamuona akiongoza timu kama kocha mkuu kwa hiyo bado hatuwezi kumuhukumu.

Wachezaji pekee wa ndani ambao naweza kusema waliweza kupata mafanikio kama makocha ni Abdallah Kibadeni na labda Charles Boniface "Mkwasa". Huyu Mkwasa namtaja ila inabidi nirudi kuhakiki rekodi zake maana najua amefundisha sana Yanga na timu ya taifa ila sina uhakika kama kuna mafanikio yoyote yaliyopatikana chini ya mikono yake.

Ili mchezaji aweze kuwa kocha mzuri inabidi awe na IQ kubwa ya kimpira yeye kama mchezaji kwanza. Kupima IQ ya kimpira inabidi uwe na jicho la kuangalia mchezaji anavyocheza uwanjani. Naangalia uwezo wa kucheza position zaidi ya moja uwanjani, uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na ya haraka akiwa na mpira, anavyojiposition anapokuwa hana mpira, uwezo wa kuusoma mchezo na kuiendesha timu uwanjani.

Nikitumia sampo zilizoko katika vikosi vya Simba na Yanga msimu huu, wachezaji ambao kwa haraka haraka wananijia kichwani kuwa kwa mtazamo wangu wanaweza kuwa sifa hizo na hivyo wanaweza kuja kuwa makocha wazuri ni pamoja na Djigui Diarra, Khalid Aucho, Che Malone, Moses Phiri, Max Nzengeli, Aziz Ki, Dickson Job, Fabrice Ngoma, Luis Miquisonne, Clatous Chama na ziada naweza kuwaongeza Shomari Kapombe na Feisal Salum (Azam). Kwa sababu ligi ya NBC sasa hivi inajumuisha wachezaji kutoka nje, nimeona mifano yangu iwajumuishe pia.

Uzi huu umejikita zaidi kuangalia wachezaji wakubwa ambao walifeli kuwa makocha. Kwa wachezaji wa nje kuna ambao walikuja kufanikiwa sana kama makocha mfano Diego Simeone, Zidane, Cruyff, Guardiola, Ancelotti, del Bosque, Antonio Conte, Beckenbauer na Mancini.

Kwa Tanzania, wachezaji wa zamani ambao kwa sifa ambazo nimesikia walikuwa nazo kwa mtazamo wangu naona kama wangeweza kuwa makocha wazuri ni Edibily Lunyamila, Salvatory Edward, Hussein Marsha, Kenny Mkapa, Hamis Gaga "Gagarino", Malota Soma, Method Mogella, Yusuph Macho na Athumani China. Sina uhakika katika hawa kuna ambaye alishajaribu ukocha ila inawezekana nao wangeishia kuwa na mafanikio kama ya Jaluo na Minziro.
 
Yaani kama kuna kocha wa ajabu huku duniani ni Zenedin Zidane zizou. Huyu jamaa ukimwangalia unaweza kudhani ni bonge la kocha.

Kumbe alibebwa na ile b.b.c. Tangu aanze ukocha kafundisha real Madrid pekeakea. Kila timu wakimwaproach anakataa. Anajua kabisa bila bbc hawezi kupata chochote.

Gerald, Lampard, Ole Guna, Di Mateo, zola nk hapa hakuna makocha.

Mwisho Uingereza haina au ina uhaba wa makocha. Vilabu vyote vikubwa vinavyocheza ligi kuu ya epl tangu mwanzo wa miaka ya 1990 mpaka napoandika hii post hawana kocha aliyebeba kombe. Wote ni wageni. Wenyewe ni kelele tu kama vyura.
 
Minziro mtoe hapo.

Ni kocha mzuri ila mazingira yetu ya Simba na Yanga yanamficha.

Laiti angeenda hata Azam halafu apewe uhuru wa kufanya Kazi yake,naamini tungeona kitu cha tofauti
 
Hongera mkuu.

Andiko lako la kiufundi sana.
Lakini kwa Tanzania sifa nyingi kwa Abdallah Kibadeni "King"

Huyu mwamba amepata mafanikio mengi sana akiwa na Simba sport kuliko makocha wote waliofanya kazi na vikabu vya Tanzania.

