Sitta, Mwakyembe, Manyanya, Mtangi jitokezeni sasa kuonyesha uzalendo wenu

Indume Yene

Platinum Member
Mar 17, 2008
2,950
711
Malipo ya Dowans yamechukuwa nafasi kubwa katika habari nchini mwetu. Kuna kila sababu ya kuchukuwa hiyo nafasi kutokana na upuuzi unaofanywa na serikali inayoongozwa na Jakaya Kikwete kukimbilia kulipa DOWANS.

Wiki kadhaa zilizopita aliyekuwa spika wa bunge lililopita Mh. Sitta alitamka wazi kuwa kuwalipa Dowans ni kuhujumu uchumi. Akaenda mbali na kudai kuwa Dowans ni genge la watu 3 ambao wanajiandaa kukomba hiyo hela kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu 2015.

Huyo alikuwa kiongozi wa bunge, aliunda kamati iliyoongozwa na Mh. Mwakyembe kuchunguza kashfa ya Richmond ambayo baadaye ilirithiwa na Dowans. Na matokeo ya ile kamati kila mtu anajua, ingawa ukweli mwingine bado umefichwa kwa makusudi ya kulinda maslahi ya watu fulani.

Nakumbuka Mh. Mwakyembe aliwahi kutamka hata kwenye vyombo vya habari kuwa kuna mambo mengine walificha kwa ajili ya usalama wa Taifa, kitu ambacho mie sikubaliani nacho.

Nikirudi kwenye kiini cha hii thread:

Mh. Sitta anaelewa wazi huu uhuni wa serikali wa kutaka kulipa Dowans. Sidhani kama alikurupuka kudai kuwa Dowans ni genge la watu 3. Anaelewa wamiliki ni nani. Kama ni kiongozi asiyependa majungu, kwa nini asije mbele ya UMMA na kutueleza anachokifahamu? Kama anajua kuwa Dowans ni genge la watu 3 huku waziri Ngeleja akitaja zaidi ya watu 3, kwa nini asiwataje tuone serikali itamfanya na kusema nini.

Hata Mh. Mwakyembe na wengine ambao walikuwa kwenye ile kamati, wanajisikiaje kuona nchi inatafunwa huku wakijua ukweli? Kama hawa watu hawataki kutupa ukweli inabidi tuwalazimishe watuambie ukweli. Hakuna mtu ambaye anaweza kushindana na nguvu ya UMMA. Mfano halisi ni kile kilichotokea Arusha juzi, sasa serikali inajiumauma kuwa wanataka mazungumzo. Hawakutaka hata hayo mazungumzo at a first place lakini wameona nguvu ya umma ikitumika ndio wanajikosha kuwa ooh mazungumzo.

Waziri Sitta, Mwakyembe, Eng. Manyanya, Seleli na wengineo, tafadhali tuelezeni mnachokifahamu kuhusu Dowans kwa kulinda mali na maslahi ya Taifa letu.

Kila kiongozi wa jamii anatakiwa kusimama ahesabiwe kuhusu suala hili la WIZI wa MCHANA kulipa Dowans.
 
inabidi ujiulize kwa nini walichaguliwa kuwa mawaziri? ili wawafunge na collective responsibility au wawape hela chafu halfu washindwe kuwa huru
 
inabidi ujiulize kwa nini walichaguliwa kuwa mawaziri? ili wawafunge na collective responsibility au wawape hela chafu halfu washindwe kuwa huru

Mkuu nakubaliana na wewe.
Nafikiri huu ni muda muafaka kwa viongozi wa jamii kusimama tuwahesabu tujue misimamo yao dhidi ya hili genge la wahujumu uchumi wetu.
 
Billion 185 kama utaziwekeza ktk usimamizi mzuri ktk bonde bikira la kilombero au usangu kama sio rufiji basi njaa itakuwa historia ktk taifa hili na hata pengine zingeweza kusaidia kushusha bei za vyakula na kukabiliana na mfumuko wa bei.

Ni wakati sasa wa wale mitume 12 wa ccm chini ya mzee sitta kuonyesha uzalendo wao kwa kuwaeleza nini kilichojificha nyuma ya dowans kama sehemu ya huruma yao kwa masikini wa kitanzania,ni kipimo cha uzalendo kwa taifa la tanzania
 
Ktk hili nipo upande wa kuwataka hawa waliofichua kuanzia Richmond na baadae Dowans waonyeshe uaminifu wao kwa wapiga kura wao. S. Sitta keshasema huu ni mchezo wa watu watatu kujitayarisha na uchaguzi 2015. hapa ni JK, EL na RA. anayetaka uraisi ni EL, na amekwishaanza kampeni. SS na wenzako, waambieni wapiga kura kinachojiri ili wafanye maamuzi.

