Sitasahau!!!

Susy

JF-Expert Member
Feb 5, 2011
1,431
220
Asalam aleikum!!!

Bwana Yesu asifiwe!!

Nimesoma thread ya Lizy kuhusu unyanyasaji wa watoto ikanikumbusha mbali sana, hakika imenitoa machozi!!

Nakumbuka miaka ya nyuma sana wakati nikiwa na miaka 4 tu, mama yangu alifariki kwa ugonjwa wa cancer, hatukukaa hata mwaka baba naye alifariki na ugonjwa wa figo, hapo ndipo nilipotamani dunia igeuke chini juu.

Nakumbuka dada yangu mkubwa alikuwa ndio kwanza yupo 4m3 na kaka yangu ambaye nafatana naye alikua yupo darasa la pili, tulinyang'anywa mali zote za baba yetu, tena tukarudishwa kijijini kabisa ambapo baba aliweka mifugo yake, baada ya muda bb mdg akaja akachukua ngombe wote wakagawana na watoto wa mama mkubwa.

Hakuna aliyetujali, tuliachiwa mbuzi tu pale kijijini, nakumbuka kaka yangu ilibidi aache shule aanze kuchunga hao mbuzi kwa taabu, mimi nilikua nachota maji na kufagia, hakuna aliyejua tunakula nini, tunavaa nini wala tunalala vipi. Dada yangu alichukuliwa na dada mtoto wa mm mkubwa na kugeuzwa house girl.

Nakumbuka wale rafikize baba walipoona hivyo, wakamlipia dada yangu ada tena kwa kuchangiwa na kijiji dada akarudi shule, jirani yetu mmoja akasema tuchanganye mbuzi zetu na zake ili kaka asiende kuchunga tena awe anaenda shule.

kutokana na baridi ya mkoa ambao tulikuwepo, na hatukuwa na blanket siku moja nilishikwa na naimonia ikiambatana na homa kali, yule bb mkubwa rafikiye baba akamtuma kaka yangu aende kwa ba-mdogo akamweleze, kaka yangu akapanda gari kwenda mjini kumwambia baba mdogo, baba mdogo akamwambia kama baba yake na mama yake wamekufa yeye anafaida gani, mwache afe akupunguzieni taabu!! kaka alirudi kijijini na kuomba msaada kwa yule rafiki yake na baba (ba-mkubwa) ndipo nikapelekwa hospitali na kulazwa, ikimlazimu kufanya vibarua vya kulima wakati akiwa mdogo ili kutupatia fedha za matumizi na kuniuguza.

kaka yangu mtoto wa m.mkubwa akaoa kule kijijini akatuchukua lakini niliona bora tulivyokuwa tunakaa wenyewe maana wifi alitunyanyasa sana, jina langu lilibadilika ghafla, nikawa naitwa mbwa, nakumbuka alikua ananiita hivi, "we mbwa mkubwa njoo hapa" ukifika tu unakutana na kibao kizito alafu ndio maagizo mengine yanafuatia!!!

Baada ya muda, wale wote waliotudhulumu alikufa mmoja baada ya mwingine, wale waliotunyanyasa kwa chakula leo ndio wanatuomba chakula, waliotulaza chini leo wanatembea wameinamisha vichwa vyao!!

"usimnyanyase yatima wala kumuonea mjane, mkono wa Mungu utakuwa juu yako"
 
Mungu ni baba wa Yatima na ni Mume wa wajane. Poleni sana Suzy. Ila namshukuru Mungu kwa sababu fadhili zake zilikuwa pamoja nanyi. Ndio maana amewaandalia meza machoni pa watesi wenu.

Songa mbele, na pia kumbuka Mungu aliwapitisha hapo ili mje kuwa msaada kwa Yatima na watu wengine wanaoteseka. Msiache kabisa kufanya utumishi huo.
UBARIKIWE
 
Daah
Pole sana mpenzi


Lakini mpenzi umepitia mengi
MShukuru Mungu kwa yote
Na walokutendea hayo yote wasamehe
Na mwachie Mungu..
jipongeze kwa hatua uliyofikia

Girl
Your so brave to share your story
Thanx my dear..
 
Mungu ni baba wa Yatima na ni Mume wa wajane. Poleni sana Suzy. Ila namshukuru Mungu kwa sababu fadhili zake zilikuwa pamoja nanyi. Ndio maana amewaandalia meza machoni pa watesi wenu.

Songa mbele, na pia kumbuka Mungu aliwapitisha hapo ili mje kuwa msaada kwa Yatima na watu wengine wanaoteseka. Msiache kabisa kufanya utumishi huo.
UBARIKIWE

LD namshukuru Mungu kwa sasa tunajenga kituo cha watoto yatima kule kibamba!! hatuwezi kusahau!!
 
Daah
Pole sana mpenzi


Lakini mpenzi umepitia mengi
MShukuru Mungu kwa yote
Na walokutendea hayo yote wasamehe
Na mwachie Mungu..
jipongeze kwa hatua uliyofikia

Girl
Your so brave to share your story
Thanx my dear..

niliapa kuwa sitawasamehe hasa yule wifi yangu, ila leo Mungu amenifundisha kusamehe!!! nawapenda sana! najua dhahabu safi lazima ipite kwenye moto!!
 
Pole sana dearest.Haya mambo yanatokea sana kwenye jamii zetu lakini siku zote Mungu huwasimamia wenye machungu na wanaoonewa.
I believe kupitia experience hiyo mbaya utakuwa umejifunza jinsi ya kuishi na kuwatreat yatima na hivyo uwe mfano wa kuigwa na wengine.
Ubarikiwe.
 
