Sitakuja ludia tena huu ujasiri

Mkimuyangu

JF-Expert Member
Oct 5, 2022
1,054
1,929
Hii ni stori ya kweli kabisa, iliyonifanya nichungulie mauti.

Samahani kwa uandishi mbovu, kwa asili mimi ni muhehe,najiamini sana,sina hata chembe ya woga,linapokujaga swala la woga,nikisema Uoga una tofauti yake, mfano mtu mwingine anaogopa kutembea usiku,au kulala peke yake,na kunakuogopa vitu vya giza kama wachawi au majambazi

Lakini kwangu mimi hakuna ninachoogopa iwe popote pale,nakumbuka kunasiku tulisafiri na boti kupitia ziwa nyasa,kutoka Malawi kwenda Mozambique,tulipofika mwisho wa safari,kila abiria akashika njia yake kwenda kwake,na palikuwa hamna guest,basi nikatoa mizigo yangu nikaweka kwenye mchanga,umbali kidogo kutoka kwenye maji,nikaokota vipande vya miwa vikavu,nikawasha moto,mpaka asubuhi,hiyo unajikuta unashindana na usingizi,hutaki kulala sababu ya usalama wako, na usingizi nao unataka ulale

Siku yenyewe niliyoamua kujivua nyota au kujishusha cheo ilikuwa hivi, kipindi cha korona Mozambique walifunga mipaka,ikawa hakuna kusafiri,tukajikuta inabidi kusafiri kama wezi,yaani mnapita mpakani usiku wa manane kama wezi,mnachokifanya mnakula diri na baadhi ya maskari,mnawapa hera,halafu wanakuja kuwavusha usiku,na wanawaambia ukisikia shaba,utajijua mwenyewe na mmewapa hela

Sasa siku hiyo nilijikuta niko peke yangu msafiri baada ya kufika border,ambayo inabidi nivuke,nikapiga hesabu hawa nikila nao dili la kunivusha watanipiga hela ndefu,

Ikanibidi niamke kama saa nane ya usiku ya Tanzania kwa ajili ya kuanza safari,ukumbuka niko upande wa Tanzania,nikapita freshi uhamiaji ya Tanzania,huku walinzi wakiwa wamelala,nikavuka mto ruvuma ambao unatenganiza mpaka,nikaingia upande wa Mozambique,hapa kuna taa zinawaka,kwa hiyo mwanga ni mkubwa,nikawa napita kwenye vivuli ya miti,nikafanikiwa kuipita border bila kikwazo,ninakokwenda kama umbali wa mita 500 kuna Camp ya askari,ambapo getini kuna maskari,ikabidi niingie porini ili nikatoke mbele yake,ni msituni,nikajikuta natokea kijijini,hapo nimeshakata kama kilomita moja na nusu,inabidi nitembee ya miguu kilomita 20,huko ndiyo nitakuwa salama na ni katikati ya mbuga.

Kuangalia saa inasema ni kama saa tisa na madakika,nikasema hapa nikizubaa hawa jamaa wakinikuta azabu yao ni viboko,ngoja nieendele mbele,mapambazuko yanikutie msituni,nikakata kama nusuu saa hivi,niseme ndiyo naviacha vijiji sasa nitokomee msituni,nikakuta nyumba moja kuna watu wako inje,wakastuka kuniona,ikabidi nijisalimishe kwa kuwasalimia,maana hapa lugha inayotumika ni kiswahili na kiyao,ikabidi waniite na kuniuliza,kulikoni usiku huu,unaenda wapi?nikawadanganya, nimepungukiwa na nauli,nataka hiki kipande cha kilomita 50,nitembee ya miguu,
Wakaniambia kaa kwanza hapo,ili nianze kuhojiwa, sasa tunakuwaga na umafia wetu,unapoona umebanwa,kila ulichonacho ni silaa,ili upate huruma

Nilikuwa na mikate na juisi,nikwapa watoto zao wadogo,kuonyesha kama huruma na upendo,mala nyingi binadamu ukimuonyesha upendo mwanaye,anakuwaga na huluma