Lakini hana bahati ya kutajwa vizuri, angalau kukumbukwa tu kwa rekodi zake.
 
Kwahiyo unataka kumaanisha kuwa waliofeli walikuwa na IQ ndogo kimpira?

Walikuwa hawawezi kuusoma mchezo na kuendesha timu?

Walikuwa hawawezi kucheza position zaidi ya moja? Hawakuweza kuji position pindi wakiwa na wasipokua na mpira? Hawakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na haraka uwanjani?

Embu chambua kila kocha aliyefeli ukijusisha na factors zako hapo juu. Tuone hao wachezaji unaowaita bora halafu wakashindwa kuusoma mcheza, kuji position n.k ni yupi katika hilo kundi?
 
Hongera mkuu.

Andiko lako la kiufundi sana.
Lakini kwa Tanzania sifa nyingi kwa Abdallah Kibadeni "King"

Huyu mwamba amepata mafanikio mengi sana akiwa na Simba sport kuliko makocha wote waliofanya kazi na vikabu vya Tanzania.

Lakini hana bahati ya kutajwa vizuri, angalau kukumbukwa tu kwa rekodi zake.
Nitakuwa wa mwisho kuamini hii mada ipo kiufundi. Kwamba Tony Adams kafeli ukocha sababu alikuwa na IQ ndogo kwenye mpira, alikuwa hawezi kuusoma mchezo na kuendesha timu, hajui kuji position, n.k.
Kucheza mpira ni swala lingine na kuufundisha ni swala lingine.
Kuna makocha ambao hawakuwahi kucheza mpira je wao mliwapima lini IQ zao za uwanjani?
Arrigo Sacchi, Carlos Parreira, n.k ni miongoni mwa makocha ambao wamefanya vizuri ila hawakicheza mpira
 
Nitakuwa wa mwisho kuamini hii mada ipo kiufundi. Kwamba Tony Adams kafeli ukocha sababu alikuwa na IQ ndogo kwenye mpira, alikuwa hawezi kuusoma mchezo na kuendesha timu, hajui kuji position, n.k.
Kucheza mpira ni swala lingine na kuufundisha ni swala lingine.
Kuna makocha ambao hawakuwahi kucheza mpira je wao mliwapima lini IQ zao za uwanjani?
Arrigo Sacchi, Carlos Parreira, n.k ni miongoni mwa makocha ambao wamefanya vizuri ila hawakicheza mpira
Mkuu mada mezani ni mafanikio na kufeli kwa makocha waliowahi kusakata soka.

Mleta mada hajakosoa uwezo wa makocha wakubwa, wenye majina, ambao wameutendea haki mchezo wa soka na ambao hawakucheza mpira kabisa ama hawakupata mafanikio kwenye kucheza kwao.
Vinginevyo Kocha wa soka anapimwa kwa mafanikio ya timu alizofundisha.
 
Minziro mtoe hapo
Ni kocha mzuri ila mazingira yetu ya Simba na Yanga yanamficha
Laiti angeenda hata Azam halafu apewe uhuru wa kufanya Kazi yake,naamini tungeona kitu cha tofauti
Binafsi siamini kama minziro anaweza kufundisha soka kwenye vilabu vikubwa.

Ni mwalimu ambaye anaamini ili mchezaji ucheze yakupaswa kukimbia sana(pumzi nyingi sanal,kuwa na nguvu kupita kiasi, kukamia na kucheza rafu ili kumtoa mpinzani mchezoni.

Nina uhakika akienda hapo Azam na kuambiwa achague nani na nani wabaki, anaweza kumbakiza Mbombo na Asamoah.

Makocha wengi wa kiswahili wapo hivi..
 
Mara kadhaa niliwahi kuahidi kuleta uzi unaohusiana na mada hii, leo nimetulia kidogo nimeukumbuka. Ngoja nitiririke.

Kuna hii kasumba iliyojengeka kwenye mpira kudhani kuwa mchezaji yoyote hasa akitokea kupata mafanikio fulani kama mchezaji anaweza kuja kuwa kocha mzuri pale atakapostaafu. Mimi binafsi naamini IQ ya mchezaji ndiyo itakayoamua kama mchezaji atakuja kuwa kocha mzuri. Mchezaji anaweza kuwa alikuwa anafunga sanaa enzi za uchezaji wake kama kina Ole Gunar Solskjaer na bado asiweze kuja kuwa kocha mzuri. Ukocha siyo kama ukuu wa wilaya kwamba unaweza ukaficha madhaifu yako siku zikasonga.