nawasilisha P.P
 
Wameishafanya mengi! yapasa na sisi tujitokeze tukatae! tusitegemee wao wawe pioneers kwa kila jambo! tukatae sote kwa pamoja! tuingie mitaani tuandamane wenye kufa tufe ili kizazi kijacho kifaidi ujasiri wetu!
 
usitegemee mtu yeyote kupinga malipo haya, hela lazima zilipwe kabla ya kikao cha bunge na hakuna mtu yeyote wa kuhoji au kutoa maoni kwenye vyombo vya habari kuhusu malipo haya. wote tunajua ni usanii ila tuanzie wapi? . Hawa uliowataja wote wameshakata kauli, huyu 6 mnampa sifa za bure, kaburuzwa kwenye chama chake, kapewa uwaziri kifuta jasho ana hamu tena? tumebakia na DR Slaa tu ndiyo tegemeo letu watanzania. nchi hii ina wenyewe ndugu zangu.
 
Ndio waliowalazimisha wataalamu wafanye kazi kisiasa, tukaingia hasara..

Besides, amepewa alichokitafuta kimya...mpole
 
sitta,mwakyembe jitokezeni sasa kuonyesha uzalendo wenu

Kazi wanayo...hata kama wana msimamo tofauti sasa hatasikilizwa hata wakipiga kelele maana wako katika
sehemu ya maamuzi ya baraza la mawaziri.Mengi yatakuwa yanapita usoni mwao na watakuwa hawana njia
bali kukubali yapite!
 
katika umri alionao, unategemea akosoe halafu yamkute yaliyomkuta mrema huko nyuma? sita si mjinga kiasi hicho, sanasana sie tunaomwamini kuwa mzee wa viwano ndio tujichunguze vizuri
 
hao ndio habari yao imeisha wameshafungwa mdomo,hawawezi kuongea tena kama mwanzo....kama wao wanajua kitu na wanalitakia mema taifa wajiuzuru uwaziri...na wamwage ukweli...na watanganyika tutakuwa upande wao.....WAPIGANAJI WENGINE KIMYA KAMA HAYAWAHUSU ..
 
Mh. Dr. H. Mwakyembe, Mbunge na Waziri, mwaka 2008 ukiwa Kiongozi wa kamati teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond una nini la kusema kuhusu yanayotokea nchini mwetu ?

Nakumbuka kuna wakati uliwahi kumtaka Spika avunje kanuni na kurejesha suala la Richmond bungeni ili uweze kuyaanika hata yale ambayo ulibaki nayo moyoni kwa ajili ya kuinusuru serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.

Napata shida kidogo kuukubali ukweli kuwa wewe hivi sasa ni sehemu ya hiyo serikali uliyoisetiri kwa kufunika kombe mwanaharamu apite.

Pamoja na hayo, ni wazi kuwa kwa kitendo chako cha kuficha maradhi sasa watanzania tuko kwenye kilio kikubwa na wewe uko kimya !

Je, unasemaje Mheshimiwa.

 
Hii ya watu dizaini ya kina Sitta, Mwakyembe kujidai ni vinara wa kupambana na ufisadi ni ubabaishaji tu. Huwezi kuwa mpambanaji huku ukishirikiana na mafisadi. Kuna msemo "You're either pregnant or not. You're either on the plane or you missed it" - hivyo tusitarajie lolote jipya kutoka kwa hawa jamaa. Wanatetea mlo wao tu!
 
Hii ya watu dizaini ya kina Sitta, Mwakyembe kujidai ni vinara wa kupambana na ufisadi ni ubabaishaji tu. Huwezi kuwa mpambanaji huku ukishirikiana na mafisadi. Kuna msemo "You're either pregnant or not. You're either on the plane or you missed it" - hivyo tusitarajie lolote jipya kutoka kwa hawa jamaa. Wanatetea mlo wao tu!

Hata maandiko matakatifu yasema pia kuwa uwe baridi au moto lakini huwezi vuguvugu. Sielewi ni kwa nini hadi sasa wametulia tu. Kwani Mwakyembe kabla ya kuwa naibu waziri si alijulikana kama mbunge? Ni jukumu la kutetea maslahi ya Taifa, mwandikie JK barua ya ku-resign kisha ueleze kile unachokijua.
 
Hawajawahi kuwa wazalendo,kama wangekuwa wazalendo wangemaliza swala hili kabla,ila huyu mwakyembe alisema et kuna mengine ameameacha,
Hawa ni wale wale,,,,tushikamane sie wana wa nchi kupambambana juu ya huu ufisadi,mapinduzi ya ufaransa hayakufanywa na viongozi bali wananchi maskini,,yes we can join the course
 
Back
Top Bottom