Wakaniambi,alikuja gavana wa jimbo,akawaambia mkiona mgeni yoyote amevuka border,inabidi mkaripoti polisi,maana yake ameleta corona,pili wakaniambia yaani huu mda unaotembea,unaenda kuliwa na simba sasa hivi,da!! nilihisi tumbo linaunguruma,wakaniambia itabidi ukae mpaka kuanze kupambazuka ndiyo uanze safari,hiyo mida ilikuwa inakwenda kwenye saa 10 kasoro,

Nikaka pale huku naota moto,ilipofika saa 11 kama na nusu hivi,wakaniambia unaweza kwenda,nilikata nikasema bado mapema

ilipofika saa 12 alfajiri safari ikaanza,naikata mbuga ya wanyama pana kilomita 20 kwenda kukipata kijiji kinachofuata,nikaanza kuacha nyumba,mala mashamba,likaanza pori kidogokidogo,badaye nikaanza kuona miguu ya wanyama wadogowadogo waliokuwa wanacheza usiku,baadaye nikaingia kwenye msitu ulioshonana,huku najitaidi kupambana na uchovu,begani nina begi la kilo kama 15,

Ikanipita pikipiki,ilikuwa na watu wamepakizana,ilikuwa kama saa 2 asubuhi hivi,kumetulia sana,ni sauti za ndege na nyan, ndiyo zinazosikika,

NIkawa naangalia nyayo zilizokanyagwa na pikipiki inamaana za jana,na nyayo zilizokanyaga pikipiki inamaana za leo,alhamdulilah nikakutana na unyayo wa tembo ambao umekanyaga juu ya pikipiki,inamaana huyu tembo kama ingekuwa vipi ningekutana naye,kidogo uwoga ukaanza kuniingia na uchovu ndani huku nikiwaza,kama nitakutana nao nifanyaje?kupanda juu ya mti haiwezekani labda uwe mti mkubwa kama mbuyu,kukimbia nasikia tembo ana mbiyo sana,ikabidi niwe namuomba Mungu tu

Mara nikakutana na unyayo wa simba ambao umekanyaga,juu ya pikipiki,kwa kweli nilichanganyikiwa na kuanza kujilaumu kwa ujasiri wangu,nikasema hapa leo sijui kama kunakupona, nikakata shauri kama litatokea gari linakokwenda kule ninakotokea,itabidi nipande tu,bila kujali nitakamatwa au vipi huko nitakakokwenda,kila nikikata msitu naona haupungui wala hauongezeki inamaana niko katikati ya msitu,

Badaye sana nikaona msitu unapungua kidogokidogo mpaka nilipoanza kuona mashamba ya watu,nikajua da leo nimepona kufa,na huu ujasiri wangu najivua kuanzia leo,siyo kila kitu ni cha kukifanyia ujasiri
 
Mbona kama huna akili
Ila weunaita ujasiri!!
Inategemeana umezaliwaje,,kuna wengine ni watoto wa mafisadi,wengine walishatafuniwa,wengine walishajikatia tamaa,wengine wanandoto ya kutokutaka watoto zao waje wawe maskini kama wao walivyozaliwa maskini,

Unaweza kumuita mtu unavyotaka sababu umejificha nyuma ya simu lakini ukweli unaujua mwenyewe,katika utafutaji kunavisa vingi sana hiki changu cha mtoto lakini kama wewe mtoto wa mama utanichukulia kama unavyojisikia
 
Hii ni stori ya kweli kabisa, iliyonifanya nichungulie mauti.

