Nimesema siku zote kwamba mtu ama kiongozi yeyote anayekubali kupeana mkono na Shetani basi huyo sii kiongozi..
Mi sielewi ni imani ipi anayozungumzia Mzee Sitta?.. Huyu Lowassa na Rostam hawa kwa pamoja ni muumini wa chama CCM. Wote wako kanisa moja, wana imani moja wanachotofautiana ni vitendo vyao, hivyop Upatanisho pekee ambao unaweza kuleta maana ni pale huyu Sitta atakapo kataa uongozi wa hawa watu ndani ya kanisa lake..
Mfano wake wa Katoliki/Protentant au Karume na Seif hii ni mifano dhaifu sana kwani hawa watu wanatengana kiimani kwanza, tafsiri ya imani zao ktk kumjenga binadamu zinagongana na hawaelewani kiimani. Kwa hiyo tunachoona kwao ni suluhu baina ya imani mbili tofauti kuweka amani baina yao.. Yaani kifupi amini unachoamini nami nitaamini nachoamini usiwalazimishe watu wangu kufuatana imani yako. lakini ktk swala la Sitta, hii ni suluhu ya waumini wenyewe wenye imani moja ambao kati yao kuna wale wanaokiuka maadili ya imani tangulizi. Kupinga kwa Sitta ndani ya imani hiyo hakuwezi kuwasaidia wauumini wala kuwalinda dhidi na vitendo dhalimu vya hawa viongozi.
Hivyo basi suluhu ya mzee Sitta ni ktk kukubali yaishe, wameshinda wao!...ni suluhu inamhusu yeye binafsi au chama (kanisa) na sii kwa maslahi ya upatanisho wa imani mbili tofauti wananchi bali upatanisho wa matendo..in other word, shake hand with a devil, kwani unaweza kumlaani shetani kanisani lakini ukaendeleza ushetani nje ya kanisa!
Lawama zote nazipeleka kwa baba wa Taifa, marehemu mwalimu Nyerere ambaye alirithisha madaraka ya nchi yetu kwa wahuni! Haya nayoyasikia leo ni uhuni mtupu..Na matokeo yote ya Ufisadi na uharamia nchini umetokana na mwalimu mwenyewe kukabidhi nchi yetu watu wasiofaa kabisa kuwa viongozi...Kikwete hawezi kubadilisha kitu na hakuna kiongozi yeyote anayeweza kubadilisha hali hii issipokuwa kiongozi dikteta kama Kagame ambaye aliwaxhalaza bakora kwanza Wahutu na Watusi hadi wakaweka akili, wakanyooka kisha ndio akaweza kuiendeleza nchi... kinyume cha hapo tusahau na haihitaji elimu ya juu sana kuelewa.
Na nasema hivi, haitatokea kiongozi yeyote ambaye ataweza kuirudisha nchi yetu ktk mstari pasipo kuwa Dikteta.. na hakika kura yangu nitampa..
Wakati wa kudanganyana umekwisha!..Iwapo imani ya Sitta ni kuukashifu Ufisadi kanisani wakati akijua fika kwamba kanisa lake mwenyewe linaendesha sala za kumshirikisha shetani sijui atachoweza kukemea ni kitu gani..