Sitta: Kuna Wabunge mizigo CCM

Sitta: Kuna Wabunge mizigo CCM

Tunakutambua Mzee Sitta ,Mguu mmoja ndani mwingine nje. yaani huaminiki tena tabia yako ya kuropoka inakumaliza ki siasa.
 
Mbunge wa Urambo mashariki na Waziri wa Afrika Mashariki Samwel Sitta amesema kuwa baadhi ya Wabunge wa Ccm ni mizigo na wanabebwa tu na Chama kwani hawana lolote zaidi ya kulala bungeni na hawachangii lolote.

Source; Gazeti la mwananchi.
 
Watu hamna shukran! Akikaa kimya mnamsema ooh kanunuliwa ndio maana kawa bubu. Akikikosoa chama chake bado mnamsema sasa lipi jema kwenu?

Mkuu ukitaka kuwa mbaya ndani ya ccm kosoa chama. Na ukitaka promosheni sifia chama, tetea chama kwa lolote, jema au baya jua au mvua.
 
Mimi structure ya benzine mpaka leo inani-comfuse..Hivi nyoka akiuma mkia wake sumu inaenda wapi?? Sitta ni miongoni mwa mawaziri waliopigwa picha na gazeti akiwa amelala bungeni!!
 
Sitta ajiandae kwa mashambulizi mazito kutoka kwa makada wenzake wa CCM. Muda si mrefu wataanza kumnanga, kumsuta na hata kumvua nguo.
Asije naye kukana kauli yake kama Nape alivyofanya juzi.
 
Mzee 6 hana lolote kelele zote hizo ni hasira za uspika,aseme tu kuwa ccm ni mzigo mbona wabunge wa ccm ni components za ccm...kwa nini awatenge wabunge na chama chao?.mzee hajitambui...muacheni apige kelele...kama anaona vp aende upinzani,mizee mingine bhana.
 
Urambo iko kama Pretoria

Hebu acha utani wa KISHINDO kijana. Nchi nzima itakuwa kama New york CHADEMA TUKISHIKA MADARAKA KUANZIA 2015 ONWARD yaani namaanisha pesa za mafisadi zote zitarudishwa serikalini.
 
Sitta naye mzigo tu, inamaana wabunge wa CCM wakienda bungeni kazi yao ni kuchachafya upinzani na si kuwawakilisha wananchi na kuibana serikali kutimiza wajibu wake?
 
jema kwetu aende chama kingine tutulie na unafiki wake huyu jizere

LAKINI mwenyekiti kamuona jembe hadi kamkabidhi WIZARA!
Iweje nyie magamba watoto muone hafai?
Au siku hizi hazidumu fikra za mwenyekiti?
 
Tatizo la CCM hawapendi kuambiwa ukweli ....akisema mtu wa nje ya CCM ataambiwa wewe CDM...akisema wa kwao ndani oooh huyu msaliti....jaribuni kubadilika na mkubali mabadiliko .....Mzee Sitta kaongea ukweli kwa wale walio mizigo ndani ya Bunge na kwenye majimbo yao kama Mh Filikunjombe alivyowachana wanaosimama kuchangia uenezi wa porojo badala ya mijadala iliyo bungeni na mwisho wanasema anaunga mkono hoja
 
Mwenda bure si mkaa bure, wakati fulani 6 huwa zinachaji kweli kweli, ni aibu bila kujali itikadi za vyama mbunge kwenda kulala au kula bungeni bila kazi, Hongera 6.
 
Back
Top Bottom