Samahani kwa uandishi mbovu, kwa asili mimi ni muhehe,najiamini sana,sina hata chembe ya woga,linapokujaga swala la woga,nikisema Uoga una tofauti yake, mfano mtu mwingine anaogopa kutembea usiku,au kulala peke yake,na kunakuogopa vitu vya giza kama wachawi au majambazi

Lakini kwangu mimi hakuna ninachoogopa iwe popote pale,nakumbuka kunasiku tulisafiri na boti kupitia ziwa nyasa,kutoka Malawi kwenda Mozambique,tulipofika mwisho wa safari,kila abiria akashika njia yake kwenda kwake,na palikuwa hamna guest,basi nikatoa mizigo yangu nikaweka kwenye mchanga,umbali kidogo kutoka kwenye maji,nikaokota vipande vya miwa vikavu,nikawasha moto,mpaka asubuhi,hiyo unajikuta unashindana na usingizi,hutaki kulala sababu ya usalama wako, na usingizi nao unataka ulale

Siku yenyewe niliyoamua kujivua nyota au kujishusha cheo ilikuwa hivi, kipindi cha korona Mozambique walifunga mipaka,ikawa hakuna kusafiri,tukajikuta inabidi kusafiri kama wezi,yaani mnapita mpakani usiku wa manane kama wezi,mnachokifanya mnakula diri na baadhi ya maskari,mnawapa hera,halafu wanakuja kuwavusha usiku,na wanawaambia ukisikia shaba,utajijua mwenyewe na mmewapa hela

Sasa siku hiyo nilijikuta niko peke yangu msafiri baada ya kufika border,ambayo inabidi nivuke,nikapiga hesabu hawa nikila nao dili la kunivusha watanipiga hela ndefu,

Ikanibidi niamke kama saa nane ya usiku ya Tanzania kwa ajili ya kuanza safari,ukumbuka niko upande wa Tanzania,nikapita freshi uhamiaji ya Tanzania,huku walinzi wakiwa wamelala,nikavuka mto ruvuma ambao unatenganiza mpaka,nikaingia upande wa Mozambique,hapa kuna taa zinawaka,kwa hiyo mwanga ni mkubwa,nikawa napita kwenye vivuli ya miti,nikafanikiwa kuipita border bila kikwazo,ninakokwenda kama umbali wa mita 500 kuna Camp ya askari,ambapo getini kuna maskari,ikabidi niingie porini ili nikatoke mbele yake,ni msituni,nikajikuta natokea kijijini,hapo nimeshakata kama kilomita moja na nusu,inabidi nitembee ya miguu kilomita 20,huko ndiyo nitakuwa salama na ni katikati ya mbuga.

Kuangalia saa inasema ni kama saa tisa na madakika,nikasema hapa nikizubaa hawa jamaa wakinikuta azabu yao ni viboko,ngoja nieendele mbele,mapambazuko yanikutie msituni,nikakata kama nusuu saa hivi,niseme ndiyo naviacha vijiji sasa nitokomee msituni,nikakuta nyumba moja kuna watu wako inje,wakastuka kuniona,ikabidi nijisalimishe kwa kuwasalimia,maana hapa lugha inayotumika ni kiswahili na kiyao,ikabidi waniite na kuniuliza,kulikoni usiku huu,unaenda wapi?nikawadanganya, nimepungukiwa na nauli,nataka hiki kipande cha kilomita 50,nitembee ya miguu,
Wakaniambia kaa kwanza hapo,ili nianze kuhojiwa, sasa tunakuwaga na umafia wetu,unapoona umebanwa,kila ulichonacho ni silaa,ili upate huruma

Nilikuwa na mikate na juisi,nikwapa watoto zao wadogo,kuonyesha kama huruma na upendo,mala nyingi binadamu ukimuonyesha upendo mwanaye,anakuwaga na huluma

Wakaniambi,alikuja gavana wa jimbo,akawaambia mkiona mgeni yoyote amevuka border,inabidi mkaripoti polisi,maana yake ameleta corona,pili wakaniambia yaani huu mda unaotembea,unaenda kuliwa na simba sasa hivi,da!! nilihisi tumbo linaunguruma,wakaniambia itabidi ukae mpaka kuanze kupambazuka ndiyo uanze safari,hiyo mida ilikuwa inakwenda kwenye saa 10 kasoro,

