Sitta afanya maajabu ya karne

Sitta afanya maajabu ya karne

usiongee kitu km huna uhakika. sijaona fact wala evidence yoyote zaidi ya hisia zako binafsi. tusikubali kuendesha Taifa kwa hisia na majungu

Kwahiyo tukubali uendesha taifa kwa ungese wa Sitta na mabwege wenzake?
 
Hicho king'ang'anizi ndizo kitanzi chao katika uchaguzi wa 2015.

Bahati mbaya watanzania huwa tunasahau haraka sana. Pamoja na kuvurunda kwote bado CCM watapeta kama hakuna baya lolote walilolifanya...hii issue ingewacost kwenye uchaguzi wa local government lakini mambo yatakuwa tofauti. ...
 
Hiyo akidi imepatikanaje?.

Nalia na ukawa.kama kuna majasiri wamejitokeza na kupiga kura ya wazi tena ya hapana,vipi ukawa wangekuwepo na kupiga debe kura ya hapana?ni dhahiri hata kuchakachua ingeshindikana.
 
Samuel Sitta mwenyekiti wa bunge maalum la katiba imebidi alazimishe ushindi kwa upande wa Zanzibar kwenye rasimu, nimethibitisha.

Uhakika ni kwamba mwenyekiti huyo atatangaza matokeo ya ushindi huku yakigubikwa na utata mkubwa na huenda yakazua tafrani kubwa.

Katika hali ya kushangaza ni kuwa wajumbe wote wa kura ya siri walipiga kura ya 'ndiyo' huku kura nyinhine zikiongezwa ili kukidhi akidi na haijulikani zilikotoka.

Bunge hilo linafikia tamati hivi leo huku likiibua mpasuko mkubwa nchini.

Hivyo ndivyo ilivyo! Akidi kwa upande wa Zanzibar imepatikana na ilivyopatikana anajua mwenyewe Sitta!

Yeye amejitetea kuwa "kuupitisha huu mchakato kwa gharama yoyote ile ni kuliokoa taifa na ni mpango wa Mungu"

Hii habari pia nimeisikia kwenye gazeti la Raia Tanzania la leo alhamisi.

Kuna tetesi kuwa huenda Kikwete akaingilia kati kushauri usitishwaji wa upigaji kura ili hali iishie hapa ilikofikia ingawa ni tetesi tu!
tumeonaa
 
Tumeshuhudia wenzetu wakijaribu kwenda hata mwezini na sasa Mars (mf. India) kwa kutegemea nguvu za siasa, je kwa siasa zetu hizi kweli tutaweza hata kutengeneza ngalawa ya kwenda Zanzibar bila kutegemea wafadhili!?
 
Hii ni rasimu na si katiba halisi. Kutokana na mambo yaliyojitokeza wazi na rasimu hiyo kupingwa kila upande, ni vigumu kwa rasimu hiyo kukubaliwa na kupitishwa kuwa katiba ya Tanzania na wananchi. Wanachokifanya sasa Dodoma ni kupoteza pesa za wananchi kwani katiba haitapatikana kutoka kwenye rasimu hii ya ccm.

Wananchi wataburuzwa tu.
 
Viongozi wa nchi hii ni wa ajabu kweli...sasa hawa wajumbe wa BMK wanafurahia utadhani ndiyo mwisho wa mchakato na Katiba mpya imeshapatikana hiyo waliyoipanga wao.....hii inaonyesha kwamba kitu walichokopitisha wao ndiyo hicho hata kama wananchi hawakitaki.....kweli Watanzani ni wapole cjui hao hatujui haki zetu......
 
usiongee kitu km huna uhakika. sijaona fact wala evidence yoyote zaidi ya hisia zako binafsi. tusikubali kuendesha Taifa kwa hisia na majungu

Kwa akili yako (kama unayo) unaona Taifa hili linaendeshwa kwa fact? Wooote tulio na akili tunajua kwamba kinachotumika ni hisia na nadhalia ktk taifa; Kwamba sisi ni wajamaa. kwamba sisi ni wazalendo. kwamba kiswahili ni lugha bora sana! Kwamba hiyo ni katiba bora sana.

Unaweza ukatumia mtu mwizi kuwa m/kiti wa kamati ya uandishi halafu upate katiba bora? Nonsense!
 
Kwa akili ya 6 anaweza kufanya haya lakn wajue twawasubiri huku mtaaani tuwakimbize na katiba ya ya CCM
 
usiongee kitu km huna uhakika. sijaona fact wala evidence yoyote zaidi ya hisia zako binafsi. tusikubali kuendesha Taifa kwa hisia na majungu
Mkuu una lingine? fuatilia mwenyewe mimi matokeo nimeyapata leo saa kumi alfajiri!!
 
Jana usiku Sitta alifanya vituko kama chizi yani hadi nikawa namshangaa!! Kwa kweli Sitta kwa nilivyomuona usiku ule "anavuta bangi"

Chezea kutimiliza 2/3
 
tatizo la watanganyika kutwa kulalamika mitandaoni lakini mkiambiwa mkadai haki yenu mnaanza tilalila. CCM wamepata katiba yao lkn watanzania mnaenda kuipigia kura hivi mnaakili kweli?

Hii katiba sitta kalazimisha ili asiumbuke ila ipo cku atajuta. Nawaomben watanganyika tuoneshe moyo wa uzalendo 2dai katiba yetu.
 
Hii ni rasimu na si katiba halisi. Kutokana na mambo yaliyojitokeza wazi na rasimu hiyo kupingwa kila upande, ni vigumu kwa rasimu hiyo kukubaliwa na kupitishwa kuwa katiba ya Tanzania na wananchi. Wanachokifanya sasa Dodoma ni kupoteza pesa za wananchi kwani katiba haitapatikana kutoka kwenye rasimu hii ya ccm.
mkuu kama wameweza kuchakachua mchana kweupe namna hii watashindwa vp kuchakachua kura za maoni?
 
Back
Top Bottom