Huko nje mifano ipo mingi sana ya wachezaji ambao enzi za uchezaji wao walikuwa mahiri sana ila walipoenda kwenye ukocha ilikuwa ni majanga matupu. Alan Shearer ambaye bado anashikiria rekodi za ufungaji bora huko Uingereza ila alipewa timu aifundishe ikashuka daraja. Sir Bobby Charlton anayeaminika ni mchezaji bora wa muda wote kutokea pale Uingereza, huyu naye alipewa timu akaishusha daraja. Thiery Henry ana mafaniko mengi sana ya binafsi kama mchezaji na alizoipatia klabu zake na timu yake ya taifa na baada ya kustaafu alipewa mikoba ya ukocha katika timu ya AS Monaco, ila baada ya miezi 3 akafukuzwa baada ya kuitumikia kwa mechi 20 tu huku 11 akiwa amepoteza.

Kuna Tony Adams, mmoja wa wachezaji wanaoheshimika mno huko Uingereza hadi wamemjengea sanamu yake pale nje ya uwanja wa Arsenal wa Emirates ambayo aliitumikia kwa miaka 22 kama mchezaji. Huyu baada ya kustaafu, timu mbili alizofundisha amezishusha daraja.

Kuna Paul Gascoigne "Gaza" na Stoichkov. Kuna Paul Scholes na mwenzake Gary Neville, wote wawili zao la Alex Ferguson pale Man United lakini wote walishindwa vibaya sana katika ukocha. Kuna Lothar Matthaus, legend wa Ujerumani ambaye timu yake ya Celta Vigo ilishuka daraja ikiwa katika mikono yake ya ukocha. Hapo sijamtaja Diego Maradona, legend mwingine wa soka ila zama zake kama kocha zilikuwa ni za visanga tu.

Tanzania tumeshuhudia wachezaji kadhaa wa zamani waliowahi kuchezea timu kubwa mfano za Simba na Yanga ambao walikuja kuwa makocha. Mifano inayonijia haraka ni Fred Felix "Minziro" huyu amefundisha kwa muda mrefu sana ila hana rekodi yoyote ya kujivunia. Kuna Mohamed Hussein "Mmachinga" mchezaji ambaye kama liivyo kwa Alan Shearer bado anashikiria rekodi katika ufungaji bora katika ligi kuu ila mpaka leo hana mafanikio yoyote katika ukocha. Sina uhakika kama Mmachinga ameshawahi kufundisha ligi kuu ila mara ya mwisho nimemuona anafundisha kwenye bonanza kwenye kombe ya Ramadhani. Kuna Jamhuri Kihwelo, naye baada ya kufundisha kwa muda mrefu hana lolote la kujivunia katika ukocha pamoja na kwamba enzi zake za uchezaji alipewa sifa kedekede. Kuna Joseph Lazaro na Juma Mgunda ambao naona kama bado wanajitafuta. Selemani Matola bado amekuwa chini ya miamvuli ya makocha wengine, bado hatujamuona akiongoza timu kama kocha mkuu kwa hiyo hatuwezi kumuhukumu bado. Wachezaji pekee wa ndani ambao naweza kusema waliweza kupata mafanikio kama makocha ni Abdallah Kibadeni na Charles Boniface "Mkwasa". Huyu Mkwasa namtaja ila inabidi nirudi kuhakiki rekodi zake maana najua amefundisha sana timu ya taifa ila sina uhakika kama kuna mafanikio yoyote yaliyopatikana chini ya mikono yake.

Ili mchezaji aweze kuwa kocha mzuri inabidi awe na IQ kubwa ya kimpira yeye kama mchezaji kwanza. Kupima IQ ya kimpira inabidi uwe na jicho la kuangalia mchezaji anavyocheza uwanjani. Naangalia uwezo wa kucheza position zaidi ya moja uwanjani, uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na ya haraka akiwa na mpira, anavyojiposition anapokuwa hana mpira, uwezo wa kuusoma mchezo na kuiendesha timu uwanjani.