Nikaka pale huku naota moto,ilipofika saa 11 kama na nusu hivi,wakaniambia unaweza kwenda,nilikata nikasema bado mapema

ilipofika saa 12 alfajiri safari ikaanza,naikata mbuga ya wanyama pana kilomita 20 kwenda kukipata kijiji kinachofuata,nikaanza kuacha nyumba,mala mashamba,likaanza pori kidogokidogo,badaye nikaanza kuona miguu ya wanyama wadogowadogo waliokuwa wanacheza usiku,baadaye nikaingia kwenye msitu ulioshonana,huku najitaidi kupambana na uchovu,begani nina begi la kilo kama 15,

Ikanipita pikipiki,ilikuwa na watu wamepakizana,ilikuwa kama saa 2 asubuhi hivi,kumetulia sana,ni sauti za ndege na nyan, ndiyo zinazosikika,

NIkawa naangalia nyayo zilizokanyagwa na pikipiki inamaana za jana,na nyayo zilizokanyaga pikipiki inamaana za leo,alhamdulilah nikakutana na unyayo wa tembo ambao umekanyaga juu ya pikipiki,inamaana huyu tembo kama ingekuwa vipi ningekutana naye,kidogo uwoga ukaanza kuniingia na uchovu ndani huku nikiwaza,kama nitakutana nao nifanyaje?kupanda juu ya mti haiwezekani labda uwe mti mkubwa kama mbuyu,kukimbia nasikia tembo ana mbiyo sana,ikabidi niwe namuomba Mungu tu

Mara nikakutana na unyayo wa simba ambao umekanyaga,juu ya pikipiki,kwa kweli nilichanganyikiwa na kuanza kujilaumu kwa ujasiri wangu,nikasema hapa leo sijui kama kunakupona, nikakata shauri kama litatokea gari linakokwenda kule ninakotokea,itabidi nipande tu,bila kujali nitakamatwa au vipi huko nitakakokwenda,kila nikikata msitu naona haupungui wala hauongezeki inamaana niko katikati ya msitu,

Badaye sana nikaona msitu unapungua kidogokidogo mpaka nilipoanza kuona mashamba ya watu,nikajua da leo nimepona kufa,na huu ujasiri wangu najivua kuanzia leo,siyo kila kitu ni cha kukifanyia ujasiri
Jasiri haachi asili yake. Usikubali kuwa fala
 
Inategemeana umezaliwaje,,kuna wengine ni watoto wa mafisadi,wengine walishatafuniwa,wengine walishajikatia tamaa,wengine wanandoto ya kutokutaka watoto zao waje wawe maskini kama wao walivyozaliwa maskini,

Unaweza kumuita mtu unavyotaka sababu umejificha nyuma ya simu lakini ukweli unaujua mwenyewe,katika utafutaji kunavisa vingi sana hiki changu cha mtoto lakini kama wewe mtoto wa mama utanichukulia kama unavyojisikia
Muyangu ndisuka undihongesa ndikosie swe
Tumefanya risk nyingi ila sio kukatiza kwenye msitu wa Simba wakati una mbadala.
 
hata sijamaliza kusoma nimegundua wewe ni mwoga sana na mwongo sana
1.jasiri hawezi kukoka moto anapambana na baridi = mwoga
2.umeamuka saa 8 usiku , kilometers 20 kuzitembea kwa mguu !!!?? kwa saa 1 = uongo

n.k n.k
 
Hii ni stori ya kweli kabisa, iliyonifanya nichungulie mauti.

Samahani kwa uandishi mbovu, kwa asili mimi ni muhehe,najiamini sana,sina hata chembe ya woga,linapokujaga swala la woga,nikisema Uoga una tofauti yake, mfano mtu mwingine anaogopa kutembea usiku,au kulala peke yake,na kunakuogopa vitu vya giza kama wachawi au majambazi

Lakini kwangu mimi hakuna ninachoogopa iwe popote pale,nakumbuka kunasiku tulisafiri na boti kupitia ziwa nyasa,kutoka Malawi kwenda Mozambique,tulipofika mwisho wa safari,kila abiria akashika njia yake kwenda kwake,na palikuwa hamna guest,basi nikatoa mizigo yangu nikaweka kwenye mchanga,umbali kidogo kutoka kwenye maji,nikaokota vipande vya miwa vikavu,nikawasha moto,mpaka asubuhi,hiyo unajikuta unashindana na usingizi,hutaki kulala sababu ya usalama wako, na usingizi nao unataka ulale