Pole sana Suzy kwa mkasa uliokupata, wengi tumepitia mkasa kama wako na hatupendi kukumbushwa yale ya nyuma kuepusha kutonesha vidonda vilivyopona!
 
Hadi machozi.Pole sana sasa Susy.

Kila kitu hutokea kwa sababu fulani duniani.
Wanasema malipo ni hapa duniani,ndo yaliyowakuta hao ndugu zenu.

Jitahidi usahau yaliyopita na ugange yajayo. Mungu yu pamoja nanyi nyote.
 
Pole sana mpendwa!Ila yote yale yanabaki kua historia na somo kwako... kwahiyo mshukuru Mungu maana amekutoa huko!Sijui roho mbaya zitatuisha lini wanadamu sie kwakweli!
 
Pole sana Suzy kwa mkasa uliokupata, wengi tumepitia mkasa kama wako na hatupendi kukumbushwa yale ya nyuma kuepusha kutonesha vidonda vilivyopona!

kuna andiko linasema shuhudia tuone kama unampenda Mungu, lazima niwaeleze nilipotoka na nilipo sasa ni kwa mkono wa Mungu tu!!
 
Pole sana mpendwa!Ila yote yale yanabaki kua historia na somo kwako... kwahiyo mshukuru Mungu maana amekutoa huko!Sijui roho mbaya zitatuisha lini wanadamu sie kwakweli!

Lizy hapa ndipo ninajiuliza kwani kipindi kile chote Mungu alikuwa wapi?? lakini leo nakuja kujua jambo tu, ya kwamba hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea!! na Mungu huinua maadui kwa sababu maalum!!
 
Hadi machozi.Pole sana sasa Susy.

Kila kitu hutokea kwa sababu fulani duniani.
Wanasema malipo ni hapa duniani,ndo yaliyowakuta hao ndugu zenu.

Jitahidi usahau yaliyopita na ugange yajayo. Mungu yu pamoja nanyi nyote.

nilishasahau dia, Lizzy ndio kanikumbusha.
 
Asalam aleikum!!!

Bwana Yesu asifiwe!!

Nimesoma thread ya Lizy kuhusu unyanyasaji wa watoto ikanikumbusha mbali sana, hakika imenitoa machozi!!

Nakumbuka miaka ya nyuma sana wakati nikiwa na miaka 4 tu, mama yangu alifariki kwa ugonjwa wa cancer, hatukukaa hata mwaka baba naye alifariki na ugonjwa wa figo, hapo ndipo nilipotamani dunia igeuke chini juu.

Nakumbuka dada yangu mkubwa alikuwa ndio kwanza yupo 4m3 na kaka yangu ambaye nafatana naye alikua yupo darasa la pili, tulinyang'anywa mali zote za baba yetu, tena tukarudishwa kijijini kabisa ambapo baba aliweka mifugo yake, baada ya muda bb mdg akaja akachukua ngombe wote wakagawana na watoto wa mama mkubwa.

Hakuna aliyetujali, tuliachiwa mbuzi tu pale kijijini, nakumbuka kaka yangu ilibidi aache shule aanze kuchunga hao mbuzi kwa taabu, mimi nilikua nachota maji na kufagia, hakuna aliyejua tunakula nini, tunavaa nini wala tunalala vipi.

Nakumbuka wale rafikize baba wakamlipia dada yangu ada kwa kuchangiwa na kijiji dada akarudi shule, jirani yetu mmoja akasema tuchanganye mbuzi zetu na zake ili kaka asiende kuchunga awe anaenda shule.

kutokana na baridi ya mkoa ambao tulikuwe, na hatukuwa na blanket siku moja nilishikwa na naimonia ikiambatana na homa kali, kaka yangu akapanda gari kwenda mjini kumwambia baba mdogo, baba mdogo akamwambia kama baba yake na mama yake wamekufa yeye anafaida gani, mwache afe akupunguzie taabu na ww!! kaka alirudi kijijini na kuomba msaada ndipo nikapelekwa hospitali na kulazwa, ikimlazimu kufanya vibarua vya kulima wakati akiwa mdogo ili kutupatia fedha za matumizi na kuniuguza.

kaka yangu mtoto wa m.mkubwa akaoa kule kijijini akatuchukua lakini niliona bora tulivyokuwa tunakaa wenyewe maana wifi alitunyanyasa sana, jina langu lilikua mbwa, nakumbuka alikua ananiita hivi, "we mbwa mkubwa njoo hapa" ukifika tu unakibao alafu ndio maagizo mengine yanaendelea!!!

Baada ya muda wale wote waliotudhulumu alikufa mmoja baada ya mwingine, wale waliotunyanyasa kwa chakula leo ndio wanatuomba chakula, waliotulaza chini leo wanatembea wameinamisha vichwa vyao!!

"usimnyanyase yatima wala kumuonea mjane, mkono wa Mungu utakuwa juu yako"
Kwa maelezo yako Suzy inaonekana ulipitia ktk hali ngumu ya maisha, lakini bado hujaeleza ilikuwaje ukafanikiwa kutokea.
Kwa ufupi tena tupe picha inaweza kusaidia watu wengine wenye hali mbaya ili wasikate tamaa!!!!!!!! Ubarikiwe!!


 
Mungu ni baba wa Yatima na ni Mume wa wajane. Poleni sana Suzy. Ila namshukuru Mungu kwa sababu fadhili zake zilikuwa pamoja nanyi. Ndio maana amewaandalia meza machoni pa watesi wenu.

Songa mbele, na pia kumbuka Mungu aliwapitisha hapo ili mje kuwa msaada kwa Yatima na watu wengine wanaoteseka. Msiache kabisa kufanya utumishi huo.
UBARIKIWE
Hicho kikombe cha chai unakunywaga mwenyewe tuu??????? Ubarikiwe!!!!!!
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom