HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,399
- 6,077
Mwaka 2002 mkoa wa Mbeya kabla haujagawanywa kuwa mikoa miwili yani Songwe na Mbeya ilikuwa asubuhi nilipopokea simu kunitaarifu kuwa ndugu yangu amekutwa amechunwa ngozi kijiji cha Isansa wilaya ya Mbozi.
Nilikurupuka kwenda eneo la tukio nikakuta watu wengi wakisubiri polisi wafike. Nilipomtazama mwili wake wote ulikuwa mwekundu na hakuwa na jeraha lolote zaidi ya uvimbe kisogoni.
Ngozi ilivuliwa kuanzia shingoni hadi miguuni kama nguo vile maana walivyokuwa wanachuna unapigwa na kitu kizito kichwani kabla haujafariki wanakuchoma sindano ngozi inaumuka inaachana na mwili hivyo wanakuja kukata shingoni na huku mikononi alafu wanaivua kama nguo huku ukiendelea kutapatapa. Baada ya hapo wanaiweka dawa isiharibike then wanasepa hivyo tulikuta ashafariki muda mrefu.
Polisi walikuja na kuruhusu tukazike. Baada ya siku nne wale wachunaji walikuwa wako Vwawa ambayo sasa hivi ni makao makuu ya mkoa wa Songwe Wilaya ya Mbozi.
Walikuwa guest house wakisubiri wafanye biashara USD 30,000. Wakati mhudumu wa guest anafanya usafi akasikia harufu isiyo ya kawaida na kwenda kuripoti ndipo walipokamatwa na kupelekwa kituoni.
Ngozi ilikuwa imehifadhiwa kwenye kopo. Wengi tulikusanyika kushuhudia lile tukio, wakaitoa nje watu tukaiona.
Taarifa zikasambaa kuwa kumbe ni boss mmoja pale Vwawa ndiye ilikuwa biashara yake. Alikuwa na vituo vya mafuta, shule, magari nk
Inaaminika Polisi walipoenda akawapa bakishishi wakapiga kimya. Matukio ya uchunaji yaliendelea baadaye yakapotea hadi leo. Wapo waliodai ngozi ile ilikuwa inauzwa Congo.
Hadi leo sijui wale watuhumiwa walifungwa wapi lakini sasa hivi ni full amani hakuna tena uchunaji.
Nilikurupuka kwenda eneo la tukio nikakuta watu wengi wakisubiri polisi wafike. Nilipomtazama mwili wake wote ulikuwa mwekundu na hakuwa na jeraha lolote zaidi ya uvimbe kisogoni.
Ngozi ilivuliwa kuanzia shingoni hadi miguuni kama nguo vile maana walivyokuwa wanachuna unapigwa na kitu kizito kichwani kabla haujafariki wanakuchoma sindano ngozi inaumuka inaachana na mwili hivyo wanakuja kukata shingoni na huku mikononi alafu wanaivua kama nguo huku ukiendelea kutapatapa. Baada ya hapo wanaiweka dawa isiharibike then wanasepa hivyo tulikuta ashafariki muda mrefu.
Polisi walikuja na kuruhusu tukazike. Baada ya siku nne wale wachunaji walikuwa wako Vwawa ambayo sasa hivi ni makao makuu ya mkoa wa Songwe Wilaya ya Mbozi.
Walikuwa guest house wakisubiri wafanye biashara USD 30,000. Wakati mhudumu wa guest anafanya usafi akasikia harufu isiyo ya kawaida na kwenda kuripoti ndipo walipokamatwa na kupelekwa kituoni.
Ngozi ilikuwa imehifadhiwa kwenye kopo. Wengi tulikusanyika kushuhudia lile tukio, wakaitoa nje watu tukaiona.
Taarifa zikasambaa kuwa kumbe ni boss mmoja pale Vwawa ndiye ilikuwa biashara yake. Alikuwa na vituo vya mafuta, shule, magari nk
Inaaminika Polisi walipoenda akawapa bakishishi wakapiga kimya. Matukio ya uchunaji yaliendelea baadaye yakapotea hadi leo. Wapo waliodai ngozi ile ilikuwa inauzwa Congo.
Hadi leo sijui wale watuhumiwa walifungwa wapi lakini sasa hivi ni full amani hakuna tena uchunaji.