Siku yenyewe niliyoamua kujivua nyota au kujishusha cheo ilikuwa hivi, kipindi cha korona Mozambique walifunga mipaka,ikawa hakuna kusafiri,tukajikuta inabidi kusafiri kama wezi,yaani mnapita mpakani usiku wa manane kama wezi,mnachokifanya mnakula diri na baadhi ya maskari,mnawapa hera,halafu wanakuja kuwavusha usiku,na wanawaambia ukisikia shaba,utajijua mwenyewe na mmewapa hela

Sasa siku hiyo nilijikuta niko peke yangu msafiri baada ya kufika border,ambayo inabidi nivuke,nikapiga hesabu hawa nikila nao dili la kunivusha watanipiga hela ndefu,

Ikanibidi niamke kama saa nane ya usiku ya Tanzania kwa ajili ya kuanza safari,ukumbuka niko upande wa Tanzania,nikapita freshi uhamiaji ya Tanzania,huku walinzi wakiwa wamelala,nikavuka mto ruvuma ambao unatenganiza mpaka,nikaingia upande wa Mozambique,hapa kuna taa zinawaka,kwa hiyo mwanga ni mkubwa,nikawa napita kwenye vivuli ya miti,nikafanikiwa kuipita border bila kikwazo,ninakokwenda kama umbali wa mita 500 kuna Camp ya askari,ambapo getini kuna maskari,ikabidi niingie porini ili nikatoke mbele yake,ni msituni,nikajikuta natokea kijijini,hapo nimeshakata kama kilomita moja na nusu,inabidi nitembee ya miguu kilomita 20,huko ndiyo nitakuwa salama na ni katikati ya mbuga.

Kuangalia saa inasema ni kama saa tisa na madakika,nikasema hapa nikizubaa hawa jamaa wakinikuta azabu yao ni viboko,ngoja nieendele mbele,mapambazuko yanikutie msituni,nikakata kama nusuu saa hivi,niseme ndiyo naviacha vijiji sasa nitokomee msituni,nikakuta nyumba moja kuna watu wako inje,wakastuka kuniona,ikabidi nijisalimishe kwa kuwasalimia,maana hapa lugha inayotumika ni kiswahili na kiyao,ikabidi waniite na kuniuliza,kulikoni usiku huu,unaenda wapi?nikawadanganya, nimepungukiwa na nauli,nataka hiki kipande cha kilomita 50,nitembee ya miguu,
Wakaniambia kaa kwanza hapo,ili nianze kuhojiwa, sasa tunakuwaga na umafia wetu,unapoona umebanwa,kila ulichonacho ni silaa,ili upate huruma

Nilikuwa na mikate na juisi,nikwapa watoto zao wadogo,kuonyesha kama huruma na upendo,mala nyingi binadamu ukimuonyesha upendo mwanaye,anakuwaga na huluma

Wakaniambi,alikuja gavana wa jimbo,akawaambia mkiona mgeni yoyote amevuka border,inabidi mkaripoti polisi,maana yake ameleta corona,pili wakaniambia yaani huu mda unaotembea,unaenda kuliwa na simba sasa hivi,da!! nilihisi tumbo linaunguruma,wakaniambia itabidi ukae mpaka kuanze kupambazuka ndiyo uanze safari,hiyo mida ilikuwa inakwenda kwenye saa 10 kasoro,

Nikaka pale huku naota moto,ilipofika saa 11 kama na nusu hivi,wakaniambia unaweza kwenda,nilikata nikasema bado mapema

ilipofika saa 12 alfajiri safari ikaanza,naikata mbuga ya wanyama pana kilomita 20 kwenda kukipata kijiji kinachofuata,nikaanza kuacha nyumba,mala mashamba,likaanza pori kidogokidogo,badaye nikaanza kuona miguu ya wanyama wadogowadogo waliokuwa wanacheza usiku,baadaye nikaingia kwenye msitu ulioshonana,huku najitaidi kupambana na uchovu,begani nina begi la kilo kama 15,

