Waziri wa Afrika mashariki Mh. Samweli Sitta amesema CCM wanatakiwa kujiangalia upya kuhusu mwenendo wa viongozi walio wengi wa chama hicho ambao wanakipeleka chama pabaya na chama kupoteza umaarufu mbele za wananchi!! Sitta amedai chama kiko kwny hali mbaya sasa kutokana na baadhi ya viongozi kuchanganya kazi za chama na biashara kubwa kubwa, ameenda mbali na kusema hatua zisipochukuliwa mapema chama kinaweza kuanguka vibaya. Vile vile ameonya CCM iache kutumia dola kupambana na upinzani bali ijibu hoja na si vinginevyo!! Katika hili namsifu sana Mh. Sitta kwa ushuri huu mzuri kwa chama chake.
Source: ITV Habari
Source: ITV Habari