Nikitumia sampo zilizoko katika vikosi vya Simba na Yanga msimu huu, wachezaji ambao kwa haraka haraka wananijia kichwani kuwa kwa mtazamo wangu wanaweza kuwa sifa hizo na hivyo wanaweza kuja kuwa makocha wazuri ni pamoja na Djigui Diarra, Khalid Aucho, Che Malone, Moses Phiri, Max Nzengeli, Aziz Ki, Dickson Job, Fabrice Ngoma, Luis Miquisonne, Clatous Chama na ziada naweza kuwaongeza Shomari Kapombe na Feisal Salum (Azam). Kwa sababu ligi ya NBC sasa hivi inajumuisha wachezaji kutoka nje, nimeona mifano yangu iwajumuishe pia.

Uzi huu umejikita zaidi kuangalia wachezaji wakubwa ambao walifeli kuwa makocha. Kwa wachezaji wa nje kuna ambao walikuja kufanikiwa sana kama makocha mfano Diego Simeone, Zidane, Cruyff, Guardiola, Ancelotti, del Bosque, Antonio Conte, Beckenbauer na Mancini.

Kwa Tanzania, wachezaji wa zamani ambao kwa sifa ambazo nimesikia walikuwa nazo kwa mtazamo wangu naona kama wangeweza kuwa makocha wazuri ni Edibily Lunyamila, Salvatory Edward, Hussein Marsha, Kenny Mkapa, Hamis Gaga "Gagarino", Malota Soma, Method Mogella, Yusuph Macho na Athumani China. Sina uhakika katika hawa kuna ambaye alishajaribu ukocha ila inawezekana nao wangeishia kuwa na mafanikio kama ya Jaluo na Minziro.
Kama ni assignment nakupa: C
 
🤣🤣🤣
Kibongobongo hamna hiyo
Ngasa mla msuba ameshindwa kuwa kocha,ingawa mlimsifia ni mchezaji Bora kumbe zilikuwa bhange zinacheza🤣🤣
 
Binafsi siamini kama minziro anaweza kufundisha soka kwenye vilabu vikubwa.

Ni mwalimu ambaye anaamini ili mchezaji ucheze yakupaswa kukimbia sana(pumzi nyingi sanal,kuwa na nguvu kupita kiasi, kukamia na kucheza rafu ili kumtoa mpinzani mchezoni.

Nina uhakika akienda hapo Azam na kuambiwa achague nani na nani wabaki, anaweza kumbakiza Mbombo na Asamoah.

Makocha wengi wa kiswahili wapo hivi..
Minziro mtoe hapo.

Ni kocha mzuri ila mazingira yetu ya Simba na Yanga yanamficha.

Laiti angeenda hata Azam halafu apewe uhuru wa kufanya Kazi yake,naamini tungeona kitu cha tofauti
Minziro hana rekodi yoyote ya kujivunia? Hizi timu alizopandisha daraja sio rekodi?
Satan nakubaliana na wewe kabisa.

New City Minziro kacheza ligi kuu tena Yanga kwa kipindi kirefu, kafundisha sana ligi kuu ikiwemo Yanga na nadhani ni zaidi ya mara moja, halafu tony92 anasema mafanikio yake pekee anayoweza kuyataja kama kocha ni kuipandisha timu daraja. Asante kwa kuipa point yangu msisitizo.
 
Yaani kama kuna kocha wa ajabu huku duniani ni Zenedin Zidane zizou. Huyu jamaa ukimwangalia unaweza kudhani ni bonge la kocha.

Kumbe alibebwa na ile b.b.c. Tangu aanze ukocha kafundisha real Madrid pekeakea. Kila timu wakimwaproach anakataa. Anajua kabisa bila bbc hawezi kupata chochote.

Gerald, Lampard, Ole Guna, Di Mateo, zola nk hapa hakuna makocha.