Ikanipita pikipiki,ilikuwa na watu wamepakizana,ilikuwa kama saa 2 asubuhi hivi,kumetulia sana,ni sauti za ndege na nyan, ndiyo zinazosikika,

NIkawa naangalia nyayo zilizokanyagwa na pikipiki inamaana za jana,na nyayo zilizokanyaga pikipiki inamaana za leo,alhamdulilah nikakutana na unyayo wa tembo ambao umekanyaga juu ya pikipiki,inamaana huyu tembo kama ingekuwa vipi ningekutana naye,kidogo uwoga ukaanza kuniingia na uchovu ndani huku nikiwaza,kama nitakutana nao nifanyaje?kupanda juu ya mti haiwezekani labda uwe mti mkubwa kama mbuyu,kukimbia nasikia tembo ana mbiyo sana,ikabidi niwe namuomba Mungu tu

Mara nikakutana na unyayo wa simba ambao umekanyaga,juu ya pikipiki,kwa kweli nilichanganyikiwa na kuanza kujilaumu kwa ujasiri wangu,nikasema hapa leo sijui kama kunakupona, nikakata shauri kama litatokea gari linakokwenda kule ninakotokea,itabidi nipande tu,bila kujali nitakamatwa au vipi huko nitakakokwenda,kila nikikata msitu naona haupungui wala hauongezeki inamaana niko katikati ya msitu,

Badaye sana nikaona msitu unapungua kidogokidogo mpaka nilipoanza kuona mashamba ya watu,nikajua da leo nimepona kufa,na huu ujasiri wangu najivua kuanzia leo,siyo kila kitu ni cha kukifanyia ujasiri
Hiyo nchi inamisitu mikubwa sana kama umeweza kukatiza huko na giza na nipeke yako nakushauri tu usirudie tena. Binadamu unatafuta kwa shida na hatarishi hivyo halafu mjinga mmoja anakuja kuchukuwa kitu chako ulichojinunulia kiurahisi tu! Mungu anisamehe nisikutane nae mwivi wangu.
 
Ungetupa kisa kizima cha hizi hustle zako ingenoga sana. Ni magendo ulikua unafanya?
 
hata sijamaliza kusoma nimegundua wewe ni mwoga sana na mwongo sana
1.jasiri hawezi kukoka moto anapambana na baridi = mwoga
2.umeamuka saa 8 usiku , kilometers 20 kuzitembea kwa mguu !!!?? kwa saa 1 = uongo

n.k n.k
Labda hujaelewa vizuri au makosa yangu ya uandishi, safari inaanza saa 8 ya usiku kuivuka border ya Tanzania, kwa wazoefu wa border huwa hazikai kalibu na raia, boda zote, kwa hiyo nimetoka kijijini naipitia immigration ya Tanzania, halafu naenda kupita mpakani, ambao ni mto ruvuma,

Halafu natokea immigration ya Mozambique, naingia kijijini, naikwepa kambi ya polisi kupitia polini, hapo ni kama nusu saa, kumbuka kuna wakati inabidii niingie porini, natokea kijijini tena, halafu nenda kusimamishwa vijiji vya mwisho kwa mahojiano, hapo nakuwa kama mimetembea kilomita 2.5, baada ya kuambiwa nianze safari, ndiyo nakutana na hiyo mikasa ni kama kilomita 17.5 nilitembea wastani wa masaa 4.na nusu hivi
 
Nachojua Simba hua hali watu hovyo hovyo na Tembo wala hana tatizo na watu kama hajachokozwa au hajahisi hatari pia Nyati

Kwa hivyo ulikua salama tu sema mindi yako ilikuaminisha kua unapita katika bonde la uvuli wa mauti na hvyo kukujaza hofu kubwa.

NB: Nimeishi Ngorongoro na Ruaha kwa vipindi tofauti.
 
Hii stori nishaisikia kwenye kijiwe cha kahawa mwaka 2003, mzee kubali ukatae umekop na kupest haijawahi kukukuta wewe ni mwongo🙌🏻
 
Back
Top Bottom