Mwisho Uingereza haina au ina uhaba wa makocha. Vilabu vyote vikubwa vinavyocheza ligi kuu ya epl tangu mwanzo wa miaka ya 1990 mpaka napoandika hii post hawana kocha aliyebeba kombe. Wote ni wageni. Wenyewe ni kelele tu kama vyura.
Zidane hauwezi kumhukumu kisa kapata mafanikio kwa kufundisha timu moja au kuwa na mastar. Kuna makocha wengi walikuwa na vikosi vyenye mastar wakashindwa kufanikiwa na wengine tunawasifu kwa mafanikio waliyoyapata katika timu moja.

Steven Gerrard ni mmoja wa wachezaji wachache wa Uingereza ambao nimewahi kuwaona wana IQ kubwa ya mpira na alipoenda Scotland kama kocha alipata ubingwa bila kufungwa hata mechi moja.
 
Mkuu mada mezani ni mafanikio na kufeli kwa makocha waliowahi kusakata soka.

Mleta mada hajakosoa uwezo wa makocha wakubwa, wenye majina, ambao wameutendea haki mchezo wa soka na ambao hawakucheza mpira kabisa ama hawakupata mafanikio kwenye kucheza kwao.
Vinginevyo Kocha wa soka anapimwa kwa mafanikio ya timu alizofundisha.
Basi hukusoma mada yote tena kwa utulivu, umepalaza palaza tu kusoma.

Nanukuu "Ili mchezaji aweze kuwa kocha mzuri inabidi awe na IQ kubwa ya kimpira yeye kama mchezaji kwanza. Kupima IQ ya kimpira inabidi uwe na jicho la kuangalia mchezaji anavyocheza uwanjani. Naangalia uwezo wa kucheza position zaidi ya moja uwanjani, uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na ya haraka akiwa na mpira, anavyojiposition anapokuwa hana mpira, uwezo wa kuusoma mchezo na kuiendesha timu uwanjani.
Mwisho wa kunukuu.

Ukisoma hayo maelezo hayo juu utaona ujumbe wake ni kuwa makocha wazuri na wenye mafanikio ni waliokidhi vigezo vyake mleta mada ambayo ni hivyo hapo juu. Jambo ambalo sio kweli.
 
Basi hukusoma mada yote tena kwa utulivu, umepalaza palaza tu kusoma.

Nanukuu "Ili mchezaji aweze kuwa kocha mzuri inabidi awe na IQ kubwa ya kimpira yeye kama mchezaji kwanza. Kupima IQ ya kimpira inabidi uwe na jicho la kuangalia mchezaji anavyocheza uwanjani. Naangalia uwezo wa kucheza position zaidi ya moja uwanjani, uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na ya haraka akiwa na mpira, anavyojiposition anapokuwa hana mpira, uwezo wa kuusoma mchezo na kuiendesha timu uwanjani.
Mwisho wa kunukuu.

Ukisoma hayo maelezo hayo juu utaona ujumbe wake ni kuwa makocha wazuri na wenye mafanikio ni waliokidhi vigezo vyake mleta mada ambayo ni hivyo hapo juu. Jambo ambalo sio kweli.
Unalazimisha mambo ambayo hayapo. Kama umeshindwa kuelewa mada, basi soma hata title ya uzi ikusaidie.

Hapa tunaangalia wachezaji waliocheza katika viwango vya juu vya mafanikio binafsi na waliyopatia timu zao halafu wakaja kuwa makocha wakafeli.
 
Unalazimisha mambo ambayo hayapo. Kama umeshindwa kuelewa mada, basi soma hata title ya uzi ikusaidie.

Hapa tunaangalia wachezaji waliocheza katika viwango vya juu vya mafanikio binafsi au waliyopatia timu zao halafu wakaja kuwa makocha halafu wakafeli.
Kwahiyo factors ulizoanisha za mchezaji mpira kuja kuwa kocha mzuri nizi ignore? Sio sehemu ya mada? Au hazikuwa na umuhimu?
Binafsi kwenye uzi wako, ujumbe nimeona hapo kwenye factors ambazo zitamfanya mchezaji aje kuwa kocha mzuri au mbaya. Sasa tujadili hizo factor zako kama zina usahihi. Usipaniki umeleta hoja mezani ijadiliwe kiufundi, sasa hasira za nini za kukataa vitu ambavyo umeviandika wewe mwenyewe?
 
Back
